Serikali ya Irani itatekeleza hukumu ya kifo kwa watuhumiwa hawa 7 ambapo 2 wanauraia wa Uingereza?!

Raphael Thedomiri

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2019
Posts
442
Reaction score
729
Wakati dunia na hasa mataifa ya magharibi yakiendelea kulaani utekelezwaji wa hukumu ya kifo kwa waandamanaji 2 walionyongwa na serikali ya Irani hivi majuzi,

Taarifa iliyochapishwa na vyombo vya habari vya serikali ya Iran leo, imesema kikosi cha walinzi wa kimapinduzi nchini Iran Jumapili kimewakamata watu saba wenye uhusiano na Uingereza,wakiwemo baadhi ambao wana uraia pacha, kuhusiana na maandamano dhidi ya serikali ambayo yameitikisa nchi hiyo.

Ni yapi yanayoweza kutokea endapo mahakama yao itawakuta na hatia na kuwahukumu vifo? Ukizingatia na hali ya kidiplomasia iliyopo kati yao na mataifa ya magharibi!?

chanzo cha taarifa;
VOA
 
Yani ukiishi irani inabidi ukae kwa kutulia la sivyo wahuni wanapita na neck
 
Uzuri wa Iran hawacheki na ma kima.

Sheria zipo pale, ukileta za kuleta na ukakutwa na hatia, wanakunyonga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…