Serikali yaendelea kuboresha miundombinu ya barabara mkoani Pwani

Serikali yaendelea kuboresha miundombinu ya barabara mkoani Pwani

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2017
Posts
458
Reaction score
1,280
Pwani

Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeendelea kuboresha na kufanya matengenezo ya miundombinu ya barabara katika mkoa wa Pwani ili kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila alipotembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali mkoani humo.

“Hapa Utete ambapo naona ujenzi unaendelea vizuri na tumesisitiza barabara ijengwe kwa ubora na kumalizika kwa wakati kwa manufaa ya wananchi, lakini pia tumetembelea ujenzi wa daraja la Muhoro ili kuona maendeleo yake kwani daraja lilikamilika litasaidia kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji z
kwa wananchi", alisema Mhandisi Mativila.

Pia, Mhandisi Mativila amewataka wasimamizi wa miradi hii kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kwa viwango kwa ajili ya manufaa ya wananchi.

Meneja wa TARURA Mkoa wa Pwani, Mhandisi Leopold
Runji ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa fedha za ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya barabara mkoani humo kwani wameweza kutatua kero za wananchi na kuwaletea maendeleo.

Alisema kuwa daraja la Muhoro ambalo awali lilijaa maji, sasa limepata ufumbuzi kwani wanaamini baada ya matengenezo kuisha wananchi wataendelea kutumia barabara bila matatizo.

Baadhi ya wananchi waliipongeza Serikali na kusema kukamilika kwa daraja hilo kutawasaidia wananchi kuvuka kwa urahisi na kuendelea na shughuli zao za kiuchumi na kijamii.

IMG-20240628-WA0133.jpg
 
Hapo Mkuranga barabara ya kuunga Mkuranga na kisarawe hali ni mbaya.
 
Mheshimiwa Samia anaupiga mwingi hongera mama
mitano Tena mama 😃😃😃
 
Pwani

Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeendelea kuboresha na kufanya matengenezo ya miundombinu ya barabara katika mkoa wa Pwani ili kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila alipotembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali mkoani humo.

“Hapa Utete ambapo naona ujenzi unaendelea vizuri na tumesisitiza barabara ijengwe kwa ubora na kumalizika kwa wakati kwa manufaa ya wananchi, lakini pia tumetembelea ujenzi wa daraja la Muhoro ili kuona maendeleo yake kwani daraja lilikamilika litasaidia kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji z
kwa wananchi", alisema Mhandisi Mativila.

Pia, Mhandisi Mativila amewataka wasimamizi wa miradi hii kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kwa viwango kwa ajili ya manufaa ya wananchi.

Meneja wa TARURA Mkoa wa Pwani, Mhandisi Leopold
Runji ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa fedha za ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya barabara mkoani humo kwani wameweza kutatua kero za wananchi na kuwaletea maendeleo.

Alisema kuwa daraja la Muhoro ambalo awali lilijaa maji, sasa limepata ufumbuzi kwani wanaamini baada ya matengenezo kuisha wananchi wataendelea kutumia barabara bila matatizo.

Baadhi ya wananchi waliipongeza Serikali na kusema kukamilika kwa daraja hilo kutawasaidia wananchi kuvuka kwa urahisi na kuendelea na shughuli zao za kiuchumi na kijamii.
ardhi inafumuliwa hadi inatoa machozi 🤣

for sure,
dare es salaam na pwani kuna kazi kubwa mno ya ujenzi wa barabara inaendelea, nadhani baada ya miaka miwili ijayo kitakua na mabandiko makubwa sana ya miundombinu ya barabara 🐒
 
Back
Top Bottom