Serikali iwe makini, Urusi imekuja na mbinu hizi kuchukua vijana wa Kitanzania kwenda kupigana Ukraine

Anajidanganya na malipo feki ya $15k per month + $750k retirement benefits.
Hata wanajeshi wa Marekani hawalipwi pesa nyingi kiasi hicho, sembuse mgambo wa Wagner group tena ngozi nyeusi kutoka Afrika.
Vijana wanajidanganya sana
Wahenga walisema: "Sikio la kufa halisikii dawa" eti malipo kwa mwezi ni $15 na mafao ya kustaafu ni $750. Watashangaa watakapokuta malipo ni hewa lakini risasi ni Real.
 
Hapo ubaya uko wapi? Wewe hujui maisha naona, watu wengi hapa Africa wanatamani kujiuga na jeshi la Urusi ukipewa hiyo Fursa, mbona ni bonge la dili, kifia uko ni bahati mbaya tu.
Yaani mfungwa, ambaye alikuwa mwanafunzi, anapelekwa vitani kwa mafunzo mafupi ya less than a month, upelekwe mstari wa mbele then useme wamekufa bahati mbaya? Really? Seriously??
 
Yaani mfungwa, ambaye alikuwa mwanafunzi, anapelekwa vitani kwa mafunzo mafupi ya less than a month, upelekwe mstari wa mbele then useme wamekufa bahati mbaya? Really? Seriously??
Mockery when ur life is at stake. e.g. Umeshaambiwa hapo kichakani kuna simba majeruhi halafu ww unajipeleka hapo. Akishakurarua wenzio wa aina yako waliobaki wanasema ni bahati mbaya. 😳
 
Yaani mfungwa, ambaye alikuwa mwanafunzi, anapelekwa vitani kwa mafunzo mafupi ya less than a month, upelekwe mstari wa mbele then useme wamekufa bahati mbaya? Really? Seriously??
Kwani wakibaki hapa hawafi? Kifo ni popote, bora ufe ukiwa kwenye harakati za kutafuta maisha.
 
Ni hatari sana tena sana hata enzi za miaka ya 1970 vijana wengi low classes walipelekwa Urusi kusoma say std seven lkn walirudi Tz na PHd au Masters degree isitoshe kurudi na wanawake kibao.Isitoshe nakulewa sana.Tukitafakari sana mfumo wa elimu Tanzania ulianza kufa tangu enzi hizo.Mfano 1979 nilimaliza FTC hapo Dsm Technical College,hapo hapo kulikuwa na mwanafunzi mwenzangu naye darasa la Saba tulimaliza naye FTC, kwa mfumo wa degree asingeweza kwenda Mlimani.Nilichaguliwa mimi kujiunga degree ya uhandisi UODsm yeye akaomba na akafanikiwa kwenda USSR.Miaka minne nikapata shahada ya kwanza Uhandisi Umeme.Baada ya miaka mitatu mwenzangu darasa la Saba katoka USSR na PhD Umeme+mwanamke mrusi na ulevi kibao.
Ushuhuda huu vijana wetu wameteseka sana vifo na vita.
Mama Samia inaombwa utuokoe na mvinyo huu
 
Kipindi cha nyuma ilikuwa ngumu sana ukilinganisha leo wakitumia nguvu kubwa ya matangazo kupitia mitandao ya kijamii.

Nimeshangaa kuona vyuo vya urusi kutumia mpaka whatsapp na formu zao ukijaza kujibiwa ni rahisi mno.

Je, Serikali yetu imechunguza ili isije ikawa kuwachukua vijana kwa njia ya kwenda kuwapeleka kwenye lile kundi la mstari wa mbele.

Urusi inasifika sana kwa kubambika kesi na rushwa .
 
mtz akiwekewa ugumu analalamika
akiwekewa urahisi analalamika pia
punguzeni nongwa
 
Jichanganye uone kama hutarudi maiti
 
mtz akiwekewa ugumu analalamika
akiwekewa urahisi analalamika pia
punguzeni nongwa

Ndio asili yetu tulikuwa na Rais mpole (Kikwete) wakalalamika tukapata Rais Mkali (Magufuli) wakalalamika tumepata tena rais mpole (Samia) Wanalalamika. Wabongo huwa hawaeleweki wanataka nini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…