Serikali kujenga hospitali mpya Wilaya ya Ukerewe

Serikali kujenga hospitali mpya Wilaya ya Ukerewe

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Serikali ya Tanzania inajenga Hospitali mpya ya Rufaa wilayani Ukerewe mkoani Mwanza katika jitihada za kutokomeza vifo vya mama na mtoto vinavyotokea baada ya kukosa huduma za matibabu ya kibingwa.

Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa afya Ummy Mwalimu wakati akikagua eneo la ujenzi huo, akisema hospitali hiyo itajengwa katika kijiji cha Bulamba kata ya Bukindo na tayari bilioni nne zimeshatengwa kwaajili ya kuanza utekelezaji wake.

“Hospital hii itakuwa na uwezo wa kutoa huduma nne za matibabu ya kibingwa, kama vile upasuaji, upasuaji wa mifupa, magonjwa ya wanawake na uzazi pamoja na magonjwa ya watoto." amesema Waziri Ummy Mwalimu

Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Elkana Balandya, amesema kukamilika kwa hospitali hiyo mpya ya rufaa Mkoa kutasaidia kutoa matibabu ya kibingwa kwa wananchi hata nyakati za usiku.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Ukerewe Joseph Mkundi, amewataka wakazi wa kijiji hicho itakapojengwa hospital hiyo kuhakikisha wanatoa ushirikiano katika ujenzi wa hospitali mpya ya Mkoa ya Rufaa wilayani humo kwa kulinda vifaa vya ujenzi wake.

Naye Mkuu wa wilaya hiyo Hassan Bomboko amemshukuru na kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa hospital hiyo ambayo amesema itatoa matibabu ya kibingwa kwa wakazi wa kisiwa hicho na kuondoa usumbufu wa kufuata matibabu ya kibingwa mkoani Mwanza.
 
Wakati huo huo Hospital ya Mkoa wa Rukwa ni mbaya na haiana hadhi ya Hospital ya Mkoa..

Hapo Mwanza kutakuwa na Bugando,Sekou Toure, Ukerewe zote za Rufaa..

Geita zipo Chato ya Rufaa ya Kanda na Geita Regional Hospital
 
Wakati huo huo Hospital ya Mkoa wa Rukwa ni mbaya na haiana hadhi ya Hospital ya Mkoa..

Hapo Mwanza kutakuwa na Bugando,Sekou Toure, Ukerewe zote za Rufaa..

Geita zipo Chato ya Rufaa ya Kanda na Geita Regional Hospital
Kwan mbunge wenu ana kazi gan
 
Serikali ya Tanzania inajenga Hospitali mpya ya Rufaa wilayani Ukerewe mkoani Mwanza katika jitihada za kutokomeza vifo vya mama na mtoto vinavyotokea baada ya kukosa huduma za matibabu ya kibingwa.

Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa afya Ummy Mwalimu wakati akikagua eneo la ujenzi huo, akisema hospitali hiyo itajengwa katika kijiji cha Bulamba kata ya Bukindo na tayari bilioni nne zimeshatengwa kwaajili ya kuanza utekelezaji wake.

“Hospital hii itakuwa na uwezo wa kutoa huduma nne za matibabu ya kibingwa, kama vile upasuaji, upasuaji wa mifupa, magonjwa ya wanawake na uzazi pamoja na magonjwa ya watoto." amesema Waziri Ummy Mwalimu

Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Elkana Balandya, amesema kukamilika kwa hospitali hiyo mpya ya rufaa Mkoa kutasaidia kutoa matibabu ya kibingwa kwa wananchi hata nyakati za usiku.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Ukerewe Joseph Mkundi, amewataka wakazi wa kijiji hicho itakapojengwa hospital hiyo kuhakikisha wanatoa ushirikiano katika ujenzi wa hospitali mpya ya Mkoa ya Rufaa wilayani humo kwa kulinda vifaa vya ujenzi wake.

Naye Mkuu wa wilaya hiyo Hassan Bomboko amemshukuru na kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa hospital hiyo ambayo amesema itatoa matibabu ya kibingwa kwa wakazi wa kisiwa hicho na kuondoa usumbufu wa kufuata matibabu ya kibingwa mkoani Mwanza.
Ukerewe+Ukara. Hiyo imekaa vizuri
 
Back
Top Bottom