Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
MAMLAKA ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), imesema kuna kundi kubwa la watoto wenye jinsia mbili, lakini wanafichwa na wazazi, hivyo kushindwa kupatiwa matibabu.
Kutokana na hatua hiyo, jamii imetakiwa kuacha imani potofu na kutumia fursa zilizopo katika mamlaka hiyo, ili watoto hao wafanyiwe uchunguzi kubaini jinsia yenye nguvu na kujengewa uwezo.
Akizungumza katika Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimatafa (DITF), yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Huduma na Udhibiti anayesimamia uingizaji, usambazaji na matumizi ya kemikali nchini, Daniel Ndiyo, alisema kundi kubwa la watoto wenye jinsia linafichwa.
“Mamlaka kwa kushirikiana na madaktari mbalimbali nchini, inafanya uchunguzi kwa watoto wanaozaliwa na jinsi mbili tofauti, lengo ni kuangalia ipi ina nguvu na inaweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi,”alisema. Alisema wakati umefika jamii kuacha kuwaficha watoto hao na kuwapeleka katika mamlaka ya mkemia mkuu ili kufanyiwa uchunguzi.
Ndiyo alisema watoto wanaozaliwa na jinsi mbili tofauti wapo na wamebaini wanafichwa, hivyo ni vyema wananchi kujengewa uwezo wa elimu na kubaini kuwa hilo ni tatizo la kawaida hivyo waache imani potofu.
“Kwa sasa hakuna haja ya kuwaficha watoto hao, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali inatoa huduma za kiuchunguzi na ile inayothibitika inatawala kati ya kiume na kike, inajengewa uwezo na kufanya kazi,”alisema
Alisema uchunguzi wa kimaabara una uwezo wa kutambua kuwa mtoto huyo ni mwanamke au ni mwanaume na jinsi ipi ambayo haitakiwi kuwepo na wataalamu wa mkemia mkuu wanawashauri madaktari kufanya upasuaji, ili kumwezesha mtoto huyo atambulike kama ni mwanaume au mwanamke.
Kutokana na hatua hiyo, jamii imetakiwa kuacha imani potofu na kutumia fursa zilizopo katika mamlaka hiyo, ili watoto hao wafanyiwe uchunguzi kubaini jinsia yenye nguvu na kujengewa uwezo.
Akizungumza katika Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimatafa (DITF), yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Huduma na Udhibiti anayesimamia uingizaji, usambazaji na matumizi ya kemikali nchini, Daniel Ndiyo, alisema kundi kubwa la watoto wenye jinsia linafichwa.
“Mamlaka kwa kushirikiana na madaktari mbalimbali nchini, inafanya uchunguzi kwa watoto wanaozaliwa na jinsi mbili tofauti, lengo ni kuangalia ipi ina nguvu na inaweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi,”alisema. Alisema wakati umefika jamii kuacha kuwaficha watoto hao na kuwapeleka katika mamlaka ya mkemia mkuu ili kufanyiwa uchunguzi.
Ndiyo alisema watoto wanaozaliwa na jinsi mbili tofauti wapo na wamebaini wanafichwa, hivyo ni vyema wananchi kujengewa uwezo wa elimu na kubaini kuwa hilo ni tatizo la kawaida hivyo waache imani potofu.
“Kwa sasa hakuna haja ya kuwaficha watoto hao, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali inatoa huduma za kiuchunguzi na ile inayothibitika inatawala kati ya kiume na kike, inajengewa uwezo na kufanya kazi,”alisema
Alisema uchunguzi wa kimaabara una uwezo wa kutambua kuwa mtoto huyo ni mwanamke au ni mwanaume na jinsi ipi ambayo haitakiwi kuwepo na wataalamu wa mkemia mkuu wanawashauri madaktari kufanya upasuaji, ili kumwezesha mtoto huyo atambulike kama ni mwanaume au mwanamke.