Serikali ya Tanzania imeshindwa kutafsiri dhana ya Burkina Faso?

Serikali ya Tanzania imeshindwa kutafsiri dhana ya Burkina Faso?

Hususan kwa watendaji, washauri wa Rais na vyombo vyetu vya intelijensia.

Nchi ndogo za magharibi ya Afrika zimeonesha jinsi Afrika inavyohitaji mabadiliko ya namna tunavyoongoza nchi na kusimamia Serikali.

Tanzania ni wakati umefika itazame uhalisia. Ya nchi hizo ndogo ni mfano mzuri sana, na tusidhani hayajafika Afrika Mashariki, yameshafika. Yanasambaa kama moto wa makumbi.

Leo tunashuhudia Kenya hata Polisi na Jeshi hawataki kuhusishwa na siasa na uongozi mbovu.

Tutakopa mpaka lini? Tutaendelea na kila kitu cha uongozi kukifanya siasa mpaka lini?

Tumeshuhudia watu kama Makonda wanaondokana na siasa za kulindana na kuingia kwenye uhalisia wa kumtumikia mwananchi. Naona mawaziri wachache sana wameliona hilo, lakini hawaonekani vilivyo na hawatumii media kuonesha dhahiri shahiri kuwa sasa siyo wakati wa siasa, ni wakati wa vitendo.

Tunataka tuone mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wakiondokana na dhanna ya kujitetea na kutetea ujinga, tunataka tuwaone wakitumikia wananchi muda wote.

Serikali iwachane kabisa na anasa za kijinga za magari ya kifahari kwa kila mkuu wa idara mpaka wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya. Hiyo ni dharau kubwa kwa wananchi wanyonge.

Kuna mengi sana ya kurekebisha na waziri wa fedha leo hii anakuja na bajeti ambayo haitekelezeki kwa jinsi fungu kubwa linavyokwenda kwenye matumiazi ya anasa. Anasa ya kwanza inayojionesha wazi wazi ni kwa Mtanzania wa kawaida, ni wakuu wote, kuaniza wa idara mpaka mawaziri kutembelea magari ya anasa ambayo ni mzigo mkubwa kwa nchi ya kimasikini.

Serikali ijirekebishe, tusifikiri sisi ni kisiwa, sisi ni nchi inayopakana na nchi nyingi Afrika. mabadiliko ya mama anayoyataka kwenye R zake nne yawekwe wazi, siyo kutangaza mabadiliko wakati naamini hata mawaziri hawaelewi ni mabadiliko yepi.

Naamini katika watendaji na idara zote za serikali waliyoelewa dhanna ya R nne ni wachache sana. Ofisi ya Rais inayohusika na habari inatakiwa itowe elimu kubwa kwa serikali na wananchi ili wote tuelewe ni kupi, kupatana, kustahamili, kubadilika na kujenga upya kuliko kusudiwa na falsafa ya R nne za mama Samia.

Ukifatilia habari za Burkina Faso kwa sasa, utaona kuwa wanaziishi R nne za mama Samia bila kuwa nazo.
Sisi tulionazo tunashindwa kuziishi.
Kuna mtu ameiba PC Yako na kutype haya?

Anyway, Putin amedhamiria time hii, Afrika itanyooka tu!!
 
Ni wewe Faiza umeandika huu uzi au Akaunti yako imevamiwa!🤣🤣🤣🤣
Tulieni Mama afungue nchi!
Naam, "msiogope mabadiliko, nendeni mkabadilike" - Rais mama Samia.
 
Serikali ijirekebishe, tusifikiri sisi ni kisiwa,
Too late. Too little.The die is cast.
Kwanza hata hamjui muanzie wapi!

Huyo mwenye hizo 'R', kwanza yeye mwenyewe hajui zinahusu nini?

Ni kama umezinduka toka usingizini, ambako umetokewa na njozi ya kutisha sana!
Hiyo haikuwa ndoto; hii ni hali halisi.
 
Hususan kwa watendaji, washauri wa Rais na vyombo vyetu vya intelijensia.

Nchi ndogo za magharibi ya Afrika zimeonesha jinsi Afrika inavyohitaji mabadiliko ya namna tunavyoongoza nchi na kusimamia Serikali.

Tanzania ni wakati umefika itazame uhalisia. Ya nchi hizo ndogo ni mfano mzuri sana, na tusidhani hayajafika Afrika Mashariki, yameshafika. Yanasambaa kama moto wa makumbi.

Leo tunashuhudia Kenya hata Polisi na Jeshi hawataki kuhusishwa na siasa na uongozi mbovu.

Tutakopa mpaka lini? Tutaendelea na kila kitu cha uongozi kukifanya siasa mpaka lini?

Tumeshuhudia watu kama Makonda wanaondokana na siasa za kulindana na kuingia kwenye uhalisia wa kumtumikia mwananchi. Naona mawaziri wachache sana wameliona hilo, lakini hawaonekani vilivyo na hawatumii media kuonesha dhahiri shahiri kuwa sasa siyo wakati wa siasa, ni wakati wa vitendo.

Tunataka tuone mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wakiondokana na dhanna ya kujitetea na kutetea ujinga, tunataka tuwaone wakitumikia wananchi muda wote.

Serikali iwachane kabisa na anasa za kijinga za magari ya kifahari kwa kila mkuu wa idara mpaka wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya. Hiyo ni dharau kubwa kwa wananchi wanyonge.

Kuna mengi sana ya kurekebisha na waziri wa fedha leo hii anakuja na bajeti ambayo haitekelezeki kwa jinsi fungu kubwa linavyokwenda kwenye matumiazi ya anasa. Anasa ya kwanza inayojionesha wazi wazi ni kwa Mtanzania wa kawaida, ni wakuu wote, kuaniza wa idara mpaka mawaziri kutembelea magari ya anasa ambayo ni mzigo mkubwa kwa nchi ya kimasikini.

Serikali ijirekebishe, tusifikiri sisi ni kisiwa, sisi ni nchi inayopakana na nchi nyingi Afrika. mabadiliko ya mama anayoyataka kwenye R zake nne yawekwe wazi, siyo kutangaza mabadiliko wakati naamini hata mawaziri hawaelewi ni mabadiliko yepi.

Naamini katika watendaji na idara zote za serikali waliyoelewa dhanna ya R nne ni wachache sana. Ofisi ya Rais inayohusika na habari inatakiwa itowe elimu kubwa kwa serikali na wananchi ili wote tuelewe ni kupi, kupatana, kustahamili, kubadilika na kujenga upya kuliko kusudiwa na falsafa ya R nne za mama Samia.

Ukifatilia habari za Burkina Faso kwa sasa, utaona kuwa wanaziishi R nne za mama Samia bila kuwa nazo.
Sisi tulionazo tunashindwa kuziishi.

Siamini kama faiza unaweza ukawa smart hivi. Siku zote sasa mbona huwa unajitoa akili? Au account yako imekuwa hacked? Tukiwaambia kuwa hata sisi tumefaidika na mfumo lakini imefikia hatua tunajisikia guilty. Hizi pesa zinakopwa tunakula tu posho na safari. Sometimes inakuja huruma nikiwatizama watanzania wenzangu kwa kodi na tozo walizo nazo. Mnyeezi Mungu atusamehe.
 
Siamini kama faiza unaweza ukawa smart hivi. Siku zote sasa mbona huwa unajitoa akili? Au account yako imekuwa hacked? Tukiwaambia kuwa hata sisi tumefaidika na mfumo lakini imefikia hatua tunajisikia guilty. Hizi pesa zinakopwa tunakula tu posho na safari. Sometimes inakuja huruma nikiwatizama watanzania wenzangu kwa kodi na tozo walizo nazo. Mnyeezi Mungu atusamehe.
Hunisomi tu, pitia nyuzi zangu nakuwekea link chini, nisome kwa utuvu, utanielewa tu:

 
Back
Top Bottom