Serikali/ Wizara ya Elimu tafuteni waalimu wa Kiingereza kutoka Uingereza

Serikali/ Wizara ya Elimu tafuteni waalimu wa Kiingereza kutoka Uingereza

Kidagaa kimemwozea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
3,680
Reaction score
6,554
Watanzania wote hatujui Kiingereza katika viwango vya 3.5-4 hii ni kutokana na kukaririshwa zaidi sarufi ya Kiingereza kuliko lugha yenyewe/mawasiliano.

Serikali inapaswa kugharamia waalimu wageni ambao watakuja kufundisha lugha ya kingereza kwa ufasaha ambapo watatumia mbinu za ufundishaji wa lugha ya kigeni.

Aidha syllabus ya kufundisha somo la kingereza ubadilishwe ili ilenge kumwezesha mwanafunzi kuzungumza Kiingereza kuliko kuijua sarufi ya kingereza. Hoja hii inapwewa mashiko na wataalam kama Martha Qorro ma na prof. F.E.M. K . senkorro.

Hakuna haja ya kuendelea kufundisha tena Kingereza kama somo la history au biology badala yake Kiingereza kifundishwe kama lugha kwa kutumia mbinu za kufundisha lugha ya kigeni.

Hii itasaidia kupata Watanzania wanaojua kingereza kuliko hawa tulionao wanaodhani wanajua Ila kiuhalisia ukiwasikiliza wakiongea wanaongea kama Kitabu, lugha ya kiuandishi. Aka Kingereza cha kitabuni.

Rai yangu ni kuwa serikali tafuteni waalimu wa kingereza wazawa wa lugha yenyewe kwaajili ya kufundisha Watanzania lugha ya Kingereza.
 
Wewe unaongea kiswahili lakini Kiswahili hujui, kuwa muinglishi haimaanishi unajua kiingilishi
 
Alichosema huyo Prof ni kweli wtz hatujui hiyo lugha kwa ufasaha,ni lugha muhimu kuijua kama unataka kusoma nje au kufanya biashara
 
Malawi, Zambia, Zimbabwe, Uganda na Namibia nchi za SADC wanaweza kusaidia somo la Kiingereza kwa dharura wakati serikali ikijipanga kuwa waalimu wa kiTanzania wa mchepuo wa kiingereza na literature wapelekwe kusoma ktk nchi hizo tajwa za SADC.
 
Mwalimu anaekujibu swali moja kwa moja bila kuweka kibwagizo cha lugha ya mzungumzo huyo alikriri sarufi
 
Hapa mitaala ibadilishwe tu,kwa sababu kuleta waalimu kutoka uingereza hakuwezi kumfanya mtoto akajua kukiongea vizuri,mbona watoto wa international schools wanaongea vizuri bila kufundishwa na wazungu?

Kwanini shule zingine za serikali ni tofauti? tatizo liko wapi? mimi mwenyewe pamoja na kusoma sana tuition za kiingereza tangu shule ya msingi lakini bado kuunga sentensi fasaha katika mazungumzo siwezi
 
Hao waingereza wenyewe hawakijui Kingereza. Hapa unataka kutuaminisha kuwa Watanzania wote tunakijua Kiswahili kwakua ni lugha yetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ni mgumu sana kuelewa.Mleta mada anasema watu wafundishwe kuingea na soli kujua.Usifundishe grama,fundisha namna ya kutumia hio grama usifundishe tense, fundisha watu watumie huzi tense.Mimi ndivi nimeelewa
 
Hivi tatizo la watazania kiuchumi ni kutojua kingerexa.Halafu ukikijua hicho ki gereza utaongea na nani? Hao waliomaliza English medium hukiongea wapi na Mani ?.Jifunze kutatua matatizo sio kingereza.
Matatizo ya watanzania in kukosa
1.Competence
2.Confidence.
Sio lugha!.
Marne hii ya teknolojia ukimkuta MTU anailamu serikali ujue ana matatizo.Mfano you tube kuna the best English teacher lakini watu hawatumii hio you tube kujifunza, wanabaki kulaumu tu.Mnafikiri hizo teknolojia ziliwekwa kwa ajili ya kupakua muziki tu
 
Atakaye kwenda uingereza kuwaomba hao walimu atakua mdada fulani. Kazi itakua hao waingereza wasipotimixa wajibu wao. Utasikia akiwakaripia " you will sleep on the cell till all tanzanians talking english. You are not teach student? You will sleep on cell till Dodoma. Police catch the teacher of britain.
 
Tunaweza pia badili mfumo wa kutahini somo la kiingereza na Kiswahili au Languages kwa mfumo ufuatao:

Tutakuwa na mitihani mitatu (3) ya lugha.
1. Reading and writing (kama ifanyimayo sasa)

2.Listening exams ( hii unapewa question paper halafu unaskiliza mazungumzo / comprehension) unaskiliza then unajibu swali.
3. Speaking exams, hapa unahojiwa halafu unajibu na hiyo conversation inarekodiwa na kisahihishwa kwa kisikilizwa na jopo la wataalami/mtaalamu.

Hapa inasaidia mtoto kujua domains zote za lugha (listening, speaking, reading and writing)

Unakuta kwa mfumo wa NECTA mtu ana A ya kiingereza lakini hawezi kuwasiliana.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bongo wapo wanaojua kiingereza kizuri tu.

Binti yangu alipomaliza form six alitunikiwa hati ya kiingereza na geography, tena shule za st Nyerere.

Kwani watu kama hao hawawezi kuwa waalim wazuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo Muingereza mwenyewe hakijui hicho kiingereza ndugu yangu sasa sijui unataka tumpate wapi huyo mwalimu!!! Unataka tuende nacho wapi kwanza?? Tuendelee na hichi hichi cha Ndalichako kinatosha bora tu kiongezwe tamshi
 
Watanzania wote hatujui Kiingereza katika viwango vya 3.5-4 hii ni kutokana na kukaririshwa zaidi sarufi ya Kiingereza kuliko lugha yenyewe/mawasiliano.

Serikali inapaswa kugharamia waalimu wageni ambao watakuja kufundisha lugha ya kingereza kwa ufasaha ambapo watatumia mbinu za ufundishaji wa lugha ya kigeni.

Aidha syllabus ya kufundisha somo la kingereza ubadilishwe ili ilenge kumwezesha mwanafunzi kuzungumza Kiingereza kuliko kuijua sarufi ya kingereza. Hoja hii inapwewa mashiko na wataalam kama Martha Qorro ma na prof. F.E.M. K . senkorro.

Hakuna haja ya kuendelea kufundisha tena Kingereza kama somo la history au biology badala yake Kiingereza kifundishwe kama lugha kwa kutumia mbinu za kufundisha lugha ya kigeni.

Hii itasaidia kupata Watanzania wanaojua kingereza kuliko hawa tulionao wanaodhani wanajua Ila kiuhalisia ukiwasikiliza wakiongea wanaongea kama Kitabu, lugha ya kiuandishi. Aka Kingereza cha kitabuni.

Rai yangu ni kuwa serikali tafuteni waalimu wa kingereza wazawa wa lugha yenyewe kwaajili ya kufundisha Watanzania lugha ya Kingereza.
Hii haiwezi kutokea na tena jiwe akisikia hili anaweza hata akaamuru vijana wake wakupoteze. Yeye mwenyewe lugha inamsumbua sio rahisi akaruhusu.
 
Kazi kweli kweli.
Utajua-Mleta mada hii sio mwongeaji wa kiswahili. Soma vizuri tu,
Utajua-Mleta mada ni mshabiki wa waingereza eti serikali iingie gharama ya kuwaleta. Ebo!
Unaona ufinyu wa mleta mada wa kutojali azma ya "Mwafrika" kujikomboa kutoka ukoloni mamboleo.
Msomaji, Umuhimu wa kutambua lugha yako mama(iwe kizaramo, kikurya, kimakonde....nk ), kuwa ndio mkombozi wa elimu, ni kuendeleza, mila na desturi za mwafrika, na hivyo kujikomboa na utegemezi wa fikra kuwa Kiingereza au waingereza ndio watakukomboa. Moja yapo ya silaha ya ukoloni mamboleo ni kukufanya usahau lugha yako, mila na desturi nk hivyo basi, ukurupaji wa mleta mada hii haitaleta tija katika safari ya "Ukombozi"
Umehatarishwa.
Mleta mada. Mimi Jeuri. wacha hizo.
 
Kwanza lazima ujue mtu anajifunzaje lugha 1.Experience of language
2.Kitivo cha lugha(ubongo)
3.Universal language.
Sasa kama mtanzania anaexperience ya kiswahili 30%.ndio kiswahili ndio lugha mamma.Lakin 70% ya watanzania kiswahili ni lugha ya pili baada ya lugha za makabila,kwa hiyo kiingereza ni lugha ya 3.sasa Unataka mtu ambaye kwake lugha ya 3 iwe sawa na lugha mama.That's impossible.Cha kufanya tuhakjkishe watu wanajua kingereza kwa kiwango cha kawaida japo kujieleza kidogo(cha kuombea maji).sisi tujikite na lugha yetu ya kiswahili ambayo pia inatupiga chini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Natofautiana na wewe mleta mada kuhusu somo la Kiingereza.
Tofauti ya Tanzania na nchi nyingine za saddc ni kuwa nchi hizo zina lugha moja ya kikabila na lugha ya pili ni kiingereza,sisi tuna lugha za kikabila,kiswahili huwa lugha ya pili na Kiingereza huwa lugha ya tatu.
Hii hutufanya kukosa umahiri kwenye lugha ya tatu.Hebu fatilia watoto waliokulia mijini wanaosoma English media uone wanavyotiririka English.
Wengi wa product za English media hawajaingia kwenye soko la Ualimu.
By the way,kujua English kiufasaha ni ukoloni mamboleo.
Wafaransa,Wareno,Wajerumani Waskandinavia na sehemu kubwa ya Ulaya hawajui kiingereza kifasaha.
Mbrazil Marcio Maximo alikuwa hajui kiingereza kiufasaha lakini alielewana na wachezaji na Watanzania hadi kukubalika
na kufanikiwa kuisogeza Taifa stars hatua chache mbele.Sikiliza kiingereza cha Josee Mourinyo na yupo Uingereza anapiga mpunga, hana hiyo English ya 3.5.Prof Ndalichako hana hizo Point zenu za English lakini anakokotoa mahesabu ya hatari.Dr.John.....anachanganya kemikali bila shida huku akiwa labda na point 1 tu.
Nasisitiza tujiamini,tupo kwenye right truck,tupiganie tume huru tu
 
Back
Top Bottom