Serikali ya Rais Samia yaingia katika mtego wa Chadema kuwatumia Polisi kuandamana kwa niaba yao

Serikali ya Rais Samia yaingia katika mtego wa Chadema kuwatumia Polisi kuandamana kwa niaba yao

😅😅😅 POLISI leo wameandamana
Kumwamrisha Polisi akufanyie kitu ni rahisi sana! Kuna hadithi jamaa alitaka polisi wamlimie shamba. Akawatumia ujumbe kuna maiti wamezikwa kwneye shamba lake. Wacha polisi watimke kwenda kufukua na majembe kutafuta wapi wamezikwa - wakalima shamba lote jmaa kaja kupanda mbegu tu!

Leo Polisi wakaza buti kuandamana mitaani kwa niaba ya Chadema!
 
"Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema wanawashikilia watu 14, wakiwemo mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, Makamu Mwenyekiti-Bara, Tundu Lissu na mwenyekiti wa chama hicho kanda ya Kaskazini, Godbless Lema"

Polisi wanazidi kutangaza kampeni ya Chadema ya kuandamna!
 
Polisi wakiwa mitaani wakifanya maandano kufikisha ujumbe kwa jumuia kwa niaba ya Chadema

Chadema wametumia akili sana, na Serikali ya Raisi Samia ikaingia katika mtego wao bila kujitambua na kwa kukurupuka. Chadema walichotaka si wao wenyewe kuandamana, bali maandamano yamefanywa kwa niaba yao na Polisi wenyewe waliotumwa mitaani na serikali ya Raisi Samia. Kwa hiyo vyombo vya habari, badala ya kuonyesha wafuasi wa Chadema wakiandamana kudai haki za binadamu, lengo hili linatimizwa kwa wadau kupitia polisi walio mitaani kuzuia maandamano ya Chadema ya kudai serikali ikomeshe ukiukwaji wa haki za binadamu!

Kuna baadhi ya viongozi wakuu hata wametoa kauli za kuwaua wafuasi wa Chadema na kumvunja mguu wa pili Lissu. Yote haya yamesikiwa na umma wa watu, ndani na nje ya nchi.

Sasa hata mtoto mdogo anajua kwa nini leo Chadema walitaka kuandamana - anapouliza Polisi wanafanya nini mitaani! Maandamano yaliyofanywa na Polisi kwa niamba ya Chadema yamekuwa makubwa kwa kuingia mitaa mingi kuliko ambavyo Chadema wenyewe waneweza kufanya!

In fact, Chadema hapa wameua ndege wawili kwa jiwe moja; ujumbe wao kwa wananchi na hata nje ya nchi umefika, na pili wameonyesha kwa ushahidi ulio wazi ni jinsi gani serikali ya Raisi Samia inatumia vyombo vya dola na nguvu kubwa kukandamiza demokrasia nchini.

Kwa hiyo kwa hapa mpaka hii game inavyomalizika, magoli ni Chadema 2 Serikali 0

Anaemshauri Raisi Samia ni zero kabisa! Lakini Raisi Samia nae anatakiwa afuate ushauri wa Kikwete - za kuambiwa changanya na za kwako upate jibu sahihi!

Pia, soma: LIVE - Yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA 23/9/2024
IMG-20240923-WA0050.jpg
 
Back
Top Bottom