Serikali kufuta zaidi ya kesi mia nne ndani ya miezi Saba nyingi za watuhumiwa wa uhujum uchumi,mahakama ina umuhimu gani nchini?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Kesi nyingi zilizofunguliwa na awamu ya JPM zimefutwa, watuhumiwa wengi tulioambiwa walihujumu uchumi wakanyimwa dhamana wameachiwa kwa maelezo kwamba serikali haina umuhimu wakuendelea na kesi hizo. Awali tuliambiwa wanazungumza na DPP wanalipa lakini Leo hii hakuna anayezungumza na DPP Wala anayelipa Jambo ambalo linatia doa mahakama yetu.

Je, Ni sahihi wanasiasa kutumia mahakama kunyima watu uhuru? Nini mahakama inapaswa kufanya kuepukan na mtego uliopo mbele yao wakuwaweka watu mahabusu bila fidia kwa sababu zakisiasa? Tutaendelea kuweka watu mahabusu Hadi lini kisa tu wanamyizamo tofauti na wetu?
 
Muhimili wa mahakama ulimezwa. Walikuwa ni watu wa kupokea maagizo tu
 
Hao Majaji wanateuliwa na kuapishwa na wanasiasa. Hawana uhuru wala ujanja wa kufanya chochote.
 
Na hili ndilo eneo ambalo Hangaya amemsaliti Magufuli mchana kweupe.
 


Kwani kufuta tena baada ya kujiridhisha kesi sio moja ya majukumu ya mahakama?
 
Banana republic ni nchi inayoendeshwa na serikali isiyofuata sheria zake hasa pale sheria hizo zinawabana watu wa kundi fulani la jamii. Kwao sheria siyo msumeno! Tanzania sasa ni banana republic; kama una kosa lolote la jinai wewe tafuta connection huko serikalini ili serikali hiyo isiwe na interest kuendelea na shauri lako mahakamani.

taratibu hizi za serikali kuamua wakati wowote kutokuwa na interest kuendesha kesi za jinai ndizo huleta rushwa sana hasa kwa wanasheria wa serikali na ofisi nzima ya DPP.
 
Mahakama zetu hazina hadhi ya kuitwa 'the Judiciary'.Ni utopolo wa CCM na serikali yake.
 
Unaweza kutupa Link ya hii habari yako?au ni mawazo yako binfsi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…