Serikali kuwabana zaidi waagizaji Magari yaliyotumika ili kulinda uzalishaji wa ndani

Mahindra sio gari za kusema wabane Kampuni used kama Land Cruiser,Ford Ranger na Nissan wao wawaruhusu kuja kushindana na si kufanya kama Mwendokasi harafu baadae wakaferi Nchi yenyewe haina magari ya kutosha zaidi ya hizo V 8 za kodi harafu mnataka Wananchi waendelee kubanana kwenye Bus...
 
Tanzania Kuna uzalishaji upi wa ndani wa magari? Upuuzi
 
Serikali nayo inunue magari hayohayo ya mwekezaji ili kumlinda na ku-support uwekezaji.

Huyo muwekezaji mmoja hawezi kutosheleza hitaji la aina ya magari yanayohitajika nchini kiasi iwepo sheria ya namna hiyo.

Hata ingekuwa ni Toyota mwenyewe anakuja bado mahitaji ya trucks watu watahitaji kuagiza scania za 450,000Km odo ndiyo wanazimudu.

Tope la Hanang limejaa kwenye vichwa vya wenye dhamana.
 
Wangeenda kujifunza Rwanda wanachofanya. Wao Wana viwanda vya Magari huko kwao. So polepole wanaanza kuzuia uagizwaji wa mitumba.
 
Watengeneze tu lakini watayauza kwa nani. Kama kipato cha Mtanzania kinamruhusu kununua gari lililotumika. Nimeyaona magari ya mahindra hayana kiwango kama magari kama toyota, harrier, vanguard yaliyotumika.
 
Umeeandika serious sana ila we know hayo ni matamko yakumfurahisha mwekezaji, Serikali yenyewe tu haiewezi kununua gari inaitwa Mahindra…hizi zitakua za ma Gabachori ambao kabla ya hapo walikua wanaimport from India.
 
Kwani lazima kuendesha magari? Baiskeli ni nzuri kwa mazoezi pia zipo pikipiki ndogo za umeme ni cheap na zipo nyingi siku hizi. Tunajaribu kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi.
 
Hili serikali letu hapana.
Juzi tu wamepitisha sheria serikali inunue magari ya aliyotumika kwa ajili ya taasisi za serikali,alafu wananchi wako unawawekea ngumu wanaunue mapya.
Hivi ni lini watanzania tutaoka tuseme hapana? Tuwakatae hawa watu. Wahuni,wezi hawana nia njema kwa watanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…