SoC04 Serikali tusaidieni wasomi kwa kutekeleza mfumo huu

SoC04 Serikali tusaidieni wasomi kwa kutekeleza mfumo huu

Tanzania Tuitakayo competition threads
Joined
May 19, 2024
Posts
10
Reaction score
7
download-1.png

Chanzo: mtandaoni​

Tatizo la ajira ndugu wa Tanzania limekuwa janga kubwa sana kwa vijana waliohitimi vyuo mbali mbali nchini ,Serikali inajaribu kifanya juu chini kuweza kupunguza makali yake.Wahitimu wengi wamekuwa wakitapatapa kujikwamua kimaisha kwa kutafuta ajira pamoja na mitaji kwa ajiri ya kujiajiri lakini mambo yamekuwa magumu hata kupata hiyo motaji.

Mikopo imekuwa ya masharti magumu mno,waajiri wamekuwa na masharti mengi wakisisitiza uzoefu zaidi kwa waombaji hali inapelekea kukosa sifa je tumesoma tuzidishe idadi ya wategemezi?

Serekali ianzishe mkakati wa lazima kwa Taasisi na makampuni binafsi kutenga asilimia 20% za ajira za Muda

MFUMO

(WASOMI BOOST)

download.png

Chanzo: Mtandaonu​

Sheria hiyo itaruhusu na kuwataka wamiliki na waajiri wa Taasisi binafsi na serikali pamoja na makampuni yote ketenga 20% kwa ajili ya Ajira za muda kwa wahitimu

(1) Wahitimu waliotoka moja kwa moja vyuoni
(2)Ambao walishahitimu

UTEKELEZWAJI WA MFUMO

Serikali inatakiwa kupitia serikali mtandao kupitia Tamisemi kuanzisha mfumo wa maombi za ajira za muda ambapo kila kuhitimu ataomba kulingana na fakalti yake nakuomba pamoja na kupatiwa

Muda wa mkataba ya ajira hizo
Waajiri kupitia sheria hiyo elekezi watapaswa kuwaajiri na kuwapatia mkataba ya mwaka mmoja tu vijana waliopata nafasi

Maelekezo juu ya malipo na staiki zote kazini
Waajiri wanatakiwa kuwalipa waajiriwa hao wa muda 70% ya mshahara ila wafaidike na marupuru yote kama ilivyo kwa wengine.

Mfumo wa Malipo na usimamizi wake kulingana na Lengo la Mkakati wa Boost
Mkakati huu ifahamike ni kwa ajili ya kuondoa kabisa 80% kwa wasomi juu ya Ajira za moja kwa Moja na kuzingatia wasomi kujiajiri wenyewe.
(1) Malipo yote ya mradi wa Boost yatalipwa kupitia Bank ya serikali chini ya mfumo wa Boost ambapo.
Waajiriwa hao watapewa 40% ya basic salary zao pamoja na makusanyo ya posho zote.

Mwisho wa mkataba
Serikali itawalipa 60% ya mishahara Yao

MKAKATI ENDELEVU NA FUATILIVU WA BOOST
Serikali miezi mitatu kabla ya kuisha kwa mikataba ya ajira wa Boost wasomi ikusanye taarifa hizi
(1) Ni waajiriwa wangapi waajiri wamependa kubaki nao
(2) Waajiriwa ambao watamaliza mkataba Wana penda kujiajiri katika kitu gani

Mkakati Saidizi ya elimu na mafunzo ya fursa na kujuajiri kwa mfumo wa Boost wasomi

Serikali na wadau mbali mbali watawapatia vijana hao elimu na kuwafungulia Fursa mbali mbali vijana wa Wasomi Boost.

Mkakati saidizi
Serikali kupitia mfumo maalum ambao utaanzishwa utatakiwa kuwa weka kimakundi kulingana na mkoa waliopo vijana hao.

Kwa kutengenezea uwezo wa kuanzisha viwanda vidogo vidogo kupitia 60% ya ile akiba ya Wasomi Boost
Kuanzia Kilimo,Usafirishaji, Uvuvi,Huduma za fedha,n.k.

USIMAMIZI JUU YA UENDELEVU WAKE
Serikali kupitia Watendaji na maafisa maendeleo ya kata wataratibu maendeleo ya miradi hiyo ngazi ya kata pamoja na wadau wengine.

FAIDA. YA MRADI WA BOOST WASOMI
1.Kuondoa utegemezi wa ajira serikalini na taasisi binafsi
2.kuanzishwa kwa wingi viwanda na wasomi
3.Serikali kuweza kurudisha kikamilifu marejesho ya mikopo ya elimu ya juu na wengine kunufaika zaidi
4.kuongezeka kwa ajira nyingi kutokana na miradi inayo anzishwa
5.Serikali kuaminika na kupendwa
6.Kupunguza matatizo ya afya ya akili kwa wasomi


Nahitimisha wasomi ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu ya taifa tuwajali na tuwaonyeshe upendo huu kama alama ya kuwa jali na hii ndio TANZANIA TUNAYO ITAKA.
 
Upvote 3
Muda wa mkataba ya ajira hizo
Waajiri kupitia sheria hiyo elekezi watapaswa kuwaajiri na kuwapatia mkataba ya mwaka mmoja tu vijana waliopata nafasi

Maelekezo juu ya malipo na staiki zote kazini
Waajiri wanatakiwa kuwalipa waajiriwa hao wa muda 70% ya mshahara ila wafaidike na marupuru yote kama ilivyo kwa wengine
Ili wapatepo kamtaji sio nzuri.

(1) Wahitimu waliotoka moja kwa moja vyuoni
(2)Ambao walishahitimu
Japo kwa hapa mi nnapendekeza wawe wale ambao angalau wametimiza mwaka mmoja baada ya kuhitimu, wametimiza mwaka mmoja wa kutangatanga kutafuta ajira.
Au basi iwe baada ya kuipata ajira hataruhusiwa kuajiriwa tena hizo ajira za muda hadi upite mwaka mmoja mtupu.

Tunataka balansi yake iwepo ili kweli wahitimu wafanyie kazi mitaji na pesa wanazojisevia wakati wa ajira. Itakuwa bonge moja la elimu kwa vitendo.
Waajiriwa hao watapewa 40% ya basic salary zao pamoja na makusanyo ya posho zote.

Mwisho wa mkataba
Serikali itawalipa 60% ya mishahara Yao
Swali kidogo, je ni lini hao wahitimu watajifunza kujisimamia wenyewe.?? Maana tunataka taifa lenye wasomi wanaowajibika kwanza kwa matendo yao na pia kwa jamii kiujumla??
 
Ili wapatepo kamtaji sio nzuri.


Japo kwa hapa mi nnapendekeza wawe wale ambao angalau wametimiza mwaka mmoja baada ya kuhitimu, wametimiza mwaka mmoja wa kutangatanga kutafuta ajira.
Au basi iwe baada ya kuipata ajira hataruhusiwa kuajiriwa tena hizo ajira za muda hadi upite mwaka mmoja mtupu.

Tunataka balansi yake iwepo ili kweli wahitimu wafanyie kazi mitaji na pesa wanazojisevia wakati wa ajira. Itakuwa bonge moja la elimu kwa vitendo.

Swali kidogo, je ni lini hao wahitimu watajifunza kujisimamia wenyewe.?? Maana tu ataka taifa kenye wasomi wanaowajibika kwanza kwa matendo yao na pia kwa jamii kiujumla??
Ok kidogo hapo tunaweza rekebisha
 
Back
Top Bottom