Serikali kuanza kujenga barabara za juu kupunguza msongamano wa magari Dar!

Serikali iache blahh blahh ihamie Dodoma kwanza na kuweka nguvu kubwa pale, waupangilie mji wa Dodoma kwa vision ya miaka 200 ijayo, kwa Dar mimi naunga mkono wazo la kuboresha feeder road na kuondoa mizunguko (roundabout) badala yake kuwe na madaraja ya kupishana kama wenzetu Kenya wanavyofanya sasa badala ya kuwa na flyover moja halafu inaenda kuishia kwenye jam ni sawa na kucheza mchezo wa kijificha..
 
yote yanawezekana kama serikali ikichukua maamuzi magumu ikiwa kwanza kuondoa mafisadi wizara zote wa-jairo walio wengi maana 1o% zinasumbua hii serikali legelege , ambayo haikusanyi kodi
 
Badala ya kukimbilia hizi flyovers kwa nini wasiimarishe feeder roads? Mfano
Mwananyamala-Sinza
Makongo-Kimara
Wazo-Kibaha
Mkuu wangeanza na hizi njia tungeona kweli wamedharia kuounguza msongamano!lakini kwa Fly overz lazima Wachekeshe!Lakini si wamezoea
 
<br />
<br />
Jf ina watu ambao wana ubunifu unao weza kuisaidia serikali kwa kias kikubwa, wakiya fanyia kazi.
 
Ujenzi wa fly overs Dar hauepukiki hata kidogo ikiwa ni lazima kumaliza tatizo la foleni. Kenya wanajenga hizo barabara na tayari wameanza kuona matunda yake. Foleni kubwa ziko katikati ya mji kwa sababu ya kushindwa kupishana katika barabara za crossroads; barabara za pembeni nazo ziongezwe mpya na kukarabati zile zilizopo.
 
Hizo fly overs hizo msishangae baada ya muda pot-holes kibao mpaka mnaona magari ya wanaopita chini.......kwi kwi kwi kwi

Kwa bongo wala sitoshangaa!!!!!!!
 
Siku hizi hata wakuja wote mnamagari, halafu hakuna maendeleo? Mnanshangaza!

Tulipokuja tulinunua magari ili yatuwahishe kwenye shughuli zetu sasa kama yanatuchelewesha kuliko hata waenda kwa miguu, hayo ni maendeleo kweli?
 
<br />
<br />
 

hayo majukumu yanasimamiwa na mamlaka tofauti. Magufuli anazungumzia barabara zilizo chini ya wizara (TANROADS) hizo za vichochoro zipo chini ya manispaa za Dar. hapo ni kuwabana madiwani pamojan na wabunge wa dar wasimamie ipasavyo maeneo hayo. tatizo watendaji wengi wa manispaa hizo wanaendekeza rushwa na kusahau majukumu yao ndiyo maana hakuna planning hata kwenye mitaa mipya
 


Wangekamilisha hizo za pembeni na kufata mawazo ya wana JF wangejenga Jina kwa mafanikio
 
Tatizo la Foleni dar es salaam, ni kwenye crossroad kama Mataa ya Ubungo, Mataa ya Magomeni Mapipa, Mataa ya Tazara, Mataa ya Mandela Road, hizi sehemu wakijenga flyover!

Natizo la foleni litakuwa hamna gari zitakuwa zinatembea kwa kasi
 
Basi waanze huo ujenzi si kupiga porojo tu nimesikia jana wametenga 90m/= kwa kazi hiyo alilalamika Idi Azan bungeni
 

Ukiangalia barabara za juu za wenzetu mfano South Africa ikijengwa pale Ubungo mataa basi Songas lazima iondolewe, ghorofa la TANESCO na power shed yao pale nyuma lazima viondoke, kile kituo cha mafuta, ofisi za TBS na sehemu ya stand ya mkoa lazima viondoke na upande wa kulia kama unaelekea Kimara ikiwemo wizara ya maji lazima viondoke. Sasa je wamekwisha tazama cost benefit analysis hapo? Je, gharama ya fidia tu kwa hayo yote si ingetosha kutengeza feeder roads za nguvu? Kama JK alikataa jengo la TANESCO kuvunjwa, kwa ili atakubali?
 
Tatizo la Foleni dar es salaam, ni kwenye crossroad kama Mataa ya Ubungo, Mataa ya Magomeni Mapipa, Mataa ya Tazara, Mataa ya Mandela Road, hizi sehemu wakijenga flyover!

Natizo la foleni litakuwa hamna gari zitakuwa zinatembea kwa kasi

Ndugu tambua hata huko kwenye flyovers huwa kuna foleni za nguvu during rush hours - mimi nimeona hii huko Pretoria, RSA ila foleni zao zinatembea nafikiri kwa sababu ya ustaarabu wa madereva kwani wanaachia kuingia main road, pia nafikiri na usimamiaji wa sheria za barabarani ni mzuri sana - CCTV. Hivi hapa bongo si kunawakati polisi walisema CCTV zitatumika barabarani?

Hivi ule mradi wa mabasi yaendayo kasi umekwisha anza? Na yatapitaje kwenye flyover yenye nguzo za nguvu?!
 
Mkuu wakaya wakati wa kampeni alisema zoezi hili lingeanza mwezi march 2011, now ishakuwa August yan sina hamu na hiyo kitu, sitaki kuamin ktk mradi wao huo!
 
Mkuu wakaya wakati wa kampeni alisema zoezi hili lingeanza mwezi march 2011, now ishakuwa August yan sina hamu na hiyo kitu, sitaki kuamin ktk mradi wao huo!
Ilikuwa ni Ahadi ya Papo kwa Papo!Sidhani kama mradi flyovers ulikuwemo kwenye budget ya 2010/2011
 
tumeacha mradi wa mabasi ya kasi tumerukia flyovers. Yote ni mawazo mazuri, utekelezaji ndo kazi. Kabla ya yote waondoe shughuli ambazo zinaweza kufanywa nje ya mji. Mfano mahakama ya kisutu inaweza kuhamia karibu na magereza maeneo ya ukonga ili daktari asisimamishwe asubui kumpisha mahabusu anayeenda kwenye kesi ya kuiba kuku
 


mradi wa mabasi yaendayo kasi BRT au DART kama yatakavyojulikana mabasi ya Dar haujaachwa ujenzi unaendelea kama kwa, cheki hapa kituo cha kivukoni karibia kinamalizika

kivukoni terminal




source http://www.skyscrapercity.com/showthread.php?t=1191319
 
Badala ya kukimbilia hizi flyovers kwa nini wasiimarishe feeder roads? Mfano
Mwananyamala-Sinza
Makongo-Kimara
Wazo-Kibaha
Hapa watakuwa wametatua Tatizo kwa kiasi kikubwa sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…