Serikali imwangalie Prof. Assad isimwache ateseke hivi. Huyu jamaa hayupo sawa

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Anahitaji ushauri wa kisaikolojia. Mpaka leo bado analia akikumbuka alivyoondolewa ofisini. Akiulizwa tu hilo jambo analia sana. Ananung'unika, anasononeka, anahuzunika, anaghadhibika, anatatajika.

Prof mpaka kufika hapo ni wazi ana akili za darasani. Ila emotional intelligence ndo shida. Prof miaka mitatu bado anaugua sana akiugulia ile nafasi. Sisi wengine tulishaondolewa makazini kwa vyeti fake n.k na maisha yakaendelea tu.

Wengine tuliondolewa sababu ya uwezo ila vyetu tulikuwa navyo tukasema tu aaargh sikuzaliwa niwe Mkurugenzi au Katibu xxxxx.

Soma pia: Prof. Mussa Assad: Taarifa ya utenguzi wangu nilipewa siku moja kabla

Kwa Prof Assad. Imekuwa tofauti. Bado analalamika. Serikali iingilie kati. Imsaidie akae sawa kihisia na kiakili. Ni wazi hili suala lilimuathiri sana. Asiachwe peke yake. Na kama ana madai Samia mlipe Prof apumzike. Pia apewe mtaalamu wa saikolojia amwambie haya ni maisha tu . Kwani

KUKATIKA KWA MPINI SI MWISHO WA KULIMA. asiumie bado ana maisha na anaweza pewa cheo kingine. Kumfariji asiachwe hivi hivi please. Afya ya akili is real.
 
Prof tatizo lake kubwa ni fundamentalist, yaani anachokiamini huwezi mbadilisha, hakufaa kuwa kiongozi. Naamini hata vetting ilikuwa mbaya ila nadhani Dkt Kikwete atakuwa alilazimisha
 
Ndugu Komeo la mbao,vipi afikiriwe asiye na maslahi na mafisadi,wezi,watekaji na wauaji,hii inaingia akilini.Huenda angeenda na na mitazamo yao usingefika hapa kumsemea.
 
Prof. Assad Sasa zamu yake kwenda kujiajiri.
Mh.Samia mlipe stahiki zake Prof Assad akajiajiri.
Siku nyingine ajifunze ukichagua kusimamia unacho amini hata kama ikibidi upishane na boss wako ukubali matokeo yake. Ukubali kuteseka sababu ya itikadi zako, na matokeo ya maamuzi yako.
Ukijiona wewe mlaini basi huna budi kufuata matakwa ya boss wako.
Kuna kiongozi alisema Katiba ni kijitabu tu, hivyo Assad alikosea kuitegemea Katiba pekee.
 
Wewe Mwehu jaribu kuandika vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…