Serikali kuu na connection

Serikali kuu na connection

Mbahili

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
281
Reaction score
525
Habari za muda wanajamvi.
Naomba nitangulize shukrani kubwa sana kwa wanajamvi wote wa jamiiforums. Kiukweli, kimekuwa chombo kikubwa kilichosheheni vingi na kutosheleza kila idara.

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada.
Ni majuzi nilikuwa na rafiki yangu tunazungumzia kazi serikalini, nilimshauri fungua portal register asubiri kazi kisha afanye application.
Niliongeza kujifanya mjuzi kuhusu bla blah blah za serikali..
Ndipo aliponionesha jambo, nikasema nishitikishe jukwaa. Alinionesha watoto wa viongozi wetu maarufu wengi wanaoandaliwa kuongoza nchi kwa kupewa vyeo mbalimbali serikalini. Seriously, nilibisha. Ila niliona majina yao nikajiuliza..

Kama Tanzania kila kiongozi atamkonekt mwanae na ndugu zake serikalini, Je mwajuma ndalandefu wa Butimba mwenye degree ambae baba'ke ni mkulima nani atamsimamia?

Kwanini Tanzania wanakosa uzalendo na kupachika watoto wao?
Ninakamilisha uzi wangu kwa kusema ifikapo mwaka 2050. Tanzania inakuwa nchi ya kifalme....
 
Kazi gani huko serikalini?


Hao Watoto wa viongozi ni akina nani?

Unaonekana kuna kitu unakitafuta tofauti na ulichokiandika.
 
Back
Top Bottom