Serikali na DPP mnakwamisha sana Haki

Serikali na DPP mnakwamisha sana Haki

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2018
Posts
21,711
Reaction score
35,644
Kumekuwa na Kundi kubwa sana la wananchi wakisota Rumande kwa kile kinachotajwa kuwa "UPELELEZI HAUJAKAMILIKA" hii kitu imekuwa adui mkubwa sana wa haki za watuhumiwa.

Kuna jamaa flani hapa mtaani amekaa rumande/jela kwa miaka miwili kwa kesi ya uhujumu uchumi, alikuwa mtuhumiwa namba mbili, kufuatilia polisi wanasema wameshamaliza upelelezi mwaka jana ila file lipo kwa DPP, kesi inatajwa mahakamani na kuahirishwa kila mara.

Kuna watu wapo "ndani" 10+ yrs kwa kisingizio cha upelelezi.

Kesi ya kubaka mwanamke mwathirika akishaoga tu ushahidi umeisha unachunguza nini miaka na miaka

Kwa style hii DPP amekua kikwazo kikubwa sana cha haki kutendeka.

Hapo huzazungumzia maamuzi mabovu ya mahakimu yanayoelekea kuupendelea "kuhimili uliojichimbia chini zaidi" wakitarajia kulipwa fadhila kwa kuteuliwa UJAJI.

Muhimili wenye kina kirefu ndio unaopanda aina ya hukumu inawafaa watuhumiwa hasa wanasiasa rejea wanachama wa CCM wanaotuhumiwa kutoa rushwa hapo husikii TAKUKURU wakijinasibu kuwaweka ndani licha ya kuwepo kwa clips zao. Tuje kwa mtoto wa Lowasa, Ndugu wa Rostam Aziz, Mbunge wa Siha alikuwa na kesi ya kufoji kitambulisho ya TISS

mambo ni mengi ila ndio hivyo......
""tumipenda wenyewe, chaguo letu wenyewe, na wavimbe wapasuke,
Wacha tuisome namba.""
search.jpg


nawasilisha
 
Uzi wako huu ni mzuri na hata Mimi nilianza Kuupenda hasa kwa Hoja zako za mwanzoni, ila mwishoni ulipokitaja tu Chama cha CCM umeuharibu.
 
Uzi wako huu ni mzuri na hata Mimi nilianza Kuupenda hasa kwa Hoja zako za mwanzoni, ila mwishoni ulipokitaja tu Chama cha CCM umeuharibu.
Hoja inahusu mhimili mkubwa kupindisha haki kwa maslahi yake
 
Hoja inahusu mhimili mkubwa kupindisha haki kwa maslahi yake

Kama ni hivyo CCM hapo kama Chama Kimeingiaje? Acha kwenda Kinyume na maana nzima ya Jina lako. Tendea Haki dhana ya Einstein sawa?
 
Kama ni hivyo CCM hapo kama Chama Kimeingiaje? Acha kwenda Kinyume na maana nzima ya ID yako. Tendea Haki dhana ya Einstein sawa?
Nimetaja wanachama wa ccm ambao kutokana na uchama wao kesi zao zinafutwa juju kwa juu na majina nimewataja sassa unahitaji nikutajie nini zaidi?
 
Ukitaka majibu ya ukandamizaji huu wa Serekali na DPP - chagua Tundu Lisu.
 
Mkuu Serikali ya CCM inatabia ya ku-influence ya maamuzi ya DPP na mahakama najua unalifahamu hilo ila unataka ligi tu

Una 'Ushahidi' Kuntu ( Vividly ) juu ya haya Madai yako au ni Chuki yako tu dhidi ya Chama cha Mapinduzi na Mbeba Bendera wake Rais Magufuli?
 
Una 'Ushahidi' Kuntu ( Vividly ) juu ya haya Madai yako au ni Chuki yako tu dhidi ya Chama cha Mapinduzi na Mbeba Bendera wake Rais Magufuli?
Mifano waijua
nakuongezea clip ya sauti ya Dr. Mwanjelwa inazunguka mitandaoni
 
CCM ni Chama Cha Maovu. Kwa mantiki hiyo haki haiwezi kuingatiwa na kulindwa na ccm.
 
Watoa rushwa wa CCM wamekua kaa la moto kwa TAKUKURU
 
Back
Top Bottom