Tetesi: Serikali kuunda tume ya kimahakama kuchunguza sintofahamu kuhusu utekaji na utesaji wa raia

Tetesi: Serikali kuunda tume ya kimahakama kuchunguza sintofahamu kuhusu utekaji na utesaji wa raia

kimpawwe

Senior Member
Joined
Aug 22, 2017
Posts
164
Reaction score
133
Amani iwe nanyi, tetesi nilisozipata zinatabiri kwamba Serikali imeshaunda task force kuchunguza na kubaini wahusika wa vitendo vya utekaji na utesaji dhidi ya raia na huenda ikaundwa tume huru ya kimahakama kuchunguza shambulio la Dodoma dhidi ya Lissu.

Kwa ushahidi wa mazingira kupitia vyanzo vya habari kama magazeti na mitandao ya kijamii ndugu Tundu Lissu ana mgogoro wa malumbano na wapinzani watatu ambao ni,

1. Mgogoro na wawekezaji wote tu mashahidi.

2. Mgogoro na serikali kwani amekuwa mkosoaji mkuu

3. Mgogoro na maadui ndani ya chama hasa kuelekea mbio za urais 2020.

Kwa mazingira haya ni vigumu sana kubashiri ni nani hasa alitaka kumuua ndugu Tundu Lissu.

Nawasihi tuwe wavumilivu na wenye subra tuache ushabiki na ukada kwa suala linalohusu maisha ya mtu.

Mwisho naona kama kweli serikali itaunda tume ya kimahakama inaweza kuleta mwarobaini dhidi ya vitendo vya kidhalimu vinavyoota mizizi kila kukicha, hatujui kesho itatokea kwa nani.

Mungu ibariki Tanzania
 
Wewe ndiyo hakuna kitu kabisa.

Lisu ana mgogoro na kiongozi gani ndani ya chama?

Lisu ana mgogoro gani na wawekezaji ambao wana mambo hayo ya hovyo ya kutumia risasi? Lisu, miaka ya 90 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000, alifanya jitihada kubwa sana kuhusiana na rasimali za Taifa, alisafiri mpaka Canada kuwashtaki Barrick, tena akiwa hajulikani kama sasa hivi, lakini alienda huko na akarudi salama. Halafu eti leo useme ni kati ya maadui wa kufikiriwa dhidi ya Lisu?

Hizi siasa za kufikia mpaka kuuana zipo huku kwetu Afrika na Russia aliyetufundisha.

Nina imani kwa ushahidi wa kauli na vitendo, sote tunajua ni nani alitaka kumwua Lisu.
 
Mgogoro na chama si amini maana kama ni chama wangesha muuwa,muda wote wako nae hospital kwann wasimuuwe?
 
Wewe ndiyo hakuna kitu kabisa.

Lisu ana mgogoro na kiongozi gani ndani ya chama?

Lisu ana mgogoro gani na wawekezaji ambao wana mambo hayo ya hovyo ya kutumia risasi? Lisu, miaka ya 90 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000, alifanya jitihada kubwa sana kuhusiana na rasimali za Taifa, alisafiri mpaka Canada kuwashtaki Barrick, tena akiwa hajulikani kama sasa hivi, lakini alienda huko na akarudi salama. Halafu eti leo useme ni kati ya maadui wa kufikiriwa dhidi ya Lisu?

Hizi siasa za kufikia mpaka kuuana zipo huku kwetu Afrika na Russia aliyetufundisha.

Nina imani kwa ushahidi wa kauli na vitendo, sote tunajua ni nani alitaka kumwua Lisu.
Wanatengeneza story nyingine hiyo ya mgogoro na watu wa chama chake kama wale waliotengeneza kwamba huyu siyo mzalendo auwawe.

Kuna mjinga mmoja nimemlabua makofi ya kutosha leo hii kwa kunieleza huu upumbavu kama wa huyu mleta mada mjinga
 
Mada ya kipuuzi kabisa, hakuna mashindano ya kupost humu ndani. Unaweza ukajipa muda wa kutosha na akili ikafanya kazi yake vizuri hatimaye ukaja na hoja yenye mashiko. Si vyombo vya ulinzi na usalama vipo na tuliambiwa tuviache vifanye kazi yake nyie huko mtaa wa pili kwa nn mnaweweseka? Tulizeni mpira hiyo timu yenu mnayounda ya kimahakama hamuoni kama itaingilia vyombo vya ulinzi na usalama? Kila siku mnaibuka na vioja, mara kamati ya ulinzi na usalama ya Bunge, leo tena tume nyingine. Ile ya Bunge hamna imani nayo tena?
 
Umaskin wa akili ni mbaya kuliko wa mali.

Tundu anagombea madaraka gan chamani??

Unabwabwaja kama unakula popcorn
Tatizo ni kutokuelewa unapo ambiwa mgogoro ktk chama..huwezi kujua labda hao hao viongozi wake wa chama..kwakuona huyu sasa ni moto chini na anazidi kujenga JINA lake kuliko sisi..
Mfano mbona ilishaonekana kwa Mh ZITO!!!!!!!!!!?
Ilikua kila uchafu au ufisadi anaofanyika ktk awamu ya Tatu na Awamu ya Nne Mh ZITO analiripua bungeni alikua mstari wa mbele saana kuikosoa serikali ktk awamu zile..alitumbua UFISADI uliokua ukifanyika BUZWAGI MINNING hadi mawaziri husika walistaafu nyadhifa zao ....Je Leo yukwapi????aliweza hadi kuwakosoa viongozi wake wa chama kua wanakiuka KATIBA ya chama pale walipo Mchomolea kua mgombea wa urais kupitia hicho chama.
Je Leo yukwapi..
Hoja iliopo,tuwe na subira tu tuwaachie serikali na hio Tume ifanye kazi yake juu ya huu unyama tunayo fanyiwa watanzania..
 
Naona mtakuwa mmebanwa sasa mnatafuta namna ya kubuy time na stori ya kutunga.
 
Acheni siasa za majitaka, wauaji mbona mnawatetea ili iweje? nendeni mkapokee book 7 tayari
 
Tatizo ni kutokuelewa unapo ambiwa mgogoro ktk chama..huwezi kujua labda hao hao viongozi wake wa chama..kwakuona huyu sasa ni moto chini na anazidi kujenga JINA lake kuliko sisi..
Mfano mbona ilishaonekana kwa Mh ZITO!!!!!!!!!!?
Ilikua kila uchafu au ufisadi anaofanyika ktk awamu ya Tatu na Awamu ya Nne Mh ZITO analiripua bungeni alikua mstari wa mbele saana kuikosoa serikali ktk awamu zile..alitumbua UFISADI uliokua ukifanyika BUZWAGI MINNING hadi mawaziri husika walistaafu nyadhifa zao ....Je Leo yukwapi????aliweza hadi kuwakosoa viongozi wake wa chama kua wanakiuka KATIBA ya chama pale walipo Mchomolea kua mgombea wa urais kupitia hicho chama.
Je Leo yukwapi..
Hoja iliopo,tuwe na subira tu tuwaachie serikali na hio Tume ifanye kazi yake juu ya huu unyama tunayo fanyiwa watanzania..
Wewe nadhani kuna kitu unapungukiwa.

Lisu ana mgogoro gani na chama? Unabwabwaja kuhusu Zito, huku huelewi unachoongea.

Zito aliingia kwenye mgogoro kwanza kwa kukisaliti chama. Kufanya vikao na maofisa wa CCM na serikali bila ya taarifa yoyote kwa chama kipindi cha kampeni. Hakumfanya kampeni mgombea wa Urais wa chama. Alikuwa akifanya vikao na mawasiliano mengi na watu ambao ni maadui wa chama, na hakuweza kueleza vikao hivyo vilikuwa vinahusu nini?

Zito aliamua kwenda kinyume cha maamuzi ya chama yaliyokuwa yamefanywa kwenye vikao. Wakati chama kilipoamua kuwa hakimtambui JK, yeye aliamua kumtambua.

Baadaye akafanya harakati za chini kwa chini nje ya utaratibu wa chama, kutaka kupindua uongozi wa chama. Pamoja na hayo yote, chama kilimivumilia. Hata kilipoamua kufanya kikao juu ya kuamua hatima yake, aliamua kujiuzulu mwenyewe.

Hata baada ya kujiuzulu, nani alimdhuru Zito. Kuna wehu wa chama chenu wakaanza kutengeneza hadithi eti Zito amewekewa sumu lakini aliwaumbua alipokataa kuwa hakuwekewa sumu. Na hiyo ilitokana na akili ndogo za wana-Lumumba kutokuelewa maana ya food poisoning wakatafsiri kuwa aliwekewa sumu kwenye chakula. Tatizo la ujinga, ambalo hata TWAWEZA limigundua kuhusiana na wapenzi/wafuasi wa CCM (wengi wao ni wale wenye elimu na uelewa mdogo).
 
Amani iwe nanyi, tetesi nilisozipata zinatabiri kwamba Serikali imeshaunda task force kuchunguza na kubaini wahusika wa vitendo vya utekaji na utesaji dhidi ya raia na huenda ikaundwa tume huru ya kimahakama kuchunguza shambulio la Dodoma dhidi ya Lissu.

Kwa ushahidi wa mazingira kupitia vyanzo vya habari kama magazeti na mitandao ya kijamii ndugu Tundu Lissu ana mgogoro wa malumbano na wapinzani watatu ambao ni,

1. Mgogoro na wawekezaji wote tu mashahidi.

2. Mgogoro na serikali kwani amekuwa mkosoaji mkuu

3. Mgogoro na maadui ndani ya chama hasa kuelekea mbio za urais 2020.

Kwa mazingira haya ni vigumu sana kubashiri ni nani hasa alitaka kumuua ndugu Tundu Lissu.

Nawasihi tuwe wavumilivu na wenye subra tuache ushabiki na ukada kwa suala linalohusu maisha ya mtu.

Mwisho naona kama kweli serikali itaunda tume ya kimahakama inaweza kuleta mwarobaini dhidi ya vitendo vya kidhalimu vinavyoota mizizi kila kukicha, hatujui kesho itatokea kwa nani.

Mungu ibariki Tanzania

Watamchunguza na aliyetamka hadharani wanaomkosoa hawastahili Ku-Survive??AU lilitoka tu mdomoni bila kujua??Watamchungu za yule aliyekuwepo Dodoma siku ya tukio na kuonekana alfajiri Chwee hapo Morogoro??

Tusidanganyane kesi ya Nyani apelekewe ngedere,wakati Mahakama,Polisi na hta Bunge lipo chini ya mtu mmoja
 
K
Amani iwe nanyi, tetesi nilisozipata zinatabiri kwamba Serikali imeshaunda task force kuchunguza na kubaini wahusika wa vitendo vya utekaji na utesaji dhidi ya raia na huenda ikaundwa tume huru ya kimahakama kuchunguza shambulio la Dodoma dhidi ya Lissu.

Kwa ushahidi wa mazingira kupitia vyanzo vya habari kama magazeti na mitandao ya kijamii ndugu Tundu Lissu ana mgogoro wa malumbano na wapinzani watatu ambao ni,

1. Mgogoro na wawekezaji wote tu mashahidi.

2. Mgogoro na serikali kwani amekuwa mkosoaji mkuu

3. Mgogoro na maadui ndani ya chama hasa kuelekea mbio za urais 2020.

Kwa mazingira haya ni vigumu sana kubashiri ni nani hasa alitaka kumuua ndugu Tundu Lissu.

Nawasihi tuwe wavumilivu na wenye subra tuache ushabiki na ukada kwa suala linalohusu maisha ya mtu.

Mwisho naona kama kweli serikali itaunda tume ya kimahakama inaweza kuleta mwarobaini dhidi ya vitendo vya kidhalimu vinavyoota mizizi kila kukicha, hatujui kesho itatokea kwa nani.

Mungu ibariki Tanzania
Kwa hoja yako mashetani in misukule tu ndio watakubaliana nayo na sio binadamu Mwenye akili timamu.na hapa mtaona watakavofurahi hao....,
 
Kanuni moja kubwa ya kuelimika ni kujua ukomo wa uwezo wako. Sijui kwanini vijana ambao wamejua tu kusoma na kuandika wanataka kujadili mambo yaliyoko juu ya uwezo wao. Au ndio ajira za siku hizi?
 
Amani iwe nanyi, tetesi nilisozipata zinatabiri kwamba Serikali imeshaunda task force kuchunguza na kubaini wahusika wa vitendo vya utekaji na utesaji dhidi ya raia na huenda ikaundwa tume huru ya kimahakama kuchunguza shambulio la Dodoma dhidi ya Lissu.

Kwa ushahidi wa mazingira kupitia vyanzo vya habari kama magazeti na mitandao ya kijamii ndugu Tundu Lissu ana mgogoro wa malumbano na wapinzani watatu ambao ni,

1. Mgogoro na wawekezaji wote tu mashahidi.

2. Mgogoro na serikali kwani amekuwa mkosoaji mkuu

3. Mgogoro na maadui ndani ya chama hasa kuelekea mbio za urais 2020.

Kwa mazingira haya ni vigumu sana kubashiri ni nani hasa alitaka kumuua ndugu Tundu Lissu.

Nawasihi tuwe wavumilivu na wenye subra tuache ushabiki na ukada kwa suala linalohusu maisha ya mtu.

Mwisho naona kama kweli serikali itaunda tume ya kimahakama inaweza kuleta mwarobaini dhidi ya vitendo vya kidhalimu vinavyoota mizizi kila kukicha, hatujui kesho itatokea kwa nani.

Mungu ibariki Tanzania
Watanzania Nani katuroga?
Tumia akili kama Hakuna cha kupost kuwa kimya
 
Kusema tume huru ni maneno tu. Sote tunajua mtu moja kaiweka mahakama na bunge chini yake. Kua huru ni maneno tu ya kwenye karatasi ila vitendo ni tofauti kabisa.

Jambo la Lissu silaumu mtu wala serikali maana yaweza kua yeyote yule, haya mambo muda mwingine unakuta ni mtu tofauti kabisa kafanya kwa nia flani. Ila kuhusu uhuru hakuna uhuru zaidi ya maneno tu. Kila kitu kinamzunguka mtu moja sa hivi kwa uoga uliogeuka kuitwa uzalendo
 
Tatizo ni kutokuelewa unapo ambiwa mgogoro ktk chama..huwezi kujua labda hao hao viongozi wake wa chama..kwakuona huyu sasa ni moto chini na anazidi kujenga JINA lake kuliko sisi..
Mfano mbona ilishaonekana kwa Mh ZITO!!!!!!!!!!?
Ilikua kila uchafu au ufisadi anaofanyika ktk awamu ya Tatu na Awamu ya Nne Mh ZITO analiripua bungeni alikua mstari wa mbele saana kuikosoa serikali ktk awamu zile..alitumbua UFISADI uliokua ukifanyika BUZWAGI MINNING hadi mawaziri husika walistaafu nyadhifa zao ....Je Leo yukwapi????aliweza hadi kuwakosoa viongozi wake wa chama kua wanakiuka KATIBA ya chama pale walipo Mchomolea kua mgombea wa urais kupitia hicho chama.
Je Leo yukwapi..
Hoja iliopo,tuwe na subira tu tuwaachie serikali na hio Tume ifanye kazi yake juu ya huu unyama tunayo fanyiwa watanzania..
Wewe unakili kama bashite! Twambie zitto alifukuzwa CHADEMA kwa kutaka kugombea uraisi? Mawaziri hawakustaafu walifukuzwa ipo siku utawambia watoto wako kitwanga alifukuzwa utachekwa. Huyo lisu anataka kugombea nafasi gani hapo CHADEMA!? Kama hujui jua kwamba mh. Mbowe huyu mnaemtukana kila siku kuwa anawaua wapinzani wake ndiyo aliyewaita hawa wote cdm. Jiulize leo kama mwenyekiti wa cdm angekuwa huyo zitto au kitila tungekuwa tunaongea nn ?
 
Amani iwe nanyi, tetesi nilisozipata zinatabiri kwamba Serikali imeshaunda task force kuchunguza na kubaini wahusika wa vitendo vya utekaji na utesaji dhidi ya raia na huenda ikaundwa tume huru ya kimahakama kuchunguza shambulio la Dodoma dhidi ya Lissu.

Kwa ushahidi wa mazingira kupitia vyanzo vya habari kama magazeti na mitandao ya kijamii ndugu Tundu Lissu ana mgogoro wa malumbano na wapinzani watatu ambao ni,

1. Mgogoro na wawekezaji wote tu mashahidi.

2. Mgogoro na serikali kwani amekuwa mkosoaji mkuu

3. Mgogoro na maadui ndani ya chama hasa kuelekea mbio za urais 2020.

Kwa mazingira haya ni vigumu sana kubashiri ni nani hasa alitaka kumuua ndugu Tundu Lissu.

Nawasihi tuwe wavumilivu na wenye subra tuache ushabiki na ukada kwa suala linalohusu maisha ya mtu.

Mwisho naona kama kweli serikali itaunda tume ya kimahakama inaweza kuleta mwarobaini dhidi ya vitendo vya kidhalimu vinavyoota mizizi kila kukicha, hatujui kesho itatokea kwa nani.

Mungu ibariki Tanzania
Kama time ya uchaguz haijawa huru he hiyo time ya kuchunguza wanaotesa raia ndo itakuwa huru ,tuhire experts kutoka nje ,mgonjwa anajichagulia dawa tangu lini
 
Vijana was Lumumba mbona mko rahisi sana kujulikana ?hamuwezi weka Uzi wa maana mpaka porojo za kitoto
 
Back
Top Bottom