Serikali ya Tanzania mshawishini Trump arejeshe misaada

Serikali ya Tanzania mshawishini Trump arejeshe misaada

Lakini ujue yeye binafsi hatapata hasara sababu kodi zetu zipo. Raia wa kawaida ndo tutapata shida
Wote tutapata shida..
Ikiwa misaada ya US itakatwa na serikali haijajipanga kuziba pengo hilo, wananchi watahisi athari moja kwa moja, hasa katika sekta za afya, elimu, na upatikanaji wa chakula, kupungua kwa dawa za ukmw,miradi ya afya inaweza kuchochea hasira ya wananchi na hapa ndipo patamu sana...

Ikiwa Marekani itaondoa AGOA na biashara za Afrika zitapoteza soko la US, viwanda vinavyouza bidhaa kama mavazi na bidhaa za kilimo vinaweza kufungwa, na kusababisha ukosefu wa ajira hapa ni patamu sana sana... kwani wananchi wanaoweza kuathirika moja kwa moja wanaweza kuandamana kupinga hali ngumu ya maisha...(hapa wameanza kupata akili na kuacha kufuatilia Zuchu na Diamond, Aziz Ki na Mobeto, Simba na Yanga)

Kwa sababu viongozi wamekuwa wakitumia misaada kwa manufaa binafsi, wananchi wanaweza kuona upungufu wa misaada kama uthibitisho wa ufisadi wa serikali... hapa patamu sana tena sana ...:ClapHD::EZclap::ClapHD::EZclap::JustClap: kwani Ikiwa wananchi walikuwa hawaoni faida ya misaada hata kabla ya kukatwa, kukosekana kabisa kwa fedha hizo kunaweza kuzidisha hali ya kuchoshwa na uongozi mbaya....


Sasa ndipo kina mzee Tundu na wenzake wanatia timu panazidi kunoga zaidi.. kwani upinzani na wanaharakati wanaweza kutumia hali hii kama nafasi ya kushinikiza mabadiliko ya uongozi kwa kuhamasisha maandamano. Mitandao ya kijamii ikiwemo X na jf havitokaa mbali, inaweza kuongeza uhamasishaji na kusababisha maandamano makubwa zaidi.

Tumeshuhudia kwa wenzetu Kenya hapo maandamano dhidi ya serikali kwa sababu ya hali ngumu ya maisha, kodi kubwa, na ukosefu wa ajira.

Hivyo Ulaya, US, China, wazidi kukaza ili akili itukae sawa...
 
Kumekuwa na sintofahamu baada ya Trump kuzuia misaada kwa nchi mbambali kutokana na kile anachokiita misaada hiyo kutoinufaisha Marekani moja kwa moja. Hapa nchini marufuku hiii imezua mijadala mingi sana ikiwemo kwenye jukwaa letu hili pendwa. Watu mbali mbali wamekuwa wakionekana kufurahia swala hili na kufikia hatua ya kuzitaka serikali ianze kujitegemea kwa kutumia rasilimali nyingi zilizopo kutoa huduma zilizositishwa na Trump. Katika baadhi ya mijadala wapo watu wamefikia hadi hatua ya kufurahia wenzao kukosa kazi kwenye mashirika mbali mbali yasiyo ya serikali (NGOs) kwa kile wanachosema watu hawa walikuwa wanaringa sana kutokana na maslahi makubwa waliyokuwa wakipata

Japo sipingani na hoja ya kutaka mataifa ya ki Afrika kupunguza kutegemea misaada kutoka kwa wahisani lakini ukweli na uhalisia ni kwamba viongozi wengi wa nchi za ki Afrika hawana muda na hawawajali wanachi wao. Na kwa hivyo misaada hiyo ikikosekana tusitegemee vipaumbele kubadilika. Hizi ni nchi ambazo viongozi wako tayari raia wale nyasi ili wanunue ndege ya rais na magari ya kifahari kwa ajili ya viongozi. Ni nchi ambazo wananchi wakilalalamika kuhusu tozo na kodi mbali mbali wanaambiwa wahame nchi.

Ni nchi ambazo viongozi wanathaminiwa kuliko wananchi, mnaweza mkasimamishwa zaidi ya dakika 40 mkisubiri msafara wa kiongozi upite bila kujali mnawahi wapi. Hizi nchi amabazo raia wanaotoa kodi wanaweza kuwa wanapita barabara mbovu yenye mashimo kila siku na hakuna anayejali lakini akija kiongozi mkuu wa chama tawala mashimo yote yanafukiwa siku hiyo hiyo

Trump ni mfanyabiashara na kwa hivyo kila kitu kwake ni mauziano (nakupa hiki na we nipe kile) tumeona mifano mingi ya nchi kama Canada na Mexico alivyoweka tariffs lakini baada ya kufanya naye mazungumzo na kumwahidi mambo aliyokuwa anataka kasogeza muda wa tarrifs kwa siku 30 na inawezekana akaondoa kabisa. Wakati wanasitisha misaada hiyo, waziri wa mambo ya nje (secretary of state) Bwana Rubio alisema wanataka waangalie misaada hiyo inanufaisha vipi Marekani.
Ni wakati muafaka kwa wana diplomasia wa nchi yetu kuongea na Trump na kumsikiliza anataka nini. Kama tumeweza kuwapa waarabu Ngorongoro na bandari huku wachina tukiwazawadia gesi kwanini tusitafute cha kuwapa wamarekani. Wao wanatupa misaada inayonufaisha watu wengi lakini mikataba ya madini na uwekezaji mingi tunawapa wachina, waarabu na waturuki, lazima wasione faida ya misaada yao. Na wakati mwingine tunawadhihaki na kuwaita mabeberu. Hawa waarabu na wachina wanatoa misaada gani? Wengine hapa misaada yao ni tende na kujenga tu nyumba za ibada, wachina ndo kwanza wameanza hadi kufanya kazi za wazawa na si tunawaangalia tu.

Na kwa wale mnaofurahia mnajua hasara kwa nchi na uchumi kwa ujumla? Kuna NGO hapa wilayani inapeleka PAYE zaidi ya Tsh 11M kwa mwezi, kuna NGO ngapi nchi hii? Vipi pesa wanayopeleka NSSF na PSSSF?. Wanatoa tender za magari, insurance na stationeries kwa wadau wengi tu. Nchi yetu ina uwezo wa kuwaajiri wafanyakazi wote kama watapoteza kazi? Familia ngapi zinawategemea?

Hivi unajua wafanyakazi hawa huwa wanajua kutumia pesa ipasavyo na kusababisha mzunguko mkubwa wa pesa? Waulize watu wenye baa, lodge na hotel jinsi wanavyopata pesa hawa jamaa wakienda semina na mafunzo mbali mbali na mapumziko (retreat). Kama una hotel au mgahawa na unawategemea wafanyakazi wa serikalini jiandae kuufunga, mara nyingi wanakunywa chai ya rangi na chapati au andazi. Ukiwatajia bei ya supu ya samaki au kuku wanatoa macho utafikiri umewaambia rangi ya nguo ya ndani ya wapenzi wao. Na hawa ndio wanaongoza kwa kuwakejeli wafanyakazi wa hizi NGO. Hawa watu wanajenga nyumba za hatari na mafundi wananufaika, faida ni nyingi sana. Wafanyabiashara wengi wanajua umuhimu wa hawa watu.

Ni wakati muafaka sasa kwa Balozi wetu wa USA, na wanadiplomasia wote kuzngumza na wenzao ili hali isiharibike zaidi

Soma: Pre GE2025 - Wabunge waiomba Serikali kuwatumia watumishi walisimamishwa kazi USAID
Mada ndefu afu umeandika upumbavu wako.
 
Wote tutapata shida..
Ikiwa misaada ya US itakatwa na serikali haijajipanga kuziba pengo hilo, wananchi watahisi athari moja kwa moja, hasa katika sekta za afya, elimu, na upatikanaji wa chakula, kupungua kwa dawa za ukmw,miradi ya afya inaweza kuchochea hasira ya wananchi na hapa ndipo patamu sana...

Ikiwa Marekani itaondoa AGOA na biashara za Afrika zitapoteza soko la US, viwanda vinavyouza bidhaa kama mavazi na bidhaa za kilimo vinaweza kufungwa, na kusababisha ukosefu wa ajira hapa ni patamu sana sana... kwani wananchi wanaoweza kuathirika moja kwa moja wanaweza kuandamana kupinga hali ngumu ya maisha...(hapa wameanza kupata akili na kuacha kufuatilia Zuchu na Diamond, Aziz Ki na Mobeto, Simba na Yanga)

Kwa sababu viongozi wamekuwa wakitumia misaada kwa manufaa binafsi, wananchi wanaweza kuona upungufu wa misaada kama uthibitisho wa ufisadi wa serikali... hapa patamu sana tena sana ...:ClapHD::EZclap::ClapHD::EZclap::JustClap: kwani Ikiwa wananchi walikuwa hawaoni faida ya misaada hata kabla ya kukatwa, kukosekana kabisa kwa fedha hizo kunaweza kuzidisha hali ya kuchoshwa na uongozi mbaya....


Sasa ndipo kina mzee Tundu na wenzake wanatia timu panazidi kunoga zaidi.. kwani upinzani na wanaharakati wanaweza kutumia hali hii kama nafasi ya kushinikiza mabadiliko ya uongozi kwa kuhamasisha maandamano. Mitandao ya kijamii ikiwemo X na jf havitokaa mbali, inaweza kuongeza uhamasishaji na kusababisha maandamano makubwa zaidi.

Tumeshuhudia kwa wenzetu Kenya hapo maandamano dhidi ya serikali kwa sababu ya hali ngumu ya maisha, kodi kubwa, na ukosefu wa ajira.

Hivyo Ulaya, US, China, wazidi kukaza ili akili itukae sawa...
Una logic nzuri sana, wasiwasi wangu ni kwamba ni raia wachache sana nchi wanaweza kuandamana na kuishinikiza serikali kutokana na aidha kukosa elimu au uoga na uchawa uliopitiliza. Kuna mambo ya hovyo sana nchi hii toka kitambo lakini watu wanakufa kimya kimya. Hata wasomi wetu wa kuelimisha raia na kuwa mstari wa mbele wengi wao wameamua kuwa machawa tu
 
Kumekuwa na sintofahamu baada ya Trump kuzuia misaada kwa nchi mbambali kutokana na kile anachokiita misaada hiyo kutoinufaisha Marekani moja kwa moja. Hapa nchini marufuku hiii imezua mijadala mingi sana ikiwemo kwenye jukwaa letu hili pendwa. Watu mbali mbali wamekuwa wakionekana kufurahia swala hili na kufikia hatua ya kuzitaka serikali ianze kujitegemea kwa kutumia rasilimali nyingi zilizopo kutoa huduma zilizositishwa na Trump. Katika baadhi ya mijadala wapo watu wamefikia hadi hatua ya kufurahia wenzao kukosa kazi kwenye mashirika mbali mbali yasiyo ya serikali (NGOs) kwa kile wanachosema watu hawa walikuwa wanaringa sana kutokana na maslahi makubwa waliyokuwa wakipata

Japo sipingani na hoja ya kutaka mataifa ya ki Afrika kupunguza kutegemea misaada kutoka kwa wahisani lakini ukweli na uhalisia ni kwamba viongozi wengi wa nchi za ki Afrika hawana muda na hawawajali wanachi wao. Na kwa hivyo misaada hiyo ikikosekana tusitegemee vipaumbele kubadilika. Hizi ni nchi ambazo viongozi wako tayari raia wale nyasi ili wanunue ndege ya rais na magari ya kifahari kwa ajili ya viongozi. Ni nchi ambazo wananchi wakilalalamika kuhusu tozo na kodi mbali mbali wanaambiwa wahame nchi.

Ni nchi ambazo viongozi wanathaminiwa kuliko wananchi, mnaweza mkasimamishwa zaidi ya dakika 40 mkisubiri msafara wa kiongozi upite bila kujali mnawahi wapi. Hizi nchi amabazo raia wanaotoa kodi wanaweza kuwa wanapita barabara mbovu yenye mashimo kila siku na hakuna anayejali lakini akija kiongozi mkuu wa chama tawala mashimo yote yanafukiwa siku hiyo hiyo

Trump ni mfanyabiashara na kwa hivyo kila kitu kwake ni mauziano (nakupa hiki na we nipe kile) tumeona mifano mingi ya nchi kama Canada na Mexico alivyoweka tariffs lakini baada ya kufanya naye mazungumzo na kumwahidi mambo aliyokuwa anataka kasogeza muda wa tarrifs kwa siku 30 na inawezekana akaondoa kabisa. Wakati wanasitisha misaada hiyo, waziri wa mambo ya nje (secretary of state) Bwana Rubio alisema wanataka waangalie misaada hiyo inanufaisha vipi Marekani.
Ni wakati muafaka kwa wana diplomasia wa nchi yetu kuongea na Trump na kumsikiliza anataka nini. Kama tumeweza kuwapa waarabu Ngorongoro na bandari huku wachina tukiwazawadia gesi kwanini tusitafute cha kuwapa wamarekani. Wao wanatupa misaada inayonufaisha watu wengi lakini mikataba ya madini na uwekezaji mingi tunawapa wachina, waarabu na waturuki, lazima wasione faida ya misaada yao. Na wakati mwingine tunawadhihaki na kuwaita mabeberu. Hawa waarabu na wachina wanatoa misaada gani? Wengine hapa misaada yao ni tende na kujenga tu nyumba za ibada, wachina ndo kwanza wameanza hadi kufanya kazi za wazawa na si tunawaangalia tu.

Na kwa wale mnaofurahia mnajua hasara kwa nchi na uchumi kwa ujumla? Kuna NGO hapa wilayani inapeleka PAYE zaidi ya Tsh 11M kwa mwezi, kuna NGO ngapi nchi hii? Vipi pesa wanayopeleka NSSF na PSSSF?. Wanatoa tender za magari, insurance na stationeries kwa wadau wengi tu. Nchi yetu ina uwezo wa kuwaajiri wafanyakazi wote kama watapoteza kazi? Familia ngapi zinawategemea?

Hivi unajua wafanyakazi hawa huwa wanajua kutumia pesa ipasavyo na kusababisha mzunguko mkubwa wa pesa? Waulize watu wenye baa, lodge na hotel jinsi wanavyopata pesa hawa jamaa wakienda semina na mafunzo mbali mbali na mapumziko (retreat). Kama una hotel au mgahawa na unawategemea wafanyakazi wa serikalini jiandae kuufunga, mara nyingi wanakunywa chai ya rangi na chapati au andazi. Ukiwatajia bei ya supu ya samaki au kuku wanatoa macho utafikiri umewaambia rangi ya nguo ya ndani ya wapenzi wao. Na hawa ndio wanaongoza kwa kuwakejeli wafanyakazi wa hizi NGO. Hawa watu wanajenga nyumba za hatari na mafundi wananufaika, faida ni nyingi sana. Wafanyabiashara wengi wanajua umuhimu wa hawa watu.

Ni wakati muafaka sasa kwa Balozi wetu wa USA, na wanadiplomasia wote kuzngumza na wenzao ili hali isiharibike zaidi

Soma: Pre GE2025 - Wabunge waiomba Serikali kuwatumia watumishi walisimamishwa kazi USAID
We ni mojawapo siyo, hujajiwekea akiba? Au ndiyo umeziponda zote km unavyowasifu kwa manunuzi na ulevi wao baa
 
Misaada ya neti, mseto, na arv ndio inafika kwa maskini lakini misaada ya fedha inaishia mifukoni mwao watawala, Trump afinye hapo hapo
Sasa wakikata na hiyo misaada si ndo hao raia watakufa ndugu. Hakuna atakayewajali nchi hii
 
We ni mojawapo siyo, hujajiwekea akiba? Au ndiyo umeziponda zote km unavyowasifu kwa manunuzi na ulevi wao baa
Mimi sio mmoja wapo lakini naliangalia swala hili kwa mapana yake. Kodi, ajira na kwa wafanya biashara na uchumi kwa ujumla
 
Una logic nzuri sana, wasiwasi wangu ni kwamba ni raia wachache sana nchi wanaweza kuandamana na kuishinikiza serikali kutokana na aidha kukosa elimu au uoga na uchawa uliopitiliza. Kuna mambo ya hovyo sana nchi hii toka kitambo lakini watu wanakufa kimya kimya. Hata wasomi wetu wa kuelimisha raia na kuwa mstari wa mbele wengi wao wameamua kuwa machawa tu
Mkuu linapokuja suala maisha ya wananchi kuathirika moja kwa moja lazima wataweka hofu pembeni..
ugumu w maisha ukifikia kiwango kisichovumilika, hata wale waliokuwa na hofu wanaweza kuona haja ya kuchukua hatua na hapo ndipo vyama vya upinzani au wanaharakati watahamasisha wananchi na kupata mwitikio mkubwa, maandamano yanaweza kutokea.

Trump aendelee kushikilia hapo hapo...
 
Daaa Kuna majitu yamenenepeana serikalin huko, yaan unakuta jitu linapumua kama limo kwenye chupa. Ukiulizia ni nani huyo utasikia ni afisa wa tra, mkurugez wa tanesko, mkurugenz wa nida, mkuu tanapa,mshauri wa mama yaan.
 
Acha tusonge hivihivi kuna baadhi ya mafuvu hayajifunzi Kwa kuambiwa Bali Kwa maumivu

Huruma siyo malezi
 
Daaa Kuna majitu yamenenepeana serikalin huko, yaan unakuta jitu linapumua kama limo kwenye chupa. Ukiulizia ni nani huyo utasikia ni afisa wa tra, mkurugez wa tanesko, mkurugenz wa nida, mkuu tanapa,mshauri wa mama yaan.
Hawa jamaa hata misaada ikikata hawajali na wala hawatahangaika kusaidia watu. Wao wana uhakika
 
Msaada siyo lazima, hizo ni kodi za wananchi kama nyie wa U.S.A. Jifunzeni kujitegemea na muanze kuhoji matumizi ya kodi zenu.
 
Msaada siyo lazima, hizo ni kodi za wananchi kama nyie wa U.S.A. Jifunzeni kujitegemea na muanze kuhoji matumizi ya kodi zenu.
Lakini mapato yetu madogo kuliko mahitaji. Bila misaada na mikopo hatutoboi
 
Trump yupo sahihi anawasaidia waafrika wajitegemee why misaaada Hali utajiri kila mahali.
Utajiri wa wilaya moja tu ya Ulanga unailisha Tanzania miaka kumi bila tegemeo la Kodi toka kwa wananchi.
Kama wilaya za Tunduru na Ulanga ndizo zinakuza uchumi wa nchi za Thailand na Sri Lanka we huoni tunapaswa kuchapwa viboko
Tuchapwe viboko nchi nzima?
 
Back
Top Bottom