Serikali lawamani kuruhusu Mkusanyiko wa Maelfu kwenye Kilimanjaro Marathon wakati Taifa linapambana na Virusi vya Korona

Serikali lawamani kuruhusu Mkusanyiko wa Maelfu kwenye Kilimanjaro Marathon wakati Taifa linapambana na Virusi vya Korona

Hawana hofu kwa kuwa wanahisi bado vijana na wenye afya tele, ni kweli ila mnawapelekea wenye afya mgogoro na wazee ambao bado walikuwa na wakati wa kuishi, hivyo mnakatisha maisha yao, pamoja na maneno yenu yasio na huruma kuwa siku zake zimefika, au kufa lazima angekufa tu hata kwa sababu nyingine!
 
Covid sio ugonjwa hatari, umekuwa overated, nimeugua huu ugonjwa mara 2 na sasa nahisi naumwa corona nasubiria tu harufu ikate nianze dose. Mara zote 2 sikunywa dawa yyt na nimepona. Death rate ni asilimia 3 ya waathirika wote hivo 3% ni ndogo sanaView attachment 1714198
Maybe so maybe not - 3% ni ndogo sana ikiwa haumo au ndugu yako hayumo kwenye takwimu hiyo.
 
Hapa hakuna wa kulaumiwa kila mtu afe kivyake [emoji2958]
 
Hivi mpaka leo Kuna watu wanaamin barakoa zinasaidia eeh
Me nawashaur tu ikiwezekana hameni nchi nenden huko wanakoo vaa hizo barakoa na hawana misongamano...
Huyu Mungu anayewalinda na kuwaponya Watanzania tu akiacha dunia ikiteketea pamoja na Italia kwa Mwakilishi wake namba 1 Baba Mtakatifu ni Mungu kweli au ni mmoja wa miungu ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara toka dunia iumbwe?

Mara tuambiwe Covid-19 Tanzania haiko ila kuna Changamoto ya Kupumua na Pneumonia kali tu ambazo zinapona kwa kujifukiza tu au watu wajilinde kwa kuvaa Barakoa zilizoshonwa na viwanda vyetu vya Cherehani Nne maana za mabeberu zina Coronavirus.

Tunachanganyikiwa!
 
Watu walikuwa wengi kwelikweli, ni maelfu ya watu wamekusanyika kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Kilimanjaro Marathon. Miongoni mwao wapo ambao hawakuvaa barakoa kabisa, na wamo amabao walizivaa na kuzivua...
Watu wameaminishwa na wakaamini kuwa maombi yameiondoa corona. Na viongozi kuendelea kukusanya watu kwenye mikutano ya kisiasa ni mwendelezo wa aminisho hilo.
 
Ila watanzania tunastahili lawama kwa kiwango cha juu sana, haiwezekani pamoja na taarifa zote kuhusu Corona zinazosambaa kwenye mitandao na vyombo vingine vya habari japo huko wanaita "nimonia", bado kuna watu hawachukui tahadhari mpaka leo....
Kiwango cha uelewa kinakuwa sambamba na elimu mhusika. Kiwango cha wastani wa elimu Tanzania ni chini ya std 7, usitarajie maajabu.
 
Waandaaji washapiga hela wamesepa kurudi south Afrika.
 
Watu walikuwa wengi kwelikweli, ni maelfu ya watu wamekusanyika kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Kilimanjaro Marathon. Miongoni mwao wapo ambao hawakuvaa barakoa kabisa, na wamo amabao walizivaa na kuzivua...
Kule Marekani BML na PB waliandamana pamoja na kuwa na Covid,kamawao wanaweza kwanini sisi tusiweze?acheni ujinga.
 
Watu wameaminishwa na wakaamini kuwa maombi yameiondoa corona. Na viongozi kuendelea kukusanya watu kwenye mikutano ya kisiasa ni mwendelezo wa aminisho hilo.
Kwani mbona Maalim seifu watu wanajua kafa kwa corona na hata huku mitaani watu wanajua kama corona ipo na ndio maana baadhi huvaa barakoa wakati mwaka jana waliacha kuvaa,kwahiyo sio kwamba watu wameaminishwa hakuna corona bali nachokiona mimi ni kwamba watu hawaoni athari za huu ugonjwa hawaoni kilichobadilika na ndio maana hawana hofu wanaendelea na maisha kama zamani.
 
Ila watanzania tunastahili lawama kwa kiwango cha juu sana, haiwezekani pamoja na taarifa zote kuhusu Corona zinazosambaa kwenye mitandao na vyombo vingine vya habari japo huko wanaita "nimonia", bado kuna watu hawachukui tahadhari mpaka leo...
Namuona RC Anna Mghwira hapo, this means serikali imeridhia usambaaji huo wa ugonjwa. This is the ultimate level of stupidity.
 
Huu ni uthibitisho kuwa hakuna corona kivile!! Viwanja vya mpira vinajaa kila weekend!! Kwenye dala dala hakuna cha siti levo! Sokoni ndio usiseme!! Mashuleni, vyuoni!! Kama tungekuwa na corona yenyewe, ndani ya wiki moja pasingekalika!! Vifo havifichiki!! Vifo tunavyoshuhudia ni vya kawaida. Hakuna muda wowote usiokuwa na vifo!
Huu ndio ukweli.
 
Watu pale wanapokuwa hawaoni uhatari wa ugonjwa kwenye uhalisia kwa kiwango kinachoelezwa hapo ndipo wanapoacha kuzingatia kujikinga na huo ugonjwa,kuna muda tulikataa kurudishwa Tanzania wale wanafunzi wa kitanzania kutoka kule china kutokana na hofu ya huu ugonjwa ila toka tutangaziwe kuingia huu ugonjwa nchini kadri siku zinavyoenda watu wanazidi kupuuzia mpaka sasa inaonekana ni ugonjwa wa wazee.
 
Katika mazingira kama haya, serikali inaruhusuje mikusanyiko kama hii?
Huwezi kukimbia huku umevaa barakoa,utakufa fasta.

Serikali ilishasema haitofungia wala kupiga marufuku mikusanyiko,ikasisitiza watu kufuata masharti.

Hao watu wameenda wenyewe baada ya kujifanyia tathmini, halafu aliekwambia wanamicho wanaathirika kwa covid ni nani.
 
huwezi kukimbia huku umevaa barakoa, utakufa fasta...
Wao wasipoathirika, watabeba virusi na kuja kuambukiza wazee na watoto ambao nao wataenda kuambukiza family members na community zao mitaani.

Ugonjwa una side mbili. Athari kwa mhusika mwenyewe au la basi mhusika kuambukiza wengine
 
Watu walikuwa wengi kwelikweli, ni maelfu ya watu wamekusanyika kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Kilimanjaro Marathon. Miongoni mwao wapo ambao hawakuvaa barakoa kabisa, na wamo amabao walizivaa na kuzivua...
Tutabakia kuwa wakutazamwa kama migrating beasts wa Serengeti
 
Corona kweni iko wapi?

Nyie wabongo vipi?
 
Back
Top Bottom