Wanabodi
Matokeo ya darasa la 7 mwaka huu ni mabaya sana waziri atayatangaza mwezi huu au mwanzoni mwa januari.
Mpaka maafisa elimu wameambiwa wachukue waliopata 70 badala ya 100 na kuendelea hawa wakifika sekondari mwaka jana waliofaulu hawajui kuandika wala kusoma 5000 mwakani watakuwa maelfu.
Wakikutana na walimu waliopuuzwa kwa madai yao ya msingi tutegemee bomu.
Hayo yakiwa yanajiri viongozi wetu hasa vijana wanahangaika na Dr slaa kaondoka na kadi yake aliyonunua alipokuwa ccm
Huku wa serikali anzia kesho wakianza kueleza mafanikio swali la kujiuliza hayo mafanikio hayaonekani mpaka yaelezwe yatangazwe
Wakifanya hivyo darasa la 7 au kiwango cha elimu kitakuwa, kero za walimu zitatulika na mlo mmoja kwa siku itakuwa miwili.
Tatizo la ajira litapungua kwa kusikia maendeleo
Mie nashukuru wanayatangaza wakati watazima matangazo ya analog watayaona wao kwa wao wenye vingamuzi na ma dstv mwananchi wa kawaida atakuwa anapotezwa na habari za tv anarudishwa enz za kusikiliza mkulima redio