Serikali pitieni upya Sera ya 'Elimu Bure', ikiwezekana ifutwe kabisa

Serikali pitieni upya Sera ya 'Elimu Bure', ikiwezekana ifutwe kabisa

Ingawa ni jambo jema kwa serikali kutoa elimu bure ili kusaidia watoto watokao kaya maskini kupata elimu ya msingi lakini huu mpango unafaa kuangaliwa upya kwa sababu utekelezaji wake una hasara nyingi kuliko faida.

Hasara ya kwanza: Tangu kuanzishwa kwa sera ya elimu bure, serikali imeshindwa kuajiri walimu wa kutosha na hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa walimu hususani wa masomo ya sayansi mashuleni na hivyo kupelekea wanafunzi wengi kufeli masomo hayo katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Kadhalika, ukosefu wa walimu pia unachangia wanafunzi kukata tamaa ya kusoma baadhi ya masomo hasa ya sayansi na wengine huamua kuacha shule kabisa na kujichanganya mtaani. Hii yote ni kwasababu serikali inatumia gharama kubwa zaidi ya billions 20 kwa mwezi kuhudumia elimu bure na hivyo kupunguza kiwango cha bajeti cha kuajiri walimu wapya kwa mwaka.

Hasara ya pili: Kufuatia mpango wa elimu bure, upatikanaji wa vifaa muhimu vya kufundishia na kujifunzia kama vile vitabu, vifaa vya maabara na kemikali za kufanyia majaribio upatikanaji wake umekuwa sio wa kuridhisha na hivyo kufanya walimu pamoja na wanafunzi kujifunza katika mazingira magumu. Hii inaweza kuwa inachangiwa na ucheleweshaji wa kupeleka pesa za kuhudumia elimu bure katika baadhi ya halmashauri au bajeti kubwa kupelekwa kwenye ujenzi wa miundo mbinu ya shule na kusahau eneo muhimu la ununuzi wa vifaa vya kielimu.

Hasara ya tatu: Serikali inatumia gharama kubwa kulipia wanafunzi ada ambao saa nyingine huamua kuacha ama kufukuzwa shule na hivyo kufanya serikali kuingia katika gharama zisizokuwa na msingi.

Hasara ya nne: pamoja na serikali kutoa elimu bure bado kuna changamoto ya madawati na hivyo kupelekea wanafunzi kusoma katika mazingira duni ya kukaa chini hasa katika vipindi vya darasani.

Hasara ya tano: Tangu serikali ianze kutoa elimu bila malipo kumekuwepo na ufuatiliaji mdogo wa wazazi kuhusu maendeleo ya watoto wao(wanafunzi). Hali hii inachangia kushusha kiwango cha taaluma mashuleni kwakuwa ufuatilaji wa maendeleo ya wanafunzi kwa asilimia kubwa umekuwa ukifanywa na walimu pekee. Katika hili, wazazi wamejiweka kando kutokana na kwamba hakuna hasara yoyote wanayopata kwakuwa gharama zote zinalipwa na serikali.

Hasara ya sita: Elimu bure imechangia kudumaza ushiriki wa wazazi katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo. Mfano, ushiriki katika ujenzi wa shule, ushiriki katika upanuzi na ujenzi wa madarasa. Linapotokea suala la kuchangia shughuli kama hizo wazazi wamekuwa wagumu wa kuchangia huku wakidai ni elimu bure hivyo hatutakiwi kuchanga chochote.

Kufuatia hasara hizo na zingine ambazo hazijatajwa, napendekeza elimu bure ifutwe badala yake wazazi waendelee kulipa ada na serikali ifanye yafuatato:

1. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kununua na kuhakikisha kuna vifaa vya kutosha vya kielimu mashuleni.

2. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kuhakikisha kuwa kuna upatikanaji wa madawati ya kutosha mashuleni ili watoto wasiendelee kukaa chini.

3. Serikali itumie bajeti ya elimu bure kuajiri walimu wa kutosha mashuleni ili kuinua kiwango cha taaluma katika sekta ya elimu.

4. Utekelezaji wa elimu bila malipo uanze baada ya changamoto zote kwenye sekta ya elimu hususani mashuleni kufanyiwa kazi.

5. Hakuna haja ya elimu bure kwakuwa wazazi wanao uwezo wa kusomesha watoto wao lakini hawana uwezo wa kuwaajiri katika ujira wa kudumu. Hivyo ipo haja ya bajeti ya elimu bure kutumika kuangazia kutoa fursa za ajira kwa vijana.

6. Kama kuna umuhimu wa Sera ya elimu bure kuendelea kuwepo basi ihamishiwe katika ngazi ya elimu ya juu(vyuo vikuu) kwakuwa ndiko kwenye gharama kubwa kuliko huku chini ambako mzazi anaweza kupambana kwa biashara ya kuuza ubuyu, karanga au kilimo cha bustani na kumsomesha mwanae.
Mkuu,

Usilete mawazo mfu kwenye jukwaa la JF utaghadjabisha wengi labda kama ni watetezi wa umwinyi na ubwanyenye kwamba waliokuwa nacho ndio wapate elimu kisha waje wawatawale wajinga hili haliwezekani kwa sasa.

Kwanza wigo wa kuto elimu bila malipo ya ada unatakiwa upanuliwe hadi kidato cha sita, vyuo vyote vya kati huku vyuo vikuu wanafunzi wote wanaochaguliwa kujiunga wapewe mikopo sawia kwa asilimia 90% hadi 100% na marejesho baada ya kumaliza upungzwe had asilimia 8% badakla ya asilimia 15% inavyofanyika kwa sasa..

Inavyoonesha wewe unamgongano wa maslahi kwamba unapata ushindani mkubwa na huna uwezo kujipangia ada ba malipo mengine yanayoumiza jwassiokuwa nacho.

Wananchi hawataki mawazo yako ya kibinafsi yaliyolenga kuimarisha biashara yako ya uendeshaji wa shule au taasisi za utoaji elimu kwa gharama kubwa yenye kuleta faida badala ya kuwa ni huduma.
 
Mtoto wa mwanasiasa gani anasoma huko? Ukitaka mwanao awe ganja man mpeleke uko
 
Ingawa ni jambo jema kwa serikali kutoa elimu bure ili kusaidia watoto watokao kaya maskini kupata elimu ya msingi lakini huu mpango unafaa kuangaliwa upya kwa sababu utekelezaji wake una hasara nyingi kuliko faida.

Hasara ya kwanza: Tangu kuanzishwa kwa sera ya elimu bure, serikali imeshindwa kuajiri walimu wa kutosha na hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa walimu hususani wa masomo ya sayansi mashuleni na hivyo kupelekea wanafunzi wengi kufeli masomo hayo katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Kadhalika, ukosefu wa walimu pia unachangia wanafunzi kukata tamaa ya kusoma baadhi ya masomo hasa ya sayansi na wengine huamua kuacha shule kabisa na kujichanganya mtaani. Hii yote ni kwasababu serikali inatumia gharama kubwa zaidi ya billions 20 kwa mwezi kuhudumia elimu bure na hivyo kupunguza kiwango cha bajeti cha kuajiri walimu wapya kwa mwaka.

Hasara ya pili: Kufuatia mpango wa elimu bure, upatikanaji wa vifaa muhimu vya kufundishia na kujifunzia kama vile vitabu, vifaa vya maabara na kemikali za kufanyia majaribio upatikanaji wake umekuwa sio wa kuridhisha na hivyo kufanya walimu pamoja na wanafunzi kujifunza katika mazingira magumu. Hii inaweza kuwa inachangiwa na ucheleweshaji wa kupeleka pesa za kuhudumia elimu bure katika baadhi ya halmashauri au bajeti kubwa kupelekwa kwenye ujenzi wa miundo mbinu ya shule na kusahau eneo muhimu la ununuzi wa vifaa vya kielimu.

Hasara ya tatu: Serikali inatumia gharama kubwa kulipia wanafunzi ada ambao saa nyingine huamua kuacha ama kufukuzwa shule na hivyo kufanya serikali kuingia katika gharama zisizokuwa na msingi.

Hasara ya nne: pamoja na serikali kutoa elimu bure bado kuna changamoto ya madawati na hivyo kupelekea wanafunzi kusoma katika mazingira duni ya kukaa chini hasa katika vipindi vya darasani.

Hasara ya tano: Tangu serikali ianze kutoa elimu bila malipo kumekuwepo na ufuatiliaji mdogo wa wazazi kuhusu maendeleo ya watoto wao(wanafunzi). Hali hii inachangia kushusha kiwango cha taaluma mashuleni kwakuwa ufuatilaji wa maendeleo ya wanafunzi kwa asilimia kubwa umekuwa ukifanywa na walimu pekee. Katika hili, wazazi wamejiweka kando kutokana na kwamba hakuna hasara yoyote wanayopata kwakuwa gharama zote zinalipwa na serikali.

Hasara ya sita: Elimu bure imechangia kudumaza ushiriki wa wazazi katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo. Mfano, ushiriki katika ujenzi wa shule, ushiriki katika upanuzi na ujenzi wa madarasa. Linapotokea suala la kuchangia shughuli kama hizo wazazi wamekuwa wagumu wa kuchangia huku wakidai ni elimu bure hivyo hatutakiwi kuchanga chochote.

Kufuatia hasara hizo na zingine ambazo hazijatajwa, napendekeza elimu bure ifutwe badala yake wazazi waendelee kulipa ada na serikali ifanye yafuatato:

1. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kununua na kuhakikisha kuna vifaa vya kutosha vya kielimu mashuleni.

2. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kuhakikisha kuwa kuna upatikanaji wa madawati ya kutosha mashuleni ili watoto wasiendelee kukaa chini.

3. Serikali itumie bajeti ya elimu bure kuajiri walimu wa kutosha mashuleni ili kuinua kiwango cha taaluma katika sekta ya elimu.

4. Utekelezaji wa elimu bila malipo uanze baada ya changamoto zote kwenye sekta ya elimu hususani mashuleni kufanyiwa kazi.

5. Hakuna haja ya elimu bure kwakuwa wazazi wanao uwezo wa kusomesha watoto wao lakini hawana uwezo wa kuwaajiri katika ujira wa kudumu. Hivyo ipo haja ya bajeti ya elimu bure kutumika kuangazia kutoa fursa za ajira kwa vijana.

6. Kama kuna umuhimu wa Sera ya elimu bure kuendelea kuwepo basi ihamishiwe katika ngazi ya elimu ya juu(vyuo vikuu) kwakuwa ndiko kwenye gharama kubwa kuliko huku chini ambako mzazi anaweza kupambana kwa biashara ya kuuza ubuyu, karanga au kilimo cha bustani na kumsomesha mwanae.
Kumbe huko kwenu bado kuna elimu bure?!
Sisi huku wazazi wametangaziwa mchango wa kila mzazi pesa ya kujenga madarasa, vyoo vya waalimu na wamepewa week moja kila mzazi awe amemaliza kulipa vinginevyo mtoto wako akitoka likizo aje na mazazi.!
Sasa hapo kuna elimu ya bure tena?
 
Ingawa ni jambo jema kwa serikali kutoa elimu bure ili kusaidia watoto watokao kaya maskini kupata elimu ya msingi lakini huu mpango unafaa kuangaliwa upya kwa sababu utekelezaji wake una hasara nyingi kuliko faida.

Hasara ya kwanza: Tangu kuanzishwa kwa sera ya elimu bure, serikali imeshindwa kuajiri walimu wa kutosha na hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa walimu hususani wa masomo ya sayansi mashuleni na hivyo kupelekea wanafunzi wengi kufeli masomo hayo katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Kadhalika, ukosefu wa walimu pia unachangia wanafunzi kukata tamaa ya kusoma baadhi ya masomo hasa ya sayansi na wengine huamua kuacha shule kabisa na kujichanganya mtaani. Hii yote ni kwasababu serikali inatumia gharama kubwa zaidi ya billions 20 kwa mwezi kuhudumia elimu bure na hivyo kupunguza kiwango cha bajeti cha kuajiri walimu wapya kwa mwaka.

Hasara ya pili: Kufuatia mpango wa elimu bure, upatikanaji wa vifaa muhimu vya kufundishia na kujifunzia kama vile vitabu, vifaa vya maabara na kemikali za kufanyia majaribio upatikanaji wake umekuwa sio wa kuridhisha na hivyo kufanya walimu pamoja na wanafunzi kujifunza katika mazingira magumu. Hii inaweza kuwa inachangiwa na ucheleweshaji wa kupeleka pesa za kuhudumia elimu bure katika baadhi ya halmashauri au bajeti kubwa kupelekwa kwenye ujenzi wa miundo mbinu ya shule na kusahau eneo muhimu la ununuzi wa vifaa vya kielimu.

Hasara ya tatu: Serikali inatumia gharama kubwa kulipia wanafunzi ada ambao saa nyingine huamua kuacha ama kufukuzwa shule na hivyo kufanya serikali kuingia katika gharama zisizokuwa na msingi.

Hasara ya nne: pamoja na serikali kutoa elimu bure bado kuna changamoto ya madawati na hivyo kupelekea wanafunzi kusoma katika mazingira duni ya kukaa chini hasa katika vipindi vya darasani.

Hasara ya tano: Tangu serikali ianze kutoa elimu bila malipo kumekuwepo na ufuatiliaji mdogo wa wazazi kuhusu maendeleo ya watoto wao(wanafunzi). Hali hii inachangia kushusha kiwango cha taaluma mashuleni kwakuwa ufuatilaji wa maendeleo ya wanafunzi kwa asilimia kubwa umekuwa ukifanywa na walimu pekee. Katika hili, wazazi wamejiweka kando kutokana na kwamba hakuna hasara yoyote wanayopata kwakuwa gharama zote zinalipwa na serikali.

Hasara ya sita: Elimu bure imechangia kudumaza ushiriki wa wazazi katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo. Mfano, ushiriki katika ujenzi wa shule, ushiriki katika upanuzi na ujenzi wa madarasa. Linapotokea suala la kuchangia shughuli kama hizo wazazi wamekuwa wagumu wa kuchangia huku wakidai ni elimu bure hivyo hatutakiwi kuchanga chochote.

Kufuatia hasara hizo na zingine ambazo hazijatajwa, napendekeza elimu bure ifutwe badala yake wazazi waendelee kulipa ada na serikali ifanye yafuatato:

1. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kununua na kuhakikisha kuna vifaa vya kutosha vya kielimu mashuleni.

2. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kuhakikisha kuwa kuna upatikanaji wa madawati ya kutosha mashuleni ili watoto wasiendelee kukaa chini.

3. Serikali itumie bajeti ya elimu bure kuajiri walimu wa kutosha mashuleni ili kuinua kiwango cha taaluma katika sekta ya elimu.

4. Utekelezaji wa elimu bila malipo uanze baada ya changamoto zote kwenye sekta ya elimu hususani mashuleni kufanyiwa kazi.

5. Hakuna haja ya elimu bure kwakuwa wazazi wanao uwezo wa kusomesha watoto wao lakini hawana uwezo wa kuwaajiri katika ujira wa kudumu. Hivyo ipo haja ya bajeti ya elimu bure kutumika kuangazia kutoa fursa za ajira kwa vijana.

6. Kama kuna umuhimu wa Sera ya elimu bure kuendelea kuwepo basi ihamishiwe katika ngazi ya elimu ya juu(vyuo vikuu) kwakuwa ndiko kwenye gharama kubwa kuliko huku chini ambako mzazi anaweza kupambana kwa biashara ya kuuza ubuyu, karanga au kilimo cha bustani na kumsomesha mwanae.
Ndugu,
1. Watoto kufeli masomo ya sayansi hiyo imekuwepo tangia zamani, hawajawahi kufaulu, sasa elimu bure imehusikaje?
2. Hela ya vifaa vya maabara hupelekwa mashuleni kila mwezi, kama shule hazinunui mkawaulize pesa wanapeleka wapi.

3. Changamoto ya madawati ipo tu maana kila mwaka wanafunzi wanaongezeka.

4. Kufuatilia maendeleo ya mwanafunzi ni jukumu la mzazi na ni wajibu wake, wazazi wakishindwa sio kosa la serikali, ni uzembe wao.
 
Ndugu,
1. Watoto kufeli masomo ya sayansi hiyo imekuwepo tangia zamani, hawajawahi kufaulu, sasa elimu bure imehusikaje?
2. Hela ya vifaa vya maabara hupelekwa mashuleni kila mwezi, kama shule hazinunui mkawaulize pesa wanapeleka wapi.

3. Changamoto ya madawati ipo tu maana kila mwaka wanafunzi wanaongezeka.

4. Kufuatilia maendeleo ya mwanafunzi ni jukumu la mzazi na ni wajibu wake, wazazi wakishindwa sio kosa la serikali, ni uzembe wao.
Wazaz wktoa pesa wnkua wachungu na pesa hvo hufatilia mwenendo w mtoto saiz hkuna mweny hbr hiyo kw sbb ya elimu bure

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Ingawa ni jambo jema kwa serikali kutoa elimu bure ili kusaidia watoto watokao kaya maskini kupata elimu ya msingi lakini huu mpango unafaa kuangaliwa upya kwa sababu utekelezaji wake una hasara nyingi kuliko faida.

Hasara ya kwanza: Tangu kuanzishwa kwa sera ya elimu bure, serikali imeshindwa kuajiri walimu wa kutosha na hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa walimu hususani wa masomo ya sayansi mashuleni na hivyo kupelekea wanafunzi wengi kufeli masomo hayo katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Kadhalika, ukosefu wa walimu pia unachangia wanafunzi kukata tamaa ya kusoma baadhi ya masomo hasa ya sayansi na wengine huamua kuacha shule kabisa na kujichanganya mtaani. Hii yote ni kwasababu serikali inatumia gharama kubwa zaidi ya billions 20 kwa mwezi kuhudumia elimu bure na hivyo kupunguza kiwango cha bajeti cha kuajiri walimu wapya kwa mwaka.

Hasara ya pili: Kufuatia mpango wa elimu bure, upatikanaji wa vifaa muhimu vya kufundishia na kujifunzia kama vile vitabu, vifaa vya maabara na kemikali za kufanyia majaribio upatikanaji wake umekuwa sio wa kuridhisha na hivyo kufanya walimu pamoja na wanafunzi kujifunza katika mazingira magumu. Hii inaweza kuwa inachangiwa na ucheleweshaji wa kupeleka pesa za kuhudumia elimu bure katika baadhi ya halmashauri au bajeti kubwa kupelekwa kwenye ujenzi wa miundo mbinu ya shule na kusahau eneo muhimu la ununuzi wa vifaa vya kielimu.

Hasara ya tatu: Serikali inatumia gharama kubwa kulipia wanafunzi ada ambao saa nyingine huamua kuacha ama kufukuzwa shule na hivyo kufanya serikali kuingia katika gharama zisizokuwa na msingi.

Hasara ya nne: pamoja na serikali kutoa elimu bure bado kuna changamoto ya madawati na hivyo kupelekea wanafunzi kusoma katika mazingira duni ya kukaa chini hasa katika vipindi vya darasani.

Hasara ya tano: Tangu serikali ianze kutoa elimu bila malipo kumekuwepo na ufuatiliaji mdogo wa wazazi kuhusu maendeleo ya watoto wao(wanafunzi). Hali hii inachangia kushusha kiwango cha taaluma mashuleni kwakuwa ufuatilaji wa maendeleo ya wanafunzi kwa asilimia kubwa umekuwa ukifanywa na walimu pekee. Katika hili, wazazi wamejiweka kando kutokana na kwamba hakuna hasara yoyote wanayopata kwakuwa gharama zote zinalipwa na serikali.

Hasara ya sita: Elimu bure imechangia kudumaza ushiriki wa wazazi katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo. Mfano, ushiriki katika ujenzi wa shule, ushiriki katika upanuzi na ujenzi wa madarasa. Linapotokea suala la kuchangia shughuli kama hizo wazazi wamekuwa wagumu wa kuchangia huku wakidai ni elimu bure hivyo hatutakiwi kuchanga chochote.

Kufuatia hasara hizo na zingine ambazo hazijatajwa, napendekeza elimu bure ifutwe badala yake wazazi waendelee kulipa ada na serikali ifanye yafuatato:

1. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kununua na kuhakikisha kuna vifaa vya kutosha vya kielimu mashuleni.

2. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kuhakikisha kuwa kuna upatikanaji wa madawati ya kutosha mashuleni ili watoto wasiendelee kukaa chini.

3. Serikali itumie bajeti ya elimu bure kuajiri walimu wa kutosha mashuleni ili kuinua kiwango cha taaluma katika sekta ya elimu.

4. Utekelezaji wa elimu bila malipo uanze baada ya changamoto zote kwenye sekta ya elimu hususani mashuleni kufanyiwa kazi.

5. Hakuna haja ya elimu bure kwakuwa wazazi wanao uwezo wa kusomesha watoto wao lakini hawana uwezo wa kuwaajiri katika ujira wa kudumu. Hivyo ipo haja ya bajeti ya elimu bure kutumika kuangazia kutoa fursa za ajira kwa vijana.

6. Kama kuna umuhimu wa Sera ya elimu bure kuendelea kuwepo basi ihamishiwe katika ngazi ya elimu ya juu(vyuo vikuu) kwakuwa ndiko kwenye gharama kubwa kuliko huku chini ambako mzazi anaweza kupambana kwa biashara ya kuuza ubuyu, karanga au kilimo cha bustani na kumsomesha mwanae.
Critical thinking,big up.
 
Ndugu,
1. Watoto kufeli masomo ya sayansi hiyo imekuwepo tangia zamani, hawajawahi kufaulu, sasa elimu bure imehusikaje?
2. Hela ya vifaa vya maabara hupelekwa mashuleni kila mwezi, kama shule hazinunui mkawaulize pesa wanapeleka wapi.

3. Changamoto ya madawati ipo tu maana kila mwaka wanafunzi wanaongezeka.

4. Kufuatilia maendeleo ya mwanafunzi ni jukumu la mzazi na ni wajibu wake, wazazi wakishindwa sio kosa la serikali, ni uzembe wao
Haya majibu ni mepesi sana.Kwa hiyo hakuna umhimu wa kuongeza ufaulu kwenye masomo ya sayansi,na pia kuondoa uhaba wa madawati???? What's this!!!
 
Serikali iliiga sera ya chadema kutoa elimu bure kwa kukurupuka kwa hili nakuuunga mkono mana serikali inagharamia elimu ambayo haiwasaidi watoto kujikomboa wanafunz wengi wanaishia kidato cha nne na tano wameishia kusoma mambo mengi lakini hayawezi kuwasaidia
So sera ya chadema ilikuwa changa la macho
 
Walikurupika, hawakujiandaa kikamilfu kutekeleza hii sera.
Unaikana sera yako na lowasa wako .huna akili kabisa kama umeanza kikengeuka wazo la kusema jpm anatekeleza ilani yenu imeishia wap
 
Haya majibu ni mepesi sana.Kwa hiyo hakuna umhimu wa kuongeza ufaulu kwenye masomo ya sayansi,na pia kuondoa uhaba wa madawati???? What's this!!!
Soma mada vizuri na uangalie nilichojibu, acha kukurupuka.
 
No retreat no surrender huyo ndio big boss
Kikwete alijaribu kwa kufuta ada za mitihani ya kidato cha pili na nne lakini alivyoona serikali inaingia gharama kubwa aliamua kufuta huo mpango. Naamini hata huu mpango utafutwa tu kama sio kipindi hiki basi kipindi kijacho.
 
Ingawa ni jambo jema kwa serikali kutoa elimu bure ili kusaidia watoto watokao kaya maskini kupata elimu ya msingi lakini huu mpango unafaa kuangaliwa upya kwa sababu utekelezaji wake una hasara nyingi kuliko faida.

Hasara ya kwanza: Tangu kuanzishwa kwa sera ya elimu bure, serikali imeshindwa kuajiri walimu wa kutosha na hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa walimu hususani wa masomo ya sayansi mashuleni na hivyo kupelekea wanafunzi wengi kufeli masomo hayo katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Kadhalika, ukosefu wa walimu pia unachangia wanafunzi kukata tamaa ya kusoma baadhi ya masomo hasa ya sayansi na wengine huamua kuacha shule kabisa na kujichanganya mtaani. Hii yote ni kwasababu serikali inatumia gharama kubwa zaidi ya billions 20 kwa mwezi kuhudumia elimu bure na hivyo kupunguza kiwango cha bajeti cha kuajiri walimu wapya kwa mwaka.

Hasara ya pili: Kufuatia mpango wa elimu bure, upatikanaji wa vifaa muhimu vya kufundishia na kujifunzia kama vile vitabu, vifaa vya maabara na kemikali za kufanyia majaribio upatikanaji wake umekuwa sio wa kuridhisha na hivyo kufanya walimu pamoja na wanafunzi kujifunza katika mazingira magumu. Hii inaweza kuwa inachangiwa na ucheleweshaji wa kupeleka pesa za kuhudumia elimu bure katika baadhi ya halmashauri au bajeti kubwa kupelekwa kwenye ujenzi wa miundo mbinu ya shule na kusahau eneo muhimu la ununuzi wa vifaa vya kielimu.

Hasara ya tatu: Serikali inatumia gharama kubwa kulipia wanafunzi ada ambao saa nyingine huamua kuacha ama kufukuzwa shule na hivyo kufanya serikali kuingia katika gharama zisizokuwa na msingi.

Hasara ya nne: pamoja na serikali kutoa elimu bure bado kuna changamoto ya madawati na hivyo kupelekea wanafunzi kusoma katika mazingira duni ya kukaa chini hasa katika vipindi vya darasani.

Hasara ya tano: Tangu serikali ianze kutoa elimu bila malipo kumekuwepo na ufuatiliaji mdogo wa wazazi kuhusu maendeleo ya watoto wao(wanafunzi). Hali hii inachangia kushusha kiwango cha taaluma mashuleni kwakuwa ufuatilaji wa maendeleo ya wanafunzi kwa asilimia kubwa umekuwa ukifanywa na walimu pekee. Katika hili, wazazi wamejiweka kando kutokana na kwamba hakuna hasara yoyote wanayopata kwakuwa gharama zote zinalipwa na serikali.

Hasara ya sita: Elimu bure imechangia kudumaza ushiriki wa wazazi katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo. Mfano, ushiriki katika ujenzi wa shule, ushiriki katika upanuzi na ujenzi wa madarasa. Linapotokea suala la kuchangia shughuli kama hizo wazazi wamekuwa wagumu wa kuchangia huku wakidai ni elimu bure hivyo hatutakiwi kuchanga chochote.

Kufuatia hasara hizo na zingine ambazo hazijatajwa, napendekeza elimu bure ifutwe badala yake wazazi waendelee kulipa ada na serikali ifanye yafuatato:

1. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kununua na kuhakikisha kuna vifaa vya kutosha vya kielimu mashuleni.

2. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kuhakikisha kuwa kuna upatikanaji wa madawati ya kutosha mashuleni ili watoto wasiendelee kukaa chini.

3. Serikali itumie bajeti ya elimu bure kuajiri walimu wa kutosha mashuleni ili kuinua kiwango cha taaluma katika sekta ya elimu.

4. Utekelezaji wa elimu bila malipo uanze baada ya changamoto zote kwenye sekta ya elimu hususani mashuleni kufanyiwa kazi.

5. Hakuna haja ya elimu bure kwakuwa wazazi wanao uwezo wa kusomesha watoto wao lakini hawana uwezo wa kuwaajiri katika ujira wa kudumu. Hivyo ipo haja ya bajeti ya elimu bure kutumika kuangazia kutoa fursa za ajira kwa vijana.

6. Kama kuna umuhimu wa Sera ya elimu bure kuendelea kuwepo basi ihamishiwe katika ngazi ya elimu ya juu(vyuo vikuu) kwakuwa ndiko kwenye gharama kubwa kuliko huku chini ambako mzazi anaweza kupambana kwa biashara ya kuuza ubuyu, karanga au kilimo cha bustani na kumsomesha mwanae.
Njoo na Statistical evidence za kabla ya elimu bila malipo na baada ya elimu bila malipo kwa kila changamoto uliyotaja hapo juu ili tuweze kuamini ulichoandika, tofauti na hapo tutajua umetumwa na chadema. provide statistical facts za before and after na utoe statistical proof by using any statistical test kama tunaweza kukubaliana na ushauri wako.
 
Ingawa ni jambo jema kwa serikali kutoa elimu bure ili kusaidia watoto watokao kaya maskini kupata elimu ya msingi lakini huu mpango unafaa kuangaliwa upya kwa sababu utekelezaji wake una hasara nyingi kuliko faida.

Hasara ya kwanza: Tangu kuanzishwa kwa sera ya elimu bure, serikali imeshindwa kuajiri walimu wa kutosha na hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa walimu hususani wa masomo ya sayansi mashuleni na hivyo kupelekea wanafunzi wengi kufeli masomo hayo katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Kadhalika, ukosefu wa walimu pia unachangia wanafunzi kukata tamaa ya kusoma baadhi ya masomo hasa ya sayansi na wengine huamua kuacha shule kabisa na kujichanganya mtaani. Hii yote ni kwasababu serikali inatumia gharama kubwa zaidi ya billions 20 kwa mwezi kuhudumia elimu bure na hivyo kupunguza kiwango cha bajeti cha kuajiri walimu wapya kwa mwaka.

Hasara ya pili: Kufuatia mpango wa elimu bure, upatikanaji wa vifaa muhimu vya kufundishia na kujifunzia kama vile vitabu, vifaa vya maabara na kemikali za kufanyia majaribio upatikanaji wake umekuwa sio wa kuridhisha na hivyo kufanya walimu pamoja na wanafunzi kujifunza katika mazingira magumu. Hii inaweza kuwa inachangiwa na ucheleweshaji wa kupeleka pesa za kuhudumia elimu bure katika baadhi ya halmashauri au bajeti kubwa kupelekwa kwenye ujenzi wa miundo mbinu ya shule na kusahau eneo muhimu la ununuzi wa vifaa vya kielimu.

Hasara ya tatu: Serikali inatumia gharama kubwa kulipia wanafunzi ada ambao saa nyingine huamua kuacha ama kufukuzwa shule na hivyo kufanya serikali kuingia katika gharama zisizokuwa na msingi.

Hasara ya nne: pamoja na serikali kutoa elimu bure bado kuna changamoto ya madawati na hivyo kupelekea wanafunzi kusoma katika mazingira duni ya kukaa chini hasa katika vipindi vya darasani.

Hasara ya tano: Tangu serikali ianze kutoa elimu bila malipo kumekuwepo na ufuatiliaji mdogo wa wazazi kuhusu maendeleo ya watoto wao(wanafunzi). Hali hii inachangia kushusha kiwango cha taaluma mashuleni kwakuwa ufuatilaji wa maendeleo ya wanafunzi kwa asilimia kubwa umekuwa ukifanywa na walimu pekee. Katika hili, wazazi wamejiweka kando kutokana na kwamba hakuna hasara yoyote wanayopata kwakuwa gharama zote zinalipwa na serikali.

Hasara ya sita: Elimu bure imechangia kudumaza ushiriki wa wazazi katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo. Mfano, ushiriki katika ujenzi wa shule, ushiriki katika upanuzi na ujenzi wa madarasa. Linapotokea suala la kuchangia shughuli kama hizo wazazi wamekuwa wagumu wa kuchangia huku wakidai ni elimu bure hivyo hatutakiwi kuchanga chochote.

Kufuatia hasara hizo na zingine ambazo hazijatajwa, napendekeza elimu bure ifutwe badala yake wazazi waendelee kulipa ada na serikali ifanye yafuatato:

1. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kununua na kuhakikisha kuna vifaa vya kutosha vya kielimu mashuleni.

2. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kuhakikisha kuwa kuna upatikanaji wa madawati ya kutosha mashuleni ili watoto wasiendelee kukaa chini.

3. Serikali itumie bajeti ya elimu bure kuajiri walimu wa kutosha mashuleni ili kuinua kiwango cha taaluma katika sekta ya elimu.

4. Utekelezaji wa elimu bila malipo uanze baada ya changamoto zote kwenye sekta ya elimu hususani mashuleni kufanyiwa kazi.

5. Hakuna haja ya elimu bure kwakuwa wazazi wanao uwezo wa kusomesha watoto wao lakini hawana uwezo wa kuwaajiri katika ujira wa kudumu. Hivyo ipo haja ya bajeti ya elimu bure kutumika kuangazia kutoa fursa za ajira kwa vijana.

6. Kama kuna umuhimu wa Sera ya elimu bure kuendelea kuwepo basi ihamishiwe katika ngazi ya elimu ya juu(vyuo vikuu) kwakuwa ndiko kwenye gharama kubwa kuliko huku chini ambako mzazi anaweza kupambana kwa biashara ya kuuza ubuyu, karanga au kilimo cha bustani na kumsomesha mwanae.
Wazo zuri.Tatizo ni mapokeo.Je,wenye mamlaka watasikiliza????
Tangu "Elimu bure" ianzishwe(kinadharia)",imekuwa mtaji kisiasa.Sidhani kama watakubali kuupoteza.

Pia si kweli kuwa elimu ni bure kwani tuna watoto katika shule tofauti na kila shule ina taratibu za michango ambayo ukijumlisha kwa mwaka ni zaidi ya karo ya 20,000 na 70,000 !(shule za serikali.

Na kuwa siasa kutawala nyanja zingine(utaalamu/taaluma) ndiyo chimbuko la mapungufu yote haya.Unakuta Mkuu wa Wilaya/Mkoa anaagiza kukamatwa na kuwekwa mahabusu "mtendaji" kwa tuhuma (ambazo hazijathibitishwa) na hivyo kushusha ari ya kazi na ubunifu. Tangu mtindo huu utamalaki sijasikia yeyote aliyewahi kutumbuliwa na DC/RC kachukuliwa hatua zaidi kwa maovu aliyotenda.(Niko radhi kukosolewa).

Itoshe kusema kuwa ili tusonge mbele,mifumo mbali mbali inayoongoza Taifa letu ibadilishwe.Kwa kuanza na mitaala ya Elimu,uendeshaji wa Taasisi za Elimu,Utawala/siasa kutoingilia(bila sababu za msingi), kuheshimu taaluma na mipaka ya kazi na jamii kufunguka.
 
Ingawa ni jambo jema kwa serikali kutoa elimu bure ili kusaidia watoto watokao kaya maskini kupata elimu ya msingi lakini huu mpango unafaa kuangaliwa upya kwa sababu utekelezaji wake una hasara nyingi kuliko faida.

Hasara ya kwanza: Tangu kuanzishwa kwa sera ya elimu bure, serikali imeshindwa kuajiri walimu wa kutosha na hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa walimu hususani wa masomo ya sayansi mashuleni na hivyo kupelekea wanafunzi wengi kufeli masomo hayo katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Kadhalika, ukosefu wa walimu pia unachangia wanafunzi kukata tamaa ya kusoma baadhi ya masomo hasa ya sayansi na wengine huamua kuacha shule kabisa na kujichanganya mtaani. Hii yote ni kwasababu serikali inatumia gharama kubwa zaidi ya billions 20 kwa mwezi kuhudumia elimu bure na hivyo kupunguza kiwango cha bajeti cha kuajiri walimu wapya kwa mwaka.

Hasara ya pili: Kufuatia mpango wa elimu bure, upatikanaji wa vifaa muhimu vya kufundishia na kujifunzia kama vile vitabu, vifaa vya maabara na kemikali za kufanyia majaribio upatikanaji wake umekuwa sio wa kuridhisha na hivyo kufanya walimu pamoja na wanafunzi kujifunza katika mazingira magumu. Hii inaweza kuwa inachangiwa na ucheleweshaji wa kupeleka pesa za kuhudumia elimu bure katika baadhi ya halmashauri au bajeti kubwa kupelekwa kwenye ujenzi wa miundo mbinu ya shule na kusahau eneo muhimu la ununuzi wa vifaa vya kielimu.

Hasara ya tatu: Serikali inatumia gharama kubwa kulipia wanafunzi ada ambao saa nyingine huamua kuacha ama kufukuzwa shule na hivyo kufanya serikali kuingia katika gharama zisizokuwa na msingi.

Hasara ya nne: pamoja na serikali kutoa elimu bure bado kuna changamoto ya madawati na hivyo kupelekea wanafunzi kusoma katika mazingira duni ya kukaa chini hasa katika vipindi vya darasani.

Hasara ya tano: Tangu serikali ianze kutoa elimu bila malipo kumekuwepo na ufuatiliaji mdogo wa wazazi kuhusu maendeleo ya watoto wao(wanafunzi). Hali hii inachangia kushusha kiwango cha taaluma mashuleni kwakuwa ufuatilaji wa maendeleo ya wanafunzi kwa asilimia kubwa umekuwa ukifanywa na walimu pekee. Katika hili, wazazi wamejiweka kando kutokana na kwamba hakuna hasara yoyote wanayopata kwakuwa gharama zote zinalipwa na serikali.

Hasara ya sita: Elimu bure imechangia kudumaza ushiriki wa wazazi katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo. Mfano, ushiriki katika ujenzi wa shule, ushiriki katika upanuzi na ujenzi wa madarasa. Linapotokea suala la kuchangia shughuli kama hizo wazazi wamekuwa wagumu wa kuchangia huku wakidai ni elimu bure hivyo hatutakiwi kuchanga chochote.

Kufuatia hasara hizo na zingine ambazo hazijatajwa, napendekeza elimu bure ifutwe badala yake wazazi waendelee kulipa ada na serikali ifanye yafuatato:

1. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kununua na kuhakikisha kuna vifaa vya kutosha vya kielimu mashuleni.

2. Serikali itumie bajeti ya kutoa elimu bure kuhakikisha kuwa kuna upatikanaji wa madawati ya kutosha mashuleni ili watoto wasiendelee kukaa chini.

3. Serikali itumie bajeti ya elimu bure kuajiri walimu wa kutosha mashuleni ili kuinua kiwango cha taaluma katika sekta ya elimu.

4. Utekelezaji wa elimu bila malipo uanze baada ya changamoto zote kwenye sekta ya elimu hususani mashuleni kufanyiwa kazi.

5. Hakuna haja ya elimu bure kwakuwa wazazi wanao uwezo wa kusomesha watoto wao lakini hawana uwezo wa kuwaajiri katika ujira wa kudumu. Hivyo ipo haja ya bajeti ya elimu bure kutumika kuangazia kutoa fursa za ajira kwa vijana.

6. Kama kuna umuhimu wa Sera ya elimu bure kuendelea kuwepo basi ihamishiwe katika ngazi ya elimu ya juu(vyuo vikuu) kwakuwa ndiko kwenye gharama kubwa kuliko huku chini ambako mzazi anaweza kupambana kwa biashara ya kuuza ubuyu, karanga au kilimo cha bustani na kumsomesha mwanae.
Kwakuwa watotowako na ndugu zako wrote wanasomea shule za kishua, ndio maana umeona shule wañazosomeshea wenyekipato kidogo nazo wasome kwa kulipia kwakuwa wewe na familia yako mnaweza kumduuu. Mkifanikiwa kifedha mbona mbona mjisahau kana kwamba mlizaliwa nazooo?? Kumbuka ulikotoka
 
Back
Top Bottom