Serikali ipige marufuku soda na vinywaji vyote vilivyoongezwa sukari

Serikali ipige marufuku soda na vinywaji vyote vilivyoongezwa sukari

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Juzi nimesikia NIHF ipo karibu kufirisika. Waziri anasema gharama za kutibu magonjwa yasiyoambukizwa ni kubwa sana. Ni magonjwa gani hayo yasiyoambukizwa?

Makubwa ni Kisukari, figo na high blood pressure. Haya kwa sehemu kubwa husababishwa na ulaji mbovu na sedentary lifestyle na yanahusiana sana. Matatizo mengi ya figo huletwa na kisukari.

Sasa kwa sehemu kubwa ulaji wa sukari na mafuta ndiyo visababishi vikubwa vya shida hiz. Inasemwa kuwa binadamu hakuumbwa kula sukari na mafuta kama anayokula leo.

Mambo hayo yana madhara kuliko vitu vikivyozoeleka kuwa na madhara kama pombe, sigara au bangi. Na mbaya zaidi, watu weusi tuna hatari zaidi ya kupata visukari na BP, lakini tumeiga ulaji wa kizungu wa mafuta na sukari nyingi.

Ni vyema, ili kuokoa jamii, serikali ikapiga marufuku soda na vinywaji vingine vilivyoongezwa sukari. Ikishindikana hilo, basi ilazimishe watengenezaji wa bidhaa hizo waweke onyo kama ilivyo kwenye sigara na pombe.
 
Vinywaji kama Soda vipewe kibandiko cha tahadhari kwa afya (Unywaji wa Soda ni hatari kwa Afya) kama ilivyo kwa sigara!

View attachment 2327218

Si rahisi kuamini kwa kuwa ni kinywaji kilichozoeleka karibu kila dunia nzima na anayekikosoa anatakiwa awe na rundo la hoja kushawishi watumiaji kudhibiti unywaji.

Lakini ni dhahiri kwamba soda imekuwa ikihusishwa na magonjwa lukuki; saratani, figo, mifupa, mstuko wa moyo.

Pia, unywaji wa vitu vya sukari pia unasababisha kuwa na unene, kitambi na upungufu wa madini muhimu mwilini. Soda haina lishe muhimu wala faida yoyote mwilini, ndivyo wanavyosema wataalamu.

Orodha hiyo ya athari za unywaji soda pia inahusisha kuzeeka haraka, kwa mujibu wa utafitiki uliofanywa na Chuo Kikuu cha Havard cha Uingereza.

Utafiti huo unaonyesha kuwa unywaji wa soda kwa kiwango kikubwa huongeza kasi ya uzee.

Unaeleza kuwa sumu zilizo kwenye soda zinazeesha mapema. Yaani kijana mdogo wa miaka 20 hujikuta anaonekana kama wa miaka 40.

“Soda inaponyweka inaongeza uzito wa nusu kilo kwa siku, hivyo watu wanaozinywa hunenepa mara mbili zaidi ya wale ambao hawanywi. Hivyo akinenepa kupita kiasi anasababisha mwili wake kuonekana na maumbile ya uzee,” unaeleza utafiti huo.

Pia, daktari wa kutoka Kenya, Theo Wangata anasema kunywa soda kwa wingi kunaweza kusababisha kisukari.

“Kunywa soda moja ni sawa na kunywa vijiko 10 vya sukari, baada ya kunywa sukari hupanda sana mwilini na kongosho hutoa homoni ya insulini nyingi. Muda unavyozidi kwenda insulini huendelea kuishiwa nguvu (insulin resisitance) na hali hii husababisha wewe kupatwa na ugonjwa wa kisukari,”anasema.

Takwimu zinaonyesha kuwa binadamu wa kawaida hunywa vinywaji visivyolewesha, kama soda, chupa 42 kwa mwaka (sawa na gramu 1,638 ya sukari au vijiko 92 vya sukari). Tafiti pia zinaeleza kuwa mtu anayekunywa soda moja kwa siku, anakunywa zaidi ya galoni au dumu 56 za soda kwa mwaka.

“Soda ina kemikali inayoitwa phosporic acid ambayo huzuia mwili kuchukua madini ya calcium kwenye chakula. Madini hayo ni muhimu kwa ajili ya mifupa na misuli yenye afya kwenye mwili wa binadamu,” anasema daktari bingwa kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Delilah Kimambo.

Anasema soda haina lishe wala faida yeyote ile kwenye mwili wa binadamu, hivyo huongeza kiasi kikubwa cha sumu mwilini ambacho ni hatari sana kwa afya mtumiaji.

Sumu hizo huongeza hatari ya kupata ugonjwa wa moyo na kuua figo,” anasema Dk Kimambo.

Pia, anaeleza soda hupunguza kiwango cha maji mwilini kwa kuwa ina kiwango kikubwa cha madini ya sodium ambacho humfanya mtu abaki na maji kidogo na kwa muda mrefu atapata matatizo mengine ya kiafya kama mawe ya kwenye figo (kidney stone) na mawe kwenye nyongo ya binadamu.

Dk Kimambo anashauri ni vizuri kubadili mfumo wa maisha na kuanza kunywa vitu ambavyo haviharibu mwili kama vile kunywa juisi ya matunda badala ya soda.
Source: Mwanachi.
Title: elmis
+
 
Upo sahihi ila Asilimia kubwa ya vyakula vinavyotuzunguka ni vichochezi vya Sukari mwilini zaidi ya sukari yenyewe...

Sioni mazingira rahisi Mbongo wa kawaida anachomoa siku bila kula Carbohydrates - Starch - Glucose-Sugar.

Kikubwa ni At least ku balance, sio tuu vinywaji bali na chakula piaa.
 
Juzi nimesikia NIHF ipo karibu kufirisika. Waziri anasema gharama za kutibu magonjwa yasiyoambukizwa ni kubwa sana. Ni magonjwa gani hayo yasiyoambukizwa?

Makubwa ni Kisukari, figo na high blood pressure. Haya kwa sehemu kubwa husababishwa na ulaji mbovu na sedentary lifestyle na yanahusiana sana. Matatizo mengi ya figo huletwa na kisukari.

Sasa kwa sehemu kubwa ulaji wa sukari na mafuta ndiyo visababishi vikubwa vya shida hiz. Inasemwa kuwa binadamu hakuumbwa kula sukari na mafuta kama anayokula leo.

Mambo hayo yana madhara kuliko vitu vikivyozoeleka kuwa na madhara kama pombe, sigara au bangi. Na mbaya zaidi, watu weusi tuna hatari zaidi ya kupata visukari na BP, lakini tumeiga ulaji wa kizungu wa mafuta na sukari nyingi.

Ni vyema, ili kuokoa jamii, serikali ikapiga marufuku soda na vinywaji vingine vilivyoongezwa sukari. Ikishindikana hilo, basi ilazimishe watengenezaji wa bidhaa hizo waweke onyo kama ilivyo kwenye sigara na pombe.

Kweli kabisa magonjwa sugu matibabu Yake yana gharama kubwa sana na magonjwa sugu yanaua sana ,ila kwa sasa kuna tiba ya kutibu magonjwa hayo Kama moyo,kisukari,presha,kansa aina zote,figo,ini ,tezi dume ,bawasiri,na maradhi mengine zaidi ya 165 ambaye anaitaj hiyo tiba aje kwa inbox nimuelekeze hiyo tiba inapopatikana
 
Juzi nimesikia NIHF ipo karibu kufirisika. Waziri anasema gharama za kutibu magonjwa yasiyoambukizwa ni kubwa sana. Ni magonjwa gani hayo yasiyoambukizwa?

Makubwa ni Kisukari, figo na high blood pressure. Haya kwa sehemu kubwa husababishwa na ulaji mbovu na sedentary lifestyle na yanahusiana sana. Matatizo mengi ya figo huletwa na kisukari.

Sasa kwa sehemu kubwa ulaji wa sukari na mafuta ndiyo visababishi vikubwa vya shida hiz. Inasemwa kuwa binadamu hakuumbwa kula sukari na mafuta kama anayokula leo.

Mambo hayo yana madhara kuliko vitu vikivyozoeleka kuwa na madhara kama pombe, sigara au bangi. Na mbaya zaidi, watu weusi tuna hatari zaidi ya kupata visukari na BP, lakini tumeiga ulaji wa kizungu wa mafuta na sukari nyingi.

Ni vyema, ili kuokoa jamii, serikali ikapiga marufuku soda na vinywaji vingine vilivyoongezwa sukari. Ikishindikana hilo, basi ilazimishe watengenezaji wa bidhaa hizo waweke onyo kama ilivyo kwenye sigara na pombe.

Chief uko sayari ya mars au? Hakuna direct connection ya hizo sukari na matatizo hayo, magonjwa yanayotokana na life style au yasiyoambukiza (NTDs$ yana multiple causes.

Ni jukumu la serikali kutoa elimu ya ufahamu ili ukitumia utumie kwa akili lakini at your own risk.

Ni vizuri kutokuwa conclusive kwenye mambo ya kitaalamu ambayo huna ufahamu nayo.
 
Bonge la ushauri
Chief uko sayari ya mars au? Hakuna direct connection ya hizo sukari na matatizo hayo, magonjwa yanayotokana na life style au yasiyoambukiza (NTDs$ yana multiple causes.

Ni jukumu la serikali kutoa elimu ya ufahamu ili ukitumia utumie kwa akili lakini at your own risk.

Ni vizuri kutokuwa conclusive kwenye mambo ya kitaalamu ambayo huna ufahamu nayo.
 
Chief uko sayari ya mars au? Hakuna direct connection ya hizo sukari na matatizo hayo, magonjwa yanayotokana na life style au yasiyoambukiza (NTDs$ yana multiple causes.

Ni jukumu la serikali kutoa elimu ya ufahamu ili ukitumia utumie kwa akili lakini at your own risk.

Ni vizuri kutokuwa conclusive kwenye mambo ya kitaalamu ambayo huna ufahamu nayo.
Ni kweli magonjwa yasiyoambukizwa yanasababu nyingi. Lakini sababu kubwa kwa sasa ni ulaji mbaya na sedentary lifestyle. Hizo sukari sukari zinasababisha moja kwa moja. Sukari zinaleta unene unaleta matatizo ya moyo, unene unaleta insulin resistance na kisukari aina ya pili. Kisukari kinaleta shida ya Ini nk nk.

Ulaji wa sukari na mafuta mengi, ukichangia na maisha ya kukaa tu ni visababishi vikubwa vya magonjwa yasiyoambukiza. Kwani we shuleni kwako ulifundishwaje?
 
Back
Top Bottom