Serikali itusaidie kuboresha Barabara ya Kaliua hadi Kahama

Serikali itusaidie kuboresha Barabara ya Kaliua hadi Kahama

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Mimi natokea Mkoa wa Tabora, Wilaya ya Kaliua, Kata ya Kashishi, kero yetu hapa ni barabara ya kutoka Kahama Mkoani Shinyanga kwenda Kaliua Mjini (Tabora) kupita Unlyankuru, Mwamnange na Kashishi.

Kwani barabara hii ni muhimu kwetu sisi Wakulima tunaitumia kusafirisha mazao kupeleka kwenye soko la Kahama ila hii barabara ni mbovu, magari hukwama njiani mara kwa mara na kusababisha hasara kwa Wakulima, Wamiliki wa magari na watumiaji wengine mbalimbali.

Nyakati za mvua hali ndio inazidi kuwa mbaya, tunaomba Serikali kupitia wizara husika itujengee lami, kwani ni barabara muhimu kwa uchumi wa Wilaya yetu ya Kaliua.
 
Kuna mpumbavu alisema "jimbo ili aliendelei coz mmemchagua mpinzani"
 
Hiyo barabara muhimu sana ila ni hatari kwa magendo ya mbao za mninga
 
Kuna tetesi nimekuwa nikiisikia lakini hainiingii akilini;

Kuwa wenye mabus ya Ruksa hawataki hiyo njia iwekewe lami, kwa sababu inawanufaisha zaidi ikiwa rough road.
 
Mimi natokea Mkoa wa Tabora, Wilaya ya Kaliua, Kata ya Kashishi, kero yetu hapa ni barabara ya kutoka Kahama Mkoani Shinyanga kwenda Kaliua Mjini (Tabora) kupita Unlyankuru, Mwamnange na Kashishi.

Kwani barabara hii ni muhimu kwetu sisi Wakulima tunaitumia kusafirisha mazao kupeleka kwenye soko la Kahama ila hii barabara ni mbovu, magari hukwama njiani mara kwa mara na kusababisha hasara kwa Wakulima, Wamiliki wa magari na watumiaji wengine mbalimbali.

Nyakati za mvua hali ndio inazidi kuwa mbaya, tunaomba Serikali kupitia wizara husika itujengee lami, kwani ni barabara muhimu kwa uchumi wa Wilaya yetu ya Kaliua.
Isingekuwa siasa za kindezi,hii ndio ilikuwa Barabara ya kujengwa badala ya inyonga maana ni shortcut kwenda Mikoa yote ya Lake zone kutoka Mpanda.
 
Barabara muhimu sana hii kiuchumi...

Lakini hakuna kiongozi mwenye habari nayo...

Hii barabara ikiwekwa lami itafungua uchumi wa kaliua na mpanda...

Maana soko kubwa la mazao yanayolimwa huko lipo Kahama...

Lakini nani anasikia...

Oh.
 
Kuna tetesi nimekuwa nikiisikia lakini hainiingii akilini;

Kuwa wenye mabus ya Ruksa hawataki hiyo njia iwekewe lami, kwa sababu inawanufaisha zaidi ikiwa rough road.
Hizi ni story tu yaani mwenye mabus ndio azuwie lami isiwekwe?
 
Mimi natokea Mkoa wa Tabora, Wilaya ya Kaliua, Kata ya Kashishi, kero yetu hapa ni barabara ya kutoka Kahama Mkoani Shinyanga kwenda Kaliua Mjini (Tabora) kupita Unlyankuru, Mwamnange na Kashishi.

Kwani barabara hii ni muhimu kwetu sisi Wakulima tunaitumia kusafirisha mazao kupeleka kwenye soko la Kahama ila hii barabara ni mbovu, magari hukwama njiani mara kwa mara na kusababisha hasara kwa Wakulima, Wamiliki wa magari na watumiaji wengine mbalimbali.

Nyakati za mvua hali ndio inazidi kuwa mbaya, tunaomba Serikali kupitia wizara husika itujengee lami, kwani ni barabara muhimu kwa uchumi wa Wilaya yetu ya Kaliua.
 
Back
Top Bottom