Serikali inalogeka?

Baridijr

Member
Joined
May 27, 2009
Posts
36
Reaction score
0
Ndugu zangu wana JF naombeni msaada wenu kidogo, wakati nipo mdogo kule kijijini niliwahi kusikia kuwa serikali hairogeki nikakubaliana nao, lakini jinsi hali ilivyo hapa tz naanza kuamini kuwa kuna watu wameiloga serikali hadi haielewi majukumu yake kwa raia, kwa sababu mfano rahisi niliwahi kuhuzuria kikao kimoja wakati wa kampeni jk alitoa ahadi nyingi ambazo kwa mtu yoyote ni rahisi kutekeleza lkn hakuna kilichofanyika hadi leo zaidi ya kuongeza migogoro makazini na kupoteza ule umoja wa kibabe aliotupa mkapa, sasa hapo ndio ninapo uliza wana JF hii serikali haijarogwa
 


Kwani hujui kwamba pale Bagamoyo ndipo serikali yetu WaDanganyika inaporogewa?

Nenda pale mwakani kuanzia miezi ya June hadi Uchaguzi mkuu uone wanavyoiroga!

Kama mkuu wa nchi anaingia katika mikataba ya kujinufaisha yeye binafsi, kama Mkapa na Sumaye walivyofanya, je kurogwa kumesalia wapi tena?

Kama rasilimali za nchi, madini, viwanda, mbuga za wanyama zote ziko kwa wageni, na wageni hao wanawachomea makazi wananchi, kama kule Loliondo, ni kupi kurogwa zaidi ya huko?

Kama Mhindi-koko, tena FISADI, ndiye anayeongoza nchi kwa rimoti-kontrol, tumebakizwa wapi?

Serikali ya TANZANIA inarogwa kirahisi sana, na kwa sasa ni MSUKULE, na tunalishwa unga na mbilimbi, wakati wageni wanakula BATA!

Maskini kabisa sisi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…