Serikali yaandaa Mkutano wa Siku 3 kwa Wadau kutoa Maoni kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2024

Serikali yaandaa Mkutano wa Siku 3 kwa Wadau kutoa Maoni kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2024

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu, tukashiriki kutoa maoni, majirani wameikataa yao na mpaka sasa wapo kwenye maandamano. Tuchukue somo kwao, kama hatujailewa basi na ijulikane.

Nimeambatisha Muswado huo hapo chini kwaajili ya mapitio.

Wito wa wadau kuja kutoa maoni kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2024.jpg


TAARIFA KWA UMMA

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imepanga kupokea maoni ya wadau kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2024, (The Finance Bill, 2024) kwa mujibu wa Kanuni ya 97(2) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Februari 2023.

Mkutano wa kupokea na kusikiliza maoni ya wadau (Public Hearing) utafanyika kuanzia siku ya Jumapili tarehe 23 Juni, 2024 hadi Jumanne tarehe 25 Juni, 2024. Majadiliano hayo yataanza saa 4:00 asubuhi katika Ukumbi wa Piusi Msekwa, Ofisi ya Bunge Jijini Dodoma.

Kamati inawaalika watu wote wenye maoni kuhusu Muswada huo kufika na kuwasilisha maoni yao kabla haujapelekwa katika hatua nyingine.

Vilevile itapokea maoni kwa njia ya posta au Barua pepe kwa anuani ifuatayo:-

Katibu wa Bunge,
Ofisi ya Bunge,
Mtaa wa Makole
S.L.P. 941
41105 DODOMA

Barua pepe: cna@bunge.go.tz na kamati@bunge.go.tz

Muswada huo pia unaweza kupakuliwa katika tovuti ya Bunge, www.bunge.go.tz. Aidha, unashauriwa kuwasilisha jina lako kupitia barua pepe tajwa endapo utaenda kuwasilisha maoni yako kwa kuzungumza kwa ajili yah atua zaidi.

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa,
Ofisi ya Bunge,
S.L.P 941,
DODOMA.
 

Attachments

Uko kwa Kiswahili au Kingereza??
Hapo ndio kipengele Mkuu, ni kinge kote isipokuwa kwenye kipengele cha marekebisho ya sheria ya bima ya afya kwa wote
 
Kama Kenya 😄
Tuanze kukiwasha na sisi... ila wabongo ni mwendo wa kugugumia kimya kimya mambo yanaenda, utafikiri tumerogwa... bila kusahau nyie chawa🙁🙄 ambao kila kitu mnasapoti hata kama unajua fika ni makamasi
 
Tuanze kukiwasha na sisi... ila wabongo ni mwendo wa kugugumia kimya kimya mambo yanaenda, utafikiri tumerogwa... bila kusahau nyie chawa🙁🙄 ambao kila kitu mnasapoti hata kama unajua fika ni makamasi
Unadhani Wabongo wenyewe hata hiyo Finance Bill Wanainua?
 
Wakuu, tukashiriki kutoa maoni, majirani wameikataa yao na mpaka sasa wapo kwenye maandamano. Tuchukue somo kwao, kama hatujailewa basi na ijulikane
Unaongea na maiti zinazotembea? Zitakuelewa kweli?

1. Samia alioweka tozo kwenye miamala, hakuna aliyeinua mdomo. Tukaambiwa asiyetaka ahamie Burundi.
2. Samia ametupilia mbali maoni ya wadau wa vyama vya siasa, viongozi wa dini na wananchi kuhusu sheria za uchaguzi na tume huru, lkn kimyaaa.!!!
3. Maoni na vilio vya watanzania kuhusu DP World yametupiliwa mbali na mkataba ukasainiwa.
4. Jiwe aliwanyima wafanyakazi (wakiwemo wanajeshi) haki yao ya kisheria ya kupata annual increments, hawakusema chochote.
5. Jiwe alivunja katiba wazi wazi kwa kuvikataza vyama vya siasa kufanya mikutano, wapinzani wakaufyata na wananchi wakachekelea..

Sembuse hili ?? Kwanza nani anajua kinachoendelea bungeni? Watu wako bize na ukahaba wa Kinondoni kwasabb ndiyo mambo yao.
 
Wakutusikiliza kishasema yeye chura hasikii. Hivi DP wedi tulisikilizwa. Hivi maoni ya tume huru ya uchaguzi je. Leo ndiyo yatokee maajabu?
 
Akili zenyewe za kujadili mnazo? Au mnaenda kuuza sura?
 
Hapo ndio kipengele Mkuu, ni kinge kote isipokuwa kwenye kipengele cha marekebisho ya sheria ya bima ya afya kwa wote
Watanzania wengi hawajui Kingereza, watajadilije?
 
Unadhani Wabongo wenyewe hata hiyo Finance Bill Wanainua?
Wabongo wanafatilia Mkuu, sema ndio hivyo kuna kuvunjika moyo baada ya kuwa yanayopendekezwa hayafiki, mwisho wa siku watu wanajiuliza nini maana ya kutaka maoni kama hayachukuliwi?
 
Unaongea na maiti zinazotembea? Zitakuelewa kweli?

1. Samia alioweka tozo kwenye miamala, hakuna aliyeinua mdomo. Tukaambiwa asiyetaka ahamie Burundi.
2. Samia ametupilia mbali maoni ya wadau wa vyama vya siasa, viongozi wa dini na wananchi kuhusu sheria za uchaguzi na tume huru, lkn kimyaaa...
Dah maiti zinazotembea🙁... labda hasira zimeongezeka Mkuu, ngoja tuone itakuaje
 
Wakutusikiliza kishasema yeye chura hasikii. Hivi DP wedi tulisikilizwa. Hivi maoni ya tume huru ya uchaguzi je. Leo ndiyo yatokee maajabu?
Lolote linaweza kutokea Mkuu, ndio maana hatutakiwi kukata tamaa. Kila mmoja kwa nafasi yake ni muhimu kupiga kelele
 
Akili zenyewe za kujadili mnazo? Au mnaenda kuuza sura?
Chawa-Kupe kwenye ubora wako.... mwenyewe unaona unafanya la maana wakati unaandaa jehanamu kwa kizazi chako! U should be ashamed of yourself Mkuu! Kwa kila uozo unaotokea nchini jua na wewe una fungu lako hapo
 
Wabongo wanafatilia Mkuu, sema ndio hivyo kuna kuvunjika moyo baada ya kuwa yanayopendekezwa hayafiki, mwisho wa siku watu wanajiuliza nini maana ya kutaka maoni kama hayachukuliwi?
Kenya wamejadili Finance Bill Mwezi mzima
 
98% ya watanzania wana elimu ya St Kayumba haya mambo kwao ni kizungumkuti
 
Back
Top Bottom