Serikali ina wajibu wa kuzuia matangazo ya kibiashara ya kidini/imani kwenye vyombo vya habari kulinda raia wake

Serikali ina wajibu wa kuzuia matangazo ya kibiashara ya kidini/imani kwenye vyombo vya habari kulinda raia wake

Je, unafahamu kwamba serikali ni mnufaika mkubwa wa uwepo wa hizo dini na madhehebu yake kuliko wananchi wenyewe?

Uwepo wa hayo madhehebu na dini unasaidia kuwapumbaza na kufubaza fikra pevu za wananchi, na kupelekea wananchi kuamini katika uchawi, ushirikina au miujiza inayopatikana kwenye dini au kwenye Imani.

Ukitaka kuamini angalia jinsi hao viongozi wa dini wanavyopewa promo na kusapotiwa na serikali.
Upo sahihi mno mno. Na pia maisha yanapokuwa magumu wananchi wanapumbazwa kuwa ni ''kazi ya shetani'' hataki maendeleo yao. Magonjwa nayo tunaambiwa ni mapepo na wanga hivyo suluhisho ni kuombewa na siyo kwenda hospital. Bado huweka ''unabii'' wa kusema wameoteshwa fulani ndiye rais bora.
 
Upo sahihi mno mno. Na pia maisha yanapokuwa magumu wananchi wanapumbazwa kuwa ni ''kazi ya shetani'' hataki maendeleo yao. Magonjwa nayo tunaambiwa ni mapepo na wanga hivyo suluhisho ni kuombewa na siyo kwenda hospital. Bado huweka ''unabii'' wa kusema wameoteshwa fulani ndiye rais bora.
Je, ulishawahi kufikiria hao wananchi wenye matatizo mbalimbali wakiamua kuacha kwenda kwa manabii na madhehebu yao na kuamua kutafuta suluhisho kupitia serikali au watawala ni nini kitatokea?

Tutafakari kwa pamoja.
 
Je, ulishawahi kufikiria hao wananchi wenye matatizo mbalimbali wakiamua kuacha kwenda kwa manabii na madhehebu yao na kuamua kutafuta suluhisho kupitia serikali au watawala ni nini kitatokea?

Tutafakari kwa pamoja.
Mkuu hili swali la msingi sana likitafakariwa kwa kina!
 
Niliwahi kuambiwa hospitali na zahanati huwa zinabanwa kufanya matangazo ya kibiashara kuvutia wateja kwenye vyombo vya habari kwa sababu za kimaadili ya afya, sina uhakika kama kuna sheria au kanuni rasmi katika kuratibu matangazo yao lakini huu ni utaratibu ambao ungefaa zaidi kwa "huduma za kidini"

Vyombo vingi vya habari(radio na TV) siku hizi vina matangazo ya kibiashara ya makanisa mbalimbali hasa haya ya manabii wa kisasa yakihamasisha watu kufika katika makanisani au katika mikutano yao kupata utatuzi wa shida zao na kubarakiwa. Pia kuna masheikh mbalimbali wamekuwa kwenye vyombo vya habari wakitangaza huduma zao.

Serikali izuie matangazo yote ya aina hiyo kwa sababu madai ya hayo makanisa na ma-sheikh ni mambo yasiyoweza kuthibitishwa kwa aina yoyote ile na serikali yenyewe. Yanaweza kuwa na mambo ya hadaa na utapeli tu au vinginevyo na serikali inao wajibu wa kuzuia raia wake kuingiziwa kwenye aina yoyote ile ya utapeli.
Hata waganga wa kienyeji hujitangaza kwenye vyombo vya habari kwa uhuru kabisa.
.......sisi kama serekali rumetenga fungus la Tsh. Billion kadhaa mwaka... Kwa ajiri ya utafiti, Ili kubaini kwanini jamii haipaendi kutumia huduma za hospitali, na wanaoenda hospital huwa wamechelewa...............
 
Je, ulishawahi kufikiria hao wananchi wenye matatizo mbalimbali wakiamua kuacha kwenda kwa manabii na madhehebu yao na kuamua kutafuta suluhisho kupitia serikali au watawala ni nini kitatokea?

Tutafakari kwa pamoja.
Huduma hazitatosha!
Pia tunazo emotion induced sicknesses nyingi ktk jamii zikitokana na changamoto za kiuchumi na kijamii.
 
Je, ulishawahi kufikiria hao wananchi wenye matatizo mbalimbali wakiamua kuacha kwenda kwa manabii na madhehebu yao na kuamua kutafuta suluhisho kupitia serikali au watawala ni nini kitatokea?

Tutafakari kwa pamoja.
Yatatokea mabadiliko ya kweli na viongozi watabadilika na kuwajibika kwa wananchi.
 
Je, ulishawahi kufikiria hao wananchi wenye matatizo mbalimbali wakiamua kuacha kwenda kwa manabii na madhehebu yao na kuamua kutafuta suluhisho kupitia serikali au watawala ni nini kitatokea?

Tutafakari kwa pamoja.
Watakosa wateja(wafuasi ) hivyo biashara (kanisa)litakufa na hivyo matangazo nayo yatoweka
 
Niliwahi kuambiwa hospitali na zahanati huwa zinabanwa kufanya matangazo ya kibiashara kuvutia wateja kwenye vyombo vya habari kwa sababu za kimaadili ya afya, sina uhakika kama kuna sheria au kanuni rasmi katika kuratibu matangazo yao lakini huu ni utaratibu ambao ungefaa zaidi kwa "huduma za kidini"

Vyombo vingi vya habari(radio na TV) siku hizi vina matangazo ya kibiashara ya makanisa mbalimbali hasa haya ya manabii wa kisasa yakihamasisha watu kufika katika makanisani au katika mikutano yao kupata utatuzi wa shida zao na kubarakiwa. Pia kuna masheikh mbalimbali wamekuwa kwenye vyombo vya habari wakitangaza huduma zao.

Serikali izuie matangazo yote ya aina hiyo kwa sababu madai ya hayo makanisa na ma-sheikh ni mambo yasiyoweza kuthibitishwa kwa aina yoyote ile na serikali yenyewe. Yanaweza kuwa na mambo ya hadaa na utapeli tu au vinginevyo na serikali inao wajibu wa kuzuia raia wake kuingiziwa kwenye aina yoyote ile ya utapeli.
Jumuiya za makanisa na misikiti nazo hulipa Kodi na zinatambulika kama 'legal persons' - zinaweza kushtaki na kushtakiwa. Hivyo, zina haki ya kunufaika na huduma zinazotolewa nchini. Ili zizuiwe ni lazima kuwe na uthibitisho wa huo utapeli. Sasa utathibitishaje kuwa hayo matangazo yanayotolewa ni ya kitapeli?
 
Jumuiya za makanisa na misikiti nazo hulipa Kodi na zinatambulika kama 'legal persons - zinaweza kushtaki na kushtakiwa. Hivyo, zina haki ya kunufaika na huduma zinazotolewa nchini. Ili zizuiwe ni lazima kiwe na utathibitisho wa huo utapeli. Sasa utathibitishaje kuwa hayo matangazo yanyotolewa ni ya kitapeli?
Hapana, taasisi za kidini hazilipi kodi.
Pia kuzuiwa kwao kutangaza ni kwa sababu za kimaadili(ethics) zaidi kama vile hospitali na law firms zinavyobanwa kufanya commercial marketing.
 
Niliwahi kuambiwa hospitali na zahanati huwa zinabanwa kufanya matangazo ya kibiashara kuvutia wateja kwenye vyombo vya habari kwa sababu za kimaadili ya afya, sina uhakika kama kuna sheria au kanuni rasmi katika kuratibu matangazo yao lakini huu ni utaratibu ambao ungefaa zaidi kwa "huduma za kidini"

Vyombo vingi vya habari(radio na TV) siku hizi vina matangazo ya kibiashara ya makanisa mbalimbali hasa haya ya manabii wa kisasa yakihamasisha watu kufika katika makanisani au katika mikutano yao kupata utatuzi wa shida zao na kubarakiwa. Pia kuna masheikh mbalimbali wamekuwa kwenye vyombo vya habari wakitangaza huduma zao.

Serikali izuie matangazo yote ya aina hiyo kwa sababu madai ya hayo makanisa na ma-sheikh ni mambo yasiyoweza kuthibitishwa kwa aina yoyote ile na serikali yenyewe. Yanaweza kuwa na mambo ya hadaa na utapeli tu au vinginevyo na serikali inao wajibu wa kuzuia raia wake kuingiziwa kwenye aina yoyote ile ya utapeli.
Mbona matangazo ya kubeti yanaendelea bila shida? Mwisho wa siku, raia si anapigwa tu kama anavyopigwa huko kwenye dini?
 
Mbona matangazo ya kubeti yanaendelea bila shida? Mwisho wa siku, raia si anapigwa tu kama anavyopigwa huko kwenye dini?
Matangazo ya betting huwa yana angalizo "bet kistaarabu", nchi nyingi duniani pia zinazuia matangazo ya kamari.
 
Hapana, taasisi za kidini hazilipi kodi.
Pia kuzuiwa kwao kutangaza ni kwa sababu za kimaadili(ethics) zaidi kama vile hospitali na law firms zinavyobanwa kufanya commercial marketing.
Nani kakwambia kwamba hazilipi kodi? Kusajiliwa wanalipia. Kununua kiwanja sehemu ya kujenga kanisa, shule, chuo, hospitali, benki etc wanalipia, vifaa vya ujenzi wanalipia, etc. Zimesamehewa tu kwa baadhi ya huduma zinazotoa. Ngoja niseme kwa upande wa Kanisa Katoliki kwa vile na mimi ni Mkatoliki. Kanisa Katoliki linatoa huduma mbalimbali. Mfano, lina shule mbalimbali na vyuo, benki na limeajiri watu wanaoendesha hizo shule, nyuo, benki na wanalipwa mshahara na wako entitled kwa mafao mbalimbali kama vile bima ya afya/maisha, NSSF na pension etc, unadhani nani anachangia hizo gharama? Labda niachie hapa kwanza.
 
Back
Top Bottom