Serikali izibane hotel zote za kulala Tanzania zinaibia wateja

Nchi gani nyingine umeenda mkuu,
Nimewahi kusafiri Dubai,Hongkong, China,Singapore,India, Malaysia,Japan,Ireland. France utaratibu ni kama hapa Tanzania,
Nimetamani huo utaratibu wa Nigeria kama kweli upo.
 
Dahh....

Sasa sijui watu wanatoka mapovu kivipi tena hapaa!??
 
Wewe jamaa inabidi uende FB maana hoja zako ni za kiuanafunzi sana, unatupotezea muda wa kusoma hizo pumba zako tuna mambo mengi ya kufanya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku jamaa mmoja alianzisha valangati la kufa mtu.
Aliingia lodge saa kumi alfajiri, kufika saa nne jamaa wanamgongea, wanamkomalia aachie chumba.
Valangati lake halikua la kitoto, na lilikuja kuamuliwa na mwenye lodge.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali Iwafungua Wabunge Na Wanachama Wa CCM Mortar Na CCTV CAMERA maana huwa wakienda chooni wanamtukana kibwengo
 
Naunga mkono,ila wamiliki wa hizo hotel wanatakiwa waongeze bei mara dufu,ili watejea wao wakae masaa 24,ukiingia saa moja jioni ya leo kesho saa moja uondoke ama ulipie tena ili uendelee kuwepo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bila shaka Nigeria ulienda kwa TB Joshua.
 
hayo masaa yako ya ulaya baki nayo huko huko.UNAPANGA KWA SIKU NZIMA MASAA 24 hakuna siku yenye masaa mawili au matatu.Unaelewa maana ya siku moja ?
 
Wewe utakuwa huwa waenda Guest za uchochoroni but hotels zinazojielewa siku huanza huanza saa Saba usiku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hakuna anayekataa hoteli kufanya usafi. muda a usafi ukifika unawapisha wasafishe mbona kitu cha kawaida.Mfano umepanga hoteli wiki nzima kwani huwa unaondoka hotelini au chumba hakisafishwi? Ninachokataa kumtoa mteja wa siku moja ikifika saa mnne asubuhi wakati masaa yake 24 hayajafika
 
Wewe ni mpumbavu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  1. Vyumba havitozwi kwa masaa 24. Ingekuwa hivi basi wangekuwa wanatoza kwa masaa. Wanafanya hivi ili kurahisisha hesabu zao maana basi mtu akichukua chumba saa 12 jioni halafu akaondoka saa 12 asubuhi basi angetakiwa kulipa nusu ya pango. Wao wana bei moja ambayo inaanzia muda wao wa kuingia ( kati ya earliest check in na latest check out), ukiingia muda wowote katikati utalipa bei nzima. Ni kama vile ukipanda daladala ya kwenda posta Mwenge hautapunguziwa nauli kwa vile unashuka Morocco. Au kwa vile wamekuambia bei ya chumba ni pamoja na kifungua kinywa basi mpishi awepo wa kukupikia wakati wowote utakapotoka au wakupunguzie bei kufidia mlo kifungua kinywa ambapo haukula.
  2. Wanafanya hivi ili wawe na muda maalum wa kusafisha vyumba vyote. Wahudumu wanajua kati ya muda fulani na muda fulani ni muda wao kusafisha vyumba, kubadilisha mashuka na mataulo na kuweka sabuni, shampoo na toilet paper mpya. Ikiwa kila mtu atatoka kulingana na muda anaoingia basi wahudumu itabidi wawe kazini kwa masaa 24 ili vyumba visafishwe mara mtu anapotoka. Hii ni ngumu kufanyika.
  3. Nchi nyingine, breakfast sio sehemu ya gharama ya chumba. Ukitaka kula asubuhi basi unalipa zaidi. Hapa kwetu kuna sehemu hawatoi sabuni ya kuogea, ukitaka kuoga kwa sabuni inabidi uje nayo.
  4. Nchi nyingine bei ya chumba inategemea siku ya wiki, msimu n.k. Usitegemee bei uliyolipia jumatatu ndio itakuwa hiyo hiyo ijumaa.
  5. Kwa kifupi upangaji wa bei na masharti ya upangaji wa chumba ni ya mwenye hoteli. Kama hauridhiki, una haki kutafuta sehemu nyingine ambayo itaendana na mahitaji yako au hata unaweza kulala stendi ambako hakuna check out time.
Amandla..........
 
Nimejikuta naona aibu mimi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…