Serikali ya Tanzania yakopa Dola Milioni 140 kujenga mradi wa kufua umeme wa Mto Malagarasi

Kwani huu wa Rufiji hautoshi?
Hapo sasa, tunaambiwa mradi wa SG utazalisha 2,115mg, yaani tutakuwa na ziada ya umeme maradufu. Sasa hii mikopo ya umeme mwingine ni ili iweje? Utapeli mwingine bana ni hatari kabisa.
 
Sioni dhambi yoyote kuwa na vyanzo vingi vya umeme kwa nchi kama yetu. Vitatusaidia sana huko mbeleni.

Tatizo letu ni mawazo ya kisiasa kutangalizwa mbele kila wakati. Nchi ya viwanda, yenye kutegemea kuwa na treni za kisasa haiwezi kuzitegemea megawatts 2115 tu.
 
Sahau kuhusu hilo. Mnadungwa sindano pole pole. Mtakuja kushtuka imeisha ingia yote.
1. Corona chanjo imekubaliwa
2. Wawekezaji wameombwa msamaha na kurudishwa
3. Mahusiano na kenya yameimarishwa
4. Walipa kodi wamepunguziwa makali na kubembelezwa
5. Ulaya wameanza kuupenda uongozi wa sasa

We hushtuki tu
 
Kwani huu wa Rufiji hautoshi?
Maana una uwezo zaidi ya vyanzo vyote vilivyopo kwa sasa na ziada ya kuuza nje ya nchi, sasa kukopa kwa miradi mingine ili iweje sasa..
 
Sawasawà
 
Mahitaji ya umeme nchi nzima bwawa la nyerere kukamilika tunabakiwa na ziada tutauza kwa majirani

Malagarasi ya nini Tena?ikiwa nyerere dam haijakamilika?tukamilishe rufiji ikiwa hautishi tutatafakari muda ukifika hiyo peas ya mikopo........
Tunakuwa na mipango mingi sana ya kuendeleza umeme nchini lakini hatuoni umuhimu wa kuwa na mradi mmoja tu kuweza kufanya hivyo. JNHEP ukikamilika utawezesha kuwa na umeme wa ziada. Sasa fedha hii badala ya kutumika kukamilisha mradi huo, tunaanzisha mradi mpya kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…