Serikali: Kwa sasa Tanzania ina wagonjwa 66 wa Corona nchi nzima ndani ya mikoa 10 na mikoa 16 haina wagonjwa

Ilishasemwa ukiwa muongo uwe na kumbukumbu.

Wengine wakadai njia ya muongo ni fupi.

Sasa twajionea!
 
Bila hata ya aibu mikoa isiyo na Corona ni pamoja na hii ya mipakani: Kagera, Mara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga ambako kila anayetusaidia kutumia, watu wetu ni Corona kwa kwenda mbele.

Kwa hili la ugonjwa huu pana watu wamejiweka wazi kuwa katu si wa kuaminika kwa lolote walisemalo na hata kwa walifanyalo.

Jidhanieni kuwa tunadanganyika na hizi longo longo zenu zisizokuwa na vichwa wala miguu.

Tanzania Finally Announces The Actual Number Of Coronavirus Patients in The Country

Mbona waungwana walishasema sana: "you can't fool all the people all the time."
 
ifikie hatua serikali ikae KIMYA kuhusu corona.
Kama tumeamua kuishi nayo tuishi nayo.
Haya matamko huyu kasema wapo 4 mwingine kasema wapo 66 ni wazi MNATUDANGANYA.
kama mmeamua kuipotezea ipotezeeni mazima.

Vipi mkuu? Na wewe unaanza kutumika na mabeberu?

Cha ajabu nini hapo mkuu? Kupungua kutoka 4 hadi 66?

Wewe hushangai mikoa ya mipakani kutokuwa na maambukizi kabisa?

Hiyo si ndiyo ya kustaajabu ya Mussa sasa? Hakuna la ajabu hapo mkuu.

Wewe ufahamu kuwa Corona haipo bila kujali nani anasema nini, au vipi mkuu?
 
Wawe na kauli MOJA.
 
Wawe na kauli MOJA.

Kwa maana ya kuwa uongo uongo tu mkuu?

Kwa nini isiwe ukweli ukweli tu mkuu? Sidhani kama hawa mabwana tuliwapa dhamana ya kutuongopea sisi kama wanavyoita wao.

Ni wao walipenda kusema msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Yameishia wapi ya kusema ukweli?

Nadhani tunavyokwenda hawa mabwana siyo!
 
Duniani kote data zinabadilika Kila siku. Mfano China ilikuwa imebaki na wagonjwa 45 lakini Sasa Ina wagonjwa zaidi ya 200!

Kwa hiyo hata China wagonjwa huwa wanaweza kupungua kituko 45 hadi 200?
 
Hakuna anayeongopa hapo.
Ila HAWANA USHIRIKIANO.
 
Kwakweli watu wamepoteana kama mnara wa babeli
 
Covid19 haiondolewi kwa matamko. As long as mipaka ipo wazi and every Tom & Dick can pop in at any time, ni upuuzi kudeclare eti Tanzania ni “covid-free”.
Tatizo ni misifa imezidi. Watu wamelewa sifa. Mara wagonjwa wanne, mara 66, mara Corona haipo. What is this?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…