Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
Mwaka jana, June 2023, wakati waziri wa mambo ya nje akiwa Dr Tax, serikali ilitoa hili tamko pale Bungeni
Leo April 2024, serikali imetoa tena tamko hilo hilo pale pale Bungeni mbunge wa viti maalumu Suma Fyandomo alipouliza swali kuhusu uraia pacha.
Sasa nakumbuka tumekuwa na matamko kama haya toka serikalini kuhusu SGR, umeme, bei ya sukari, huduma mbovu za polisi, huduma mbovu za maji, barabara mbovu, huduma za ATCL, nk.
Najiuliza, hivi tatizo ni sisi Watanzania, viongozi wetu, Bunge au Raisi Samia? Kwa nini tunadanganywa na serikali kama watoto wadogo kila siku juu ya mambo ya kila namna?
Kwamba tunadharauliwa kiasi hiki na viongozi wetu na wanatuona hatuna akili ya kukumbuka au kutafakari?
Tatizo letu liko wapi? Kwa nini tunakuwa watu wa namna hii?
Leo April 2024, serikali imetoa tena tamko hilo hilo pale pale Bungeni mbunge wa viti maalumu Suma Fyandomo alipouliza swali kuhusu uraia pacha.
Sasa nakumbuka tumekuwa na matamko kama haya toka serikalini kuhusu SGR, umeme, bei ya sukari, huduma mbovu za polisi, huduma mbovu za maji, barabara mbovu, huduma za ATCL, nk.
Najiuliza, hivi tatizo ni sisi Watanzania, viongozi wetu, Bunge au Raisi Samia? Kwa nini tunadanganywa na serikali kama watoto wadogo kila siku juu ya mambo ya kila namna?
Kwamba tunadharauliwa kiasi hiki na viongozi wetu na wanatuona hatuna akili ya kukumbuka au kutafakari?
Tatizo letu liko wapi? Kwa nini tunakuwa watu wa namna hii?