Serikali ipige marufuku vipindi vya michezo redioni kuanza asubuhi. Kipindi cha michezo ninachozidi robo saa kianze saa moja jioni

Serikali ipige marufuku vipindi vya michezo redioni kuanza asubuhi. Kipindi cha michezo ninachozidi robo saa kianze saa moja jioni

Gudasta

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2011
Posts
501
Reaction score
788
Tunaishi katika taifa linalozungumziwa sana kwa michezo, hasa mpira wa miguu, ambapo timu zinazochambuliwa kila wakati ni Simba na Yanga. Hii imekuwa ni hali ya kawaida, na jua linapotoka hadi linapozama, vipindi vingi redioni vinakuwa ni vya uchambuzi wa michezo pekee.

Hata hivyo, kazi mojawapo ya redio ni kuelimisha wananchi, na kuna fursa nyingi za kiuchumi ambazo zingeweza kujadiliwa na kuelimisha umma kuhusu sekta kama teknolojia, utalii, kilimo, na usafirishaji.


Hivi vipindi vya michezo vinaonekana kuwa na muda mbaya wa uchezaji, kwani timing yake si nzuri. Ningependekeza kwamba vipindi hivi vingeweza kuhamasishwa zaidi jioni, ili wananchi wapate maarifa ya kina kuhusu nyanja mbalimbali.

Hii itasaidia kuondoa mtindo wa kuwa taifa linalozungumziwa tu kwa michezo, na badala yake tuwe na taarifa zinazojenga jamii katika maeneo mengi.

Nashauri mamlaka husika serikalini ziangalie hili kwa makini na kubadilisha ratiba ya vipindi hivyo ili viwe vinaanza saa moja jioni, ambapo wananchi wangeweza kufuatilia na kupata maarifa muhimu.

Hii ingekuwa ni hatua muhimu katika kuendeleza umma na kuhakikisha tunajikomboa kiuchumi na kimaendeleo.

Nawasilisha maoni yangu kuhusu hili.
 
Watunga maudhui wameamua mule michezo na burudani kwa miaka 10+
 
mkuu unakwepa tatizo la msingi kabisa.
Ambalo ni mfumo wetu wa elimu haumuandai mtu kuwa na maarifa yatakayowezesha kujiri
vipindi vya michezo hakuna shida yoyote.
Na kwanza vimeanza miaka ya karibuni tu.

Kipindi cha vilikuwa hamna na taifa lilikuwa hivi hivi
kila mtu asikilize anachopenda
 
Pia vipindi vya michezo ndo vinavyouza zaidi.
Hapo nguvu ya soko ndo imeamua. "The higher the demend the higher the supply"

Wamiliki wa radio wanategemea hivyo vipindi ili kulipa mishahara wafanyakazi wao.
Vilikuwepo hivyo vipindi lakini havina wasikilizaji. Kuilazimisha virudishwe hakuna wa kusikiliza. Watu watatafuta wanachotaka
 
nimeacha kusikiliza redio na kuangalia tv
 
Ni bora mara 100 tusikilize michezo kuliko kusikiliza mapambio ya Mama mama mama,

Vipindi vya michezo ndo vipindi pekee vilivyobaki kua real kuchambua mambo kwa uwazi.
 
Back
Top Bottom