Serikali iwekeze kwenye umwagiliaji na mbegu zinazostahimili ukame

Serikali iwekeze kwenye umwagiliaji na mbegu zinazostahimili ukame

Akilindogosana

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2020
Posts
4,303
Reaction score
12,679
Sasa hivi kuna changamoto kubwa ya uhaba wa mvua au mabadiliko ya tabia nchi. Serikali iwekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji cha kisasa kinachotumia maji machache katika mashamba makubwa kwenye mikoa na wilaya ambazo zinafaa kwa umwagiliaji. Wananchi/vijana wapewe maeneo walime kwa kumwagilia. Na wawe wanatangaza kwa uwazi(bila connection au rushwa au kujuana na wakubwa) juu ya upatikanaji wa mashamba kwenye umwagiliaji. Labda pawe na system au website ya "umwagiliaji portal"

Pia wawekeze katika uzalishaji wa mbegu zinazostahimili ukame. Hasa mazao yenye uhitaji mkubwa kama Mahindi,maharage, ngano, mpunga , alizeti, njugumawe,choroko, dengu, mtama, uwele, ulezi, jamii ya mikunde n.k Hata pia zipatikane mbegu kwa ajili ya malisho ya mifugo. Maana wafugaji wa kuhamahama ndio wanaleta migogoro kwa kulisha mazao ya watu. Ndio maana kuna migogoro ya wakulima na wafugaji.

Hii Hali ya hewa kwa sasa haitabiriki. Ni bora kujipanga mapema na kujikinga na njaa. Na hizi siku za mwisho Yesu alisema patakuwa na njaa na vita. (Dalili za kurudi kwa Yesu mara ya pili.)
"Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali. "
Mathayo 24 :7

Wengine ongezeeni maoni yenu
 
Sasa hivi kuna changamoto kubwa ya uhaba wa mvua au mabadiliko ya tabia nchi. Serikali iwekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji cha kisasa kinachotumia maji machache katika mashamba makubwa kwenye mikoa na wilaya ambazo zinafaa

Wengine ongezeeni maoni yenu
Ndicho imeanza kufanya kuanzia mwaka huu ndio maana unaona hiyo Wizara imepewa pesa nyingi toka uhuru..

Samia anajua anachokifanya.
 
Kwa mada hii we si akili ndogo tena, sasa imekuwa.........ni kubwa.

Hili jambo huwa najiuliza kila siku kinashindikana nini?!!!!!!

Yaani niona legacy ya bure kabisa kwa mama samia hapa kama atasikia hili na kulizingatia!
 
Swali la msingi sana maana hizi nyimbo zipo miongo yote.
Humu jf wapo viongozi wengi wenye ID wanatuchora na wanasoma kimyakimya. Unaeza kuta hata samia yupo humuhumu anasoma kimyakimya akiwa na Id yake. Maana muda wote naonaga samia anaangalia simu yake, je anaangalia nini kwenye simu? Anasomaga nini kwenye simu?
 
Kwa mada hii we si akili ndogo tena, sasa imekuwa.........ni kubwa.

Hili jambo huwa najiuliza kila siku kinashindikana nini?!!!!!!

Yaani niona legacy ya bure kabisa kwa mama samia hapa kama atasikia hili na kulizingatia!
Yaani samia akiamua kukomaa na umwagiliaji na mbegu bora nahisi atajipatia legacy ya bure tena kwa bei nafuu sana. Sio kaa liSgr la kibwege limekula matrilioni na hakuna itakachozalisha na wala haimsaidii mtanzania wa kawaida.
 
Back
Top Bottom