Serikali kuanza kujenga barabara za juu kupunguza msongamano wa magari Dar!

Serikali kuanza kujenga barabara za juu kupunguza msongamano wa magari Dar!

Serikali iache blahh blahh ihamie Dodoma kwanza na kuweka nguvu kubwa pale, waupangilie mji wa Dodoma kwa vision ya miaka 200 ijayo, kwa Dar mimi naunga mkono wazo la kuboresha feeder road na kuondoa mizunguko (roundabout) badala yake kuwe na madaraja ya kupishana kama wenzetu Kenya wanavyofanya sasa badala ya kuwa na flyover moja halafu inaenda kuishia kwenye jam ni sawa na kucheza mchezo wa kijificha..
kwani nini tofauti ya bypass na fly overs? zote dhumuni lake ni moja kukwepa intersection. Sasa kwa siye JICA feasibility study imependekeza fly overs na si by passes tuache ujuaji jamani...fly overs muhimu pamoja na feeder roads
 
Ndugu zangu wana JF mwenzenu mkweche Nafunga mwaka sijakanyaga jiji la Dar au bongo!Zile barabara za Angani zimeshaanza kujengwa?
manake ahadi ilikuwa ni ya msisitizo kama hakuna mkandarasi eneo la tukio ntajua ilikuwa Danganya toto!
 
Ndugu zangu wa JF wa Mnaishi Bongo!
Zile barabara za juu(flyovers) zilizinduliwa na Mbio za Mwenge!?
Au Mchakato wa mkandarasi bado unaendelea au Dr Madufuli Amesahau?!
Miaka 50 ya uhuru tumethubutu,tumeweza na tunazidi kusonga mbele!
 
Mie Mkweche bado nalia na Barabara za Gorofa!Kama Magufuli ameshindwa awajibike!Si alituahidi mwenyewe!
 
Barabara za chini zimewashinda za juu wataziweza?
Ni sawa na kutaka kujenga choo kabla ya nyumba

Naam,
Siyo busara hata kidogo kuanza kujenga flyovers sasa hivi, labda with exception of TAZARA area. Ujenzi wa barabara mbadala kuelekeza magari mbali na hizo sehemu tete ni muhimu na cheaper zaidi kwa sasa. Ujenzi wa flyovers bado utaendelea kukusanya magari kwenye barabara na intersection hizo hizo na ifahamike kwamba tatizo haliko kwenye hizo intersections peke yake. Magari yakishaondoka kwenye hizo intersections yanarudi kwenye hizo hizo barabara amabzo tayari hazitoshi.

Kwa mfano ukitoka Ubungo kuelkea Morogoro kuna foleni ya kufa mtu siku hizi na wenyeji wanafikiria kuhama. Flyover haisaidii sana katika hilo na matatizo kama hayo yapo Dar nzima. Hakuna ulazima wa kuwa na hiyo shingo ya chupa hapo Ubungo na sehemu nyinginezo.

Solution ipo katika kujenga barabara kuepusha magari kukutana sehemu moja lakini pia kupunguza msongamano kwenye hizo barabara zilizopo sasa. Kwa mfano kulikuwa na proposal ya kujenga ring road kubwa (four, preferably six lane) kuanzia Airport-Kinyerezi, Mbezi mwisho, Bunju. Kisha hii barabara ring road inaunganishwa sasa na barabara ndogo kadhaa zinatoa na kuingiza magari kutoka sehemu kadhaa mjini. Hili likifanyika, traffic jams zitapungua overnight. Cha ajabu wazo hili limeachwa na sasa tunaongelea flyovers!

Ni vyema tukafanya tathmini upya, na bila shaka wazo la flyovers linaweza likawa siyo muafaka kwa sasa.
 
Naam,
Siyo busara hata kidogo kuanza kujenga flyovers sasa hivi, labda with exception of TAZARA area. Ujenzi wa barabara mbadala kuelekeza magari mbali na hizo sehemu tete ni muhimu na cheaper zaidi kwa sasa. Ujenzi wa flyovers bado utaendelea kukusanya magari kwenye barabara na intersection hizo hizo na ifahamike kwamba tatizo haliko kwenye hizo intersections peke yake. Magari yakishaondoka kwenye hizo intersections yanarudi kwenye hizo hizo barabara amabzo tayari hazitoshi.

Kwa mfano ukitoka Ubungo kuelkea Morogoro kuna foleni ya kufa mtu siku hizi na wenyeji wanafikiria kuhama. Flyover haisaidii sana katika hilo na matatizo kama hayo yapo Dar nzima. Hakuna ulazima wa kuwa na hiyo shingo ya chupa hapo Ubungo na sehemu nyinginezo.

Solution ipo katika kujenga barabara kuepusha magari kukutana sehemu moja lakini pia kupunguza msongamano kwenye hizo barabara zilizopo sasa. Kwa mfano kulikuwa na proposal ya kujenga ring road kubwa (four, preferably six lane) kuanzia Airport-Kinyerezi, Mbezi mwisho, Bunju. Kisha hii barabara ring road inaunganishwa sasa na barabara ndogo kadhaa zinatoa na kuingiza magari kutoka sehemu kadhaa mjini. Hili likifanyika, traffic jams zitapungua overnight. Cha ajabu wazo hili limeachwa na sasa tunaongelea flyovers!

Ni vyema tukafanya tathmini upya, na bila shaka wazo la flyovers linaweza likawa siyo muafaka kwa sasa.

"Kulikuwa"...sasa ipo wapi?...hatupo serious sisi...kila siku unasikia maneno haya tuu!
 
Hata mgao wa umeme walishasema itakuwa historia... Hii kauli imeshatolewa zaidi ya mara sita
 
Mi nafikiri tutumie fursa, tuwaambie wajapani tunawahakikishia soko la magari yao ila sharti wajenge barabara zetu tuwatumie wanasiasa hakika watakuja kujenga tu
 
Hizo fly overs hizo msishangae baada ya muda pot-holes kibao mpaka mnaona magari ya wanaopita chini.......kwi kwi kwi kwi

Watanzania tunajidharau saana sijui watu wengine wasemeje !!!
 
shida yetu ni namna ya kupanga na kuweka kipaumbele kipi kianze na kipi kifuate
 
Bado tunasubiri ahadi ya barabara za juu Kikwete anaondoka mwakani.
 
Hadithi njoo uongo njoo utamu ukolee

Vipi Washamaliza kuzijenga hizo barabara za Juu? manake hii ya Strabag hoi haiishi... kama magofu...
 
Back
Top Bottom