JF ya zamani tofauti na ya sasa kabisa, yeye anamwita mwenzie muongo kumbe yeye ndo muongo kabisaUmepata wapi data. Kuna graduates, kuna diploma, kuna certificate.... Vyuo vya ualimu vipo vingapi halafu useme 1200
mmea wa MadagascarAkili za mwendazake alikua anazijua mwenyewe yaan Kuna muda mpak unajiuliza anatumia mmea au?
Wewe hujasoma vyuo naona.uongo vyuo vyetu vyote ukijumlisha vinatoa graduate 1200 tu wa ualimu kwa mwaka ukipiga kwa miaka 20 nyuma ni elfu 24 tu!! hiyo laki tano umeitoa wapi?
Kwani wapoo?Sasa wahakikishe hakuna mambo ya wenye vyeti feki
Kwa ualimu pekee ni zaidi ya laki moja maana serikal haijaajiri kwa miaka mingi kwa laki tano labda na sekta nyingine ila hiyo takwimu ya graduate 1200 sio kwel ni chache mnouongo vyuo vyetu vyote ukijumlisha vinatoa graduate 1200 tu wa ualimu kwa mwaka ukipiga kwa miaka 20 nyuma ni elfu 24 tu!! hiyo laki tano umeitoa wapi?
Sure masterKada za afya na elimu na kilimo watumishi bado sana ,idadi ndogo hizo
Una uhakika ni huyo aliyekuwepo tangu 2016?Huyu Waziri toka 2016 mpaka leo Hadithi ni hii hii hakuna jipya hapo
Exaggeration laki tano hawafikiNdogo mnoooo hasa kwenya elimu, kuna graduate zaidi ya laki tano mtaani wa ualimu tu ambao wanaranda randa bila ramani.
Kwan polisi ni watumishi wa umma?JWZT sio watumishi wa umma kwa maana ya utumishi. Wana taratibu zao tofauti kidogo na watumishi wengine wa serikali.
Hawalindwi na sheria za utumishi wa umma.
Hilo halina maana kua hawalipwi mshahara kutoka kwenye pesa za umma.
Amekurupuka huyoExaggeration laki tano hawafiki
Mungu amzidishie baraka mama yetuPongezi kwa Mhe. Rais pia kwa Waziri wa Utumishi Mhe. Mchengelwa kwa kudhamiria kurudisha heshima kwa watumishi wa Umma maaana walifikia hatua mbaya sana, walilia sana mpaka machozi yamewa kauka, wamedai haki zao kwa kipindi kirefu sana!!
wamelalamika sana!! wametaabika sana!! wamedhalalika sana!!
kwa dhamira hii ya serikali ya awamu ya 6 kwa watumishi wa umma, hakika Mungu atazidisha neema na Baraka ktk Taifa letu.
mkuu tshs 720,000/= kwa mwalimu wa shule ya kata ni ndogo? siuache ufungue duka ujiajiriBinafsi sikubaliani na huu mfumo wa ajira wa sasa wa kutegemea ajira za serikali tu.
Serikali iboreshe mazingira watu wengi waajiriwe na sekta binafsi.
Serikali itaajiri hadi lini? Kwa presha ya sasa itabidi kila mwaka serikali ilazimike kuajiri ili kuwaziba watu midomo lakini hii sio njia nzuri ya kutatua tatizo.
Kwa mtindo huu wa kutegemea ajira za serikali na serikali ikawa inaajiri kila mwaka itafika wakati mapato yote na makusanyo yanaishia kwenye kulipana mishahara tu.
Serikali kwanza irekebishe mifumo, isambaze pesa sekta binafsi. Pili ipitie upya muundo wa watumishi wake. Unaenda shule za mjini waalimu 80, shule za vijijini waalimu 2.
Kabla ya kufikiria kuajiri, kwanza pitia miundo upya, boresha mazingira ya hao watumishi waliopo watafanya kazi kwa morali, mfano mwalimu leo analipwa 720,000. Unataka utajiri mwalimu mwingine, wakati hiyo hela ya mwalimu mpya ukiboresha mazingira kwa mwalimu aliepo ukamlipa 1M ama 1.1M, huyu atakua moralized sana na atafanya kazi hata ya waalimu 2.
Tuboreshe sekta binafsi kwanza, pili tuboreshe maslahi ya watumishi tulionao kabla ya kufikiria kuajiri wapya.
Huu ni uongoKada ya elimu wataajiri watumishi wapya 10,297, afya 11,215, kilimo 1,383, mifugo 1,250, uvuvi 733, Jeshi la Polisi 1,782, Magereza 843, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji 512 na watumishi wapya wa hospitali za mashirika ya kidini na hiari 1,240.
Serikali ya Tanzania imesema katika mwaka wa fedha 2021/22 inatarajia kuajiri watumishi wa umma wapya 44,096.
Hayo yameelezwa leo Alhamisi Aprili 22, 2021 Waziri wa Nchi Ofisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilishwa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2021/22.
Amesema kada ya elimu wataajiri watumishi wapya 10,297, afya 11,215, kilimo 1,383, mifugo 1,250, uvuvi 733, Jeshi la Polisi 1,782, Magereza 843, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji 512 na watumishi wapya wa hospitali za mashirika ya kidini na hiari 1,240.
Amesema Serikali itaajiri watumishi 14,841 wa kada mbalimbali ikiwemo wahadhiri wa vyuo vikuu vyote vya umma nchini pamoja na kada nyingine ambazo haziko kwenye sekta zilizoainishwa awali.
Hata hivyo, amesema watumishi 92,619 wa kada mbalimbali watapandishwa vyeo na watumishi 2,360 watabadilishwa kada katika utumishi.
Amebainisha kuwa maelekezo yatakayotolewa wakati huo ni kuchambua na kuhakiki madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa umma 17,699 yenye thamani ya Sh37.47 bilioni na kuchukua hatua ipasavyo.
Aprili 15, 2021 Serikali ya Tanzania ilieleza matarajio yake ya kuajiri watumishi wapya 44,811 katika mwaka wa fedha 2020/21.
Hayo yalielezwa na aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika wakati akiwasilisha bajeti yake kwa mwaka huo wa fedha.
Alitaja ajira hizo mpya kuwa ni kada ya elimu (13,529), afya (10,467), kilimo, mifugo na uvuvi (2,145) Jeshi la Polisi (2,725), magereza (685), Jeshi la Zimamoto (501), uhamiaji (495) na hospitali za mashirika ya kidini na hiyari (1,262).
Chanzo: MWANANCHI
Hiyo ni kwa mwalimu wa degree, unafahamu wa certificate analipwa sh ngapi?mkuu tshs 720,000/= kwa mwalimu wa shule ya kata ni ndogo? siuache ufungue duka ujiajiri
hiyo degree ya geography na history hiyo hela nyingi hivyo kwa kazi gani unayofanya? naona tuanzishe opras na walimu waajiriwe kwa mkataba wa miaka mitatu mitatu kama ElitreaHiyo ni kwa mwalimu wa degree, unafahamu wa certificate analipwa sh ngapi?
Hujajibu swali, certificate analipwa ngapi?hiyo degree ya geography na history hiyo hela nyingi hivyo kwa kazi gani unayofanya? naona tuanzishe opras na walimu waajiriwe kwa mkataba wa miaka mitatu mitatu kama Elitrea