Serikali mkoani Mwanza yaamuru wamachinga wote kuondoka ifikapo Jumatatu, 15/4/2013

Serikali mkoani Mwanza yaamuru wamachinga wote kuondoka ifikapo Jumatatu, 15/4/2013

YAGHAMBA

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2012
Posts
545
Reaction score
147
Wakuu jana na leo gari la matangazo limekuwa likipita mitaa mbalimbali ya jiji la Mwanza na vitongoji vyake likitangaza tangazo la serikali ya CCM la kuwaamuru wamachinga wote, mama ntilie na wote wa kufanana nao kuondoka katikati ya jiji na sehemu zote 'zisizoruhusiwa' kabla ya siku ya jumatatu tarehe 15 Aprili 2013.

Tangazo hilo lenye vitisho vingi vyenye mwelekeo wa kuwadhuru wale wote watakaokaidi amri hiyo, limekuwa gumzo kubwa hapa jijini miongoni mwa wamachinga na wananchi wote kwa ujumla huku ikileta hofu kubwa ya kutokea maafa makubwa ikiwa litatekelezwa kwa namna ambavyo maneno ya tangazo hilo yanavyotamkwa na mtangazaji.

Mtangazaji amekuwa akisema kauli hizi " Kama unaipenda familia yako tii amri hii ya kuondoka ktk eneo unalofanyia biashara za umachinga kwani operation hii itakuwa kubwa na haina msalia mtume" na manenon mengine mengi yenye kutia hofu.
 
Waondoke waende wapi?..Nauli zenyewe ziimepanda, huko wanakowataka waende kunafikika? Pili lugha ya kistaarabu, heshima lakini yenye ONYO ingefaa zaidi kuliko kuwapatia hofu 'wanafamilia'.
 
Naunga mkono. Hili ni jiji sa hv,kama sivyo wamachinga wa magomeni/ama machinga complex wapelekwe posta wapange vitu chini uone kama kutakuwa na raha yeyote ktk kutembea kwa kuhofia unaweza kanyaga bidhaa.
Mfano wa makoroboi mwanza aliyekodi chumba cha biashara analipa millioni 5 na kuendelea kwa mwaka anauza viatu,halafu wakati huo huo mlangoni pake anaweka machinga anayeuza product zinazofanana na zake iwe viatu etc na halipi kodi kama mwenye rum,what do you expect? Watolewe wapelekwe sehemu nyingine
 
nisisikie mmewagusa mkitaka kuona nguvu ya mlevi mwaga pombe yake.
 
CCM imewanyima watanzania elimu, wanafunzi wanamaliza drs la saba hawajui kusoma wala kuandika, wanaobahatika kwenda sekondari 90% wanapata div 0 na div 4, wachache wanaendelea na kidato cha tano na sita, wanaobahatika kwenda chuo kikuu wananyimwa mikopo na wanashindwa kwenda chuo, wanajiunga na wale wengine mitaani, wanajiajiri na wanakuwa wamachinga. Leo serkali ileile iliyowapuuza kwenye elimu inakuja kuwafurusha kwa kuharibu bidhaa zao ambazo mitaji yenyewe wameipata kwa taabu na kuwatia vilema vya maisha na wengine kuuawa huku serikali hiyohiyo ikiwakumbatia wawekezaji uchwara wanaotuibia kwenye sekta za madini na nyinginezo. Hakika serikali ya CCM imekosa uhalali wa kutawala. Lazima ing'oke.
 
Machinga wa Mwanza, tujikumbushe ule mtiti wa mwaka jana chini ya wabunge wetu wapendwa, Highness Kiwia na Wenje wa CHADEMA jinsi tulivyokomaa hadi leo tunauza na kuendesha maisha. Wale wachache waliopewa pesa na ccm wakaacha kaz hii tunawapongeza, lakn wajue wanatumika tu, ladha iliisha watatemwa. Haya ni mapambano kati ya mafisadi na wenye nchi. Cha ajabu kesho utamsikia Mwigulu anakuja kutuhadaa. Ccm gudbai
 
machinga imetowehewa kutoka neno la kiingereza matching guy ambao hutembeza biashara zao.ni haki ya wamachinga kutembeza biashara zao kokote ni hii serikali iliyopitwa na wakati isiyoelewa.
 
Back
Top Bottom