Serikali kufufua mgodi wa Buzwagi uliofungwa na Acacia kwa madai ya Madini kuisha Ardhini

Serikali kufufua mgodi wa Buzwagi uliofungwa na Acacia kwa madai ya Madini kuisha Ardhini

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
PAMOJA na mmiliki wa sasa wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi, kampuni ya Acacia Mining, kutangaza kutaka kufunga mgodi wake, serikali ya Tanzania imesema, mgodi huo, uatendelea kufanya kazi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Acacia iliamua kuufunga mgodi wake wa Buzwagi, uliyopo wilayani Kahama, mkoani Shinyanga, baada ya kujiridhisha kuwa utajiri wa madini uliyopo katika eneo hilo, umemalizika.

Taarifa ya mgodi huo kuendelea kutumika, imetolewa leo Jumanne, tarehe 19 Januari 2021 na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Prof. Palamagamba Kabudi, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba kati ya serikali ya Tanzania na kampuni ya Madini ya LZ Nickel Limited.

Akizungumza katika halfa hiyo, mbele ya rais John Magufuli, Prof. Kabudi alisema, “faida kubwa ya mradi huu, ni kuanza matumizi mbadala ya miundombinu iliyokuwa inatumika kwenye uendeshwaji wa mgodi wa Buzwagi, ambao unatarajiwa kufungwa hivi karibuni.”

Alisema, muwekezaji huyo mpya, ameomba kwa serikali kuruhusu kutumika kwa miundombinu ya mgodi wa Buzwagi, pindi mgodi huo utakapofungwa.

Aidha, kampuni hiyo imeomba kibali cha kuchenjua masalia ya madini yaliyoko katika mgodi wa Buzwagi, kwa maelezo kuwa teknolojia yake ya kuchenjua masalia hayo kuwa madini, yaweza kufanya kazi hiyo.

Alisema, “…mheshimiwa rais, wawekezaji hawa wameomba mgodi huu utakapofungwa wauchukue ili badala ya kufungwa ufanye kazi nyingine, ili kuuongezea uhai zaidi sababu wanasema yale masalia yaliyoko pale Buzwagi bado yana madini.”

Ameongeza, “…na kwa teknolojia hii mpya, bado watavuna madini haya ambayo sasa ni rundo. Teknolojia ya wale ilikuwa haiwezi kuyachenjua. Hawa wanaweza; sasa masalia yote ya Buzwagi yatarudishwa tena kwenye mitambo na kutoa madini.”

Prof. Kabudi alitoa taarifa hiyo wakati anataja faida za mkataba huo wa uchimbaji madini ya Nickel katika mgodi wa Kabanga mkoani Kagera na ujenzi wa Kiwanda uchakataji madini mkoani Shinyanga.

Ametaja faida nyingine za mradi huo, ni kuongezeka kwa ukuaji wa uchumi kupitia sekta ya madini.

“Mradi huu utaongeza ukuaji wa sekta ya madini, kwa kuanzisha na kuendeleza uchimbaji wa madini ya Nickel na madini muambata kama kopa na kobati,” ameeleza
 
Utaolewa we bwege
Kibaraka wa Acacia Lisu akisikia hii taarifa ataangua kilio. Yote haya ni matokeo ya kazi nzuri ya Barrick Gold

Acacia alikuwa akituibia watanzania na Barick Gold wenye hisa yingi akiwa a management company

Mimi nilitetea sana Barrick nikasema Acacia wezi wanaibia serikali na barrick na watetezi wa Acacia Lissu na Zitto Kabwe wezi wakubwa wanachukua rushwa Acacia hasa Tundu Lissu ndie alikuwa kibaka mkubwa mla pesa za Acacia na Fatuma Karume walikuwa wakila pesa za Acacia bila kunawa kama mawakili wao

Fatuma Karume, Tundu Lissu na Zitto Kabwe rudisheni hela zao mlizochukua Acacia
 
Kibaraka wa Acacia Lisu akisikia hii taarifa ataangua kilio .Yote haya ni matokeo ya kazi nzuri ya Barrick Gold

Acacia alikuwa akituibia watanzania na Barick Gold wenye hisa yingi akiwa a management company

Mimi nilitetea sana Barrick nikasema Acacia wezi wanaibia serikali na Natick na watetezi wa Acacia Lisu na zitto kabwe wakubwa wanachukua rushwa Acacia hasa Tundu Lisu ndie alikuwa kibaka mkubwa mla pesa za Acacia na Fatuma Karume walikuwa wakila pesa za Acacia bila kunawa kama mawakili wao

Fatuma karume .Tundu Lisu na zitto kabwe rudisheni hela zao mlizochukua Acacia
Ni nani aliwapa Acacia mkabata ka si CCM..

Tumewaambia mikataba hii ipite Bungeni ijadiliwe mmegoma hadi wa leo...na kibaya zaidi mmefanya Bunge kuwa kikao cha Halmashauri ya CCM taifa.
 
Kibaraka wa Acacia Lisu akisikia hii taarifa ataangua kilio .Yote haya ni matokeo ya kazi nzuri ya Barrick Gold

Acacia alikuwa akituibia watanzania na Barick Gold wenye hisa yingi akiwa a management company

Mimi nilitetea sana Barrick nikasema Acacia wezi wanaibia serikali na barrick na watetezi wa Acacia Lisu na zitto kabwe wezi wakubwa wanachukua rushwa Acacia hasa Tundu Lisu ndie alikuwa kibaka mkubwa mla pesa za Acacia na Fatuma Karume walikuwa wakila pesa za Acacia bila kunawa kama mawakili wao

Fatuma karume .Tundu Lisu na zitto kabwe rudisheni hela zao mlizochukua Acacia

..acha uongo.

..barrick ndio walioanzisha acacia na waliokuwa na hisa nyingi zaidi.

..vigogo wa ccm ndio waliowaleta barrick na acacia nchini na kuwafungulia milango wajichotee madini.

..walioruhusu barrick watulipe kishika uchumba cha usd 300 million, badala ya deni la usd 191 billion, ndio wezi wakubwa na vibaraka wa mabeberu.
 
Ameongea kilayman hasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji38][emoji38][emoji38]

Kifupi:

Mgodi ukifika CUT OFF GRADE ni kufunga tu.

Sasa kama huu ulifungwa kwa kufika cut off grade sijui serikali wana mbinu gan ya kuuendesha kwa faida.

Vinginevyo labda haukufika huko

------
Cut-Off grade is the minimum grade required in order for a mineral or metal to be economically mined (or processed)
 
..ebu acha uongo.

..barrick ndio walioanzisha acacia na waliokuwa na hisa nyingi zaidi.

..vigogo wa ccm ndio waliowaleta barrick na acacia nchini na kuwafungulia milango wajichotee madini.
Sio kweli Barrick walitafuta management company ya kuendesha mgodi tenda wakashinda kampuni ya acacia katika malipo na incentive walizopewa ni hisa kidogo kuwa pamoja na malipo watakayolipwa pia watapewa hisa ni kama Tanzania brewerias walipokuja walimpa managing director Arnold Kileo hisa kuwa pamoja na malipo ya ku manage wakampa hisa moja

Acacia walipishika management ya mgodi ndio wakaanza kuiibia Tanzania na main shareholders Barrick ndio maana serikali ilikataa katakata kujadiliana chochote na management Accacia ikataka kujadili na main shareholder Barrick aliyemwajiri Acacia

Akina Lisu Fatuma karume na Tundu Lisu wakawa wanaikingia kifua management company ya Acacia ndio kibaka Lisu akawa akitutishia kuwa Acacia itatupeleka MIGA!!! Yaani anatushia eti management itatupeleka MIGA

Dk Magufufuli akakomaa na main shareholders anawaambia Acacia siongei na mbwa naongea na mwenye mbwa Barrick.Leo ndio haya matunda tunayaona Acacia vibaka walifunga mgodi wakitishia nyau kwa ushauri wa vibaka Lissu Fatuma karume na zitto kabwe leo mgodi huo unaendelea! Barrik oyeee Dk Magufuli hoyee Tundu Lisu ziiiii Fatuma Karume ziiiii Zito Kabwe ziiiiiii
 
Jenga hoja yako bila kuwachafua wasio husika
Huwezi ongelea Acacia bila kugusa Lisu Mzee wa MIGA Fatuma karume wakili wa kesi ya ACACIA na Zitto Kabwe mtetezi bungeni
 
[emoji38][emoji38][emoji38]

Kifupi:

Mgodi ukifika CUT OFF GRADE ni kufunga tu.

Sasa kama huu ulifungwa kwa kufila cut off grade sijui serikali wana mbinu gan ya kuuendesha kwa faida.

------
Cut-Off grade is the minimum grade required in order for a mineral or metal to be economically mined (or processed)
Chunga ulimi wako
 
Huwezi ongelea Acacia bila kugusa Lisu Mzee wa MIGA Fatuma karume wakili wa kesi ya ACACIA na Zitto Kabwe mtetezi bungeni
Hao wanaingiaje katika kujenga hoja wewe, mliona wanawachelewesha, sasa wameamua mpate uhuru wa kufanya kile mlichotamani, bado mnahangaika nao tu.
 
Magufuli chimba hapo madini yapo.
wanaosema serikali haifanyi biashara ni wahujumu uchumi hao wala usiwasikilize
 
Back
Top Bottom