serikali mmeona madhara ya kutowasikiliza walimu

serikali mmeona madhara ya kutowasikiliza walimu

serikali inabidi ijiulize upya, jua ukikamatwa ugoni kwa mke wa mtu thn mwenye mke mke akakuambia we nenda tu nimekusamehe nina hakika utaomba adhabu mwenyewe na ndivyo ilivyo kwa mgomo baridi ni hatari zaidi bora wangegoma mpaka hasira zao zingeisha halafu wangerudi kazini haya yasingetokea TULIOMBEE TAIFA
 
Its so sad Tanzania kuporomoka kiasi hiki ila siasa ni mbaya yaani elimu ni ustawi wa nchi lkn inapuuzwa. Haya ngoja tuone.



Sent from my GT-N7100 using Tapatalk 2
 
Nawatamani walioko huko madarakani!!?? yaani nawatamani, wamshukuru shetani wao lakini kadri siku zinavyosonga hasira zetu zinaongezeka, siku yaja nasema tutafukua hadi makaburi yao kule ismani na msoga ili tuwahukumu, hakika halitasalia jiwe juu ya jiwe kwa udhalimu huu wanaotutenda
 
Mgomo baridi ni hatari.JK alisema walimu watumie za mbayumbayu na wakamsikia mkuu wa nchi yao .kwa hili nimewakubali.inasemekana wanafunzi wa primary 2012 wamefeli hadi kufikia hatua ya wanafunzi wenye maksi 70 badala ya maksi 100 nao kuruhusiwa wachaguliwe wajiunge na secondary 2013.kwani wanafunzi wamefeli sana.na hii ni kutokana na serikali kutowasikiliza walimu kilio chao cha kuongezwa mshahara na kulipwa madai yao.VIVA WALIMU.MSHIKAMANO DAIMA
Hivi siyo Blandina kweli huyu...?!
 
Jk si amesema mwalimu wa primary awe na dergree au?? ndio kwamba watafaulu sana??
 
duuu ....! 70/250 = 28%. Mimi nakumbuka mwaka 1997 nilifaulu kwenda hapo mzumbe kwa alama 142/150= 94.7% hivi! Yaani
hisabati 50,maarifa 44 na lugha 48! Sasa ... Daaah! I hate politics.... I hate politicians...... I hate .....all dhaifu people! Over..



mm nakumbuka nilikuwa na marks 126 katika masomo ma 3 mwaka 2004 ila hawakunichagua first selection

sasahv katika masomo matano hata kufikisha marks 100 hawawezi....

Kama hii hali itaendelea kutakuwa na wimbikubwa la vilaza#

kama magamba wasipozisikiliza shidazetu bac am sure chadema watazisikiliza na kuzitatua.

baada 2015 ccm tutakiita chama cha upinzani#
 
Mtu aliyekata tamaa ni hatari sana kwani haoni shida hata kuidhuru nafsi yake sembuse ya mtu mwingine. Walimu katika nchi hii wamekata tamaa na haya yanayotokea sasa ni zao la kukata tamaa na kupuuzwa kwao kwa muda mrefu. Maadam tuliowapa dhamana wanajifanya hamnazo basi tutegmee udhaifu mkubwa zaidi katika elimu hapa TZ.
 
Serikali ya ccm ni kipofu na haina uwezo wa kuleta maendeleo ya maana zaidi ya kukurupuka kufanya madudu kama kawaida yake.Watanzania ifike mahala tuone umuhimu wa kubadili mfumo mbovu wa uongozi wa serikali hii dharimu inayoongozwa na porojo za viongozi mafisadi wanafiki ,vigeugeu,waroho wa madaraka vinginevyo tutaendelea kulalamika kila siku.
 
Mgomo baridi ni hatari.JK alisema walimu watumie za mbayumbayu na wakamsikia mkuu wa nchi yao .kwa hili nimewakubali.inasemekana wanafunzi wa primary 2012 wamefeli hadi kufikia hatua ya wanafunzi wenye maksi 70 badala ya maksi 100 nao kuruhusiwa wachaguliwe wajiunge na secondary 2013.kwani wanafunzi wamefeli sana.na hii ni kutokana na serikali kutowasikiliza walimu kilio chao cha kuongezwa mshahara na kulipwa madai yao.VIVA WALIMU.MSHIKAMANO DAIMA

Wanajifanya hawakubali lakini Athari za PASSIVE RESISTANCE ya walimu zaanza kuonekana, serikali yashusha viwango vya ufaulu huku ikijinasibu eti kiwango cha ufaulu kimepanda. Wadanganyeni hao hao wasiojua kuchanganua mambo. Kauli hii ya waziri kwamba ufaulu umepanda ni sawa na ile isemayo uchumi wa nchi umekua wakati hali ya mwananchi wa kawaida inazidi kudidimia.
Matokeo ya Mtihani wa kumaliza elimu ya msingi ni matokeo ya ubabe wa serikali. Matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka huu ni vituko na aibu kubwaaa! Baada ya serikali kukomaaa kutowasikiliza walimu na kukimbilia mahakamani kukwepa na kusitisha mgomo wa walimu leo wameamua kushusha kiwango cha ufaulu. Kwa mara ya kwanza Eti mwaka huu wanafunzi waliopata alama D yaani alama chini ya 100 wamefaulu na kuchaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari. Ni ajabu kusikia kuwa kuna wanafunzi wenye alama 70 mpaka 50 wamechaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari. Bado tuna bomu kubwa tunalisubiri la idadi ya wanafunzi walioingia kidato cha kwanza wasiojua kusoma na kuandika, maana yake mtihani wenyewe ulikuwa wa kuchagua hadi somo la Hesabu, aibu kubwa kwa nchi hii. “Shame of this Government”.
 
Back
Top Bottom