Serikali yafuta maombi 2648 ya utafutaji wa madini kwa kutokidhi vigezo vya Sheria ya Madini

Serikali yafuta maombi 2648 ya utafutaji wa madini kwa kutokidhi vigezo vya Sheria ya Madini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-08-14 at 17.13.02_febcc9ae.jpg
Maombi 2648 ya utafutaji wa madini yafutwa katika kipindi cha kuanzia mwezi Oktoba 2023 hadi Julai 2024 kutokana na kutokidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura 123.

Hayo yamesemwa leo Agosti 14 , 2024 na Waziri wa Madini Anthony Mavunde wakati akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Bunge Nishati na Madini kuhusu hali ya Usimamizi na Uendelezaji wa Leseni zilizotolewa kwa ajili ya Utafutaji na Uchimbaji wa Madini.

Mavunde amesema kuwa maombi hayo yalifutwa baada ya kubainika kuwa, waombaji hawakuwa na nia ya kupatiwa leseni za utafutaji madini na badala yake walikuwa wameyashikilia na kuhodhi maeneo hayo na hivyo kuwanyima fursa wenye nia ya kuyaendeleza.
WhatsApp Image 2024-08-14 at 17.13.05_1fb9fdc6.jpg

WhatsApp Image 2024-08-14 at 17.13.07_bfbe89a1.jpg
Amesema, Tume ya Madini inaandaa mwongozo na masharti ya namna bora ya kuomba maeneo hayo kwa wawekezaji wenye nia na uwezo wa kuwekeza kwenye Sekta ya Madini.

Mavunde amesema kuwa, Wizara kupitia Tume ya Madini imeendelea kutoa hati za makosa kwa wamiliki wa leseni kutokana na ukiukwaji wa masharti ya leseni zao kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura 123 ambapo jumla ya leseni 110 za utafutaji madini, leseni 13 za uchimbaji wa kati na leseni 2 za uyeyushaji wa madini zilipewa hati ya makosa.

Awali, akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Bunge Nishati na Madini, Kaimu Katibu Mtendaji Tume ya Madini Mhandisi Ramadhani Lwambo amesema kwa kipindi cha Oktoba 2023 hadi Julai 2024 , Tume ya Madini ilitoa leseni moja ya uchimbaji mkubwa , leseni 20 za uchimbaji wa kati na leseni 7974 za uchimbaji mdogo katika maeneo mbalimbali nchini.
WhatsApp Image 2024-08-14 at 17.13.03_d1c84e65.jpg
 
Maombi 2648 ya utafutaji wa madini yafutwa katika kipindi cha kuanzia mwezi Oktoba 2023 hadi Julai 2024 kutokana na kutokidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura 123.
Nyuso zao ukizitazama utajua tu, kutokidhi vigezo ni pamoja na kutotoa mlungura
 
Hawa jamaa wa tume ya madini wanapenda sana mambo ya mkono mrefu yaani kuna leseni wametoa kipind cha mwezi July na August mwaka huu wakati wanatuambia eti board haipo hadi iundwe nyingine nauliza hawa walopewa leseni wamepata kupitia board gani?????Acheni double standard kuona sie wengine ni majuha tupeni leseni na sie au tuelezeni hawa waliopata leseni wao ni special!!!Mavunde hii suala sio !!!!!!!!!!!!!!!!!!Shame on this!!!!!
 
Maombi 2648 ya utafutaji wa madini yafutwa katika kipindi cha kuanzia mwezi Oktoba 2023 hadi Julai 2024 kutokana na kutokidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura 123.

Hayo yamesemwa leo Agosti 14 , 2024 na Waziri wa Madini Anthony Mavunde wakati akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Bunge Nishati na Madini kuhusu hali ya Usimamizi na Uendelezaji wa Leseni zilizotolewa kwa ajili ya Utafutaji na Uchimbaji wa Madini.

Mavunde amesema kuwa maombi hayo yalifutwa baada ya kubainika kuwa, waombaji hawakuwa na nia ya kupatiwa leseni za utafutaji madini na badala yake walikuwa wameyashikilia na kuhodhi maeneo hayo na hivyo kuwanyima fursa wenye nia ya kuyaendeleza.
Amesema, Tume ya Madini inaandaa mwongozo na masharti ya namna bora ya kuomba maeneo hayo kwa wawekezaji wenye nia na uwezo wa kuwekeza kwenye Sekta ya Madini.

Mavunde amesema kuwa, Wizara kupitia Tume ya Madini imeendelea kutoa hati za makosa kwa wamiliki wa leseni kutokana na ukiukwaji wa masharti ya leseni zao kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura 123 ambapo jumla ya leseni 110 za utafutaji madini, leseni 13 za uchimbaji wa kati na leseni 2 za uyeyushaji wa madini zilipewa hati ya makosa.

Awali, akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Bunge Nishati na Madini, Kaimu Katibu Mtendaji Tume ya Madini Mhandisi Ramadhani Lwambo amesema kwa kipindi cha Oktoba 2023 hadi Julai 2024 , Tume ya Madini ilitoa leseni moja ya uchimbaji mkubwa , leseni 20 za uchimbaji wa kati na leseni 7974 za uchimbaji mdogo katika maeneo mbalimbali nchini.
POLE kwa waliofutiwa leseni.
 
Huyu mzee kashika kichwa na Kopo la maji kaliweka kata funua Yani kichwa chini miguu juu! Itakuwa report imemvuruga
 
Habari njema sana hii kwa tuliopo kwenye hii sekta. Kuna Wazee wanamiliki acres kibao walizolipia application fees tu afu wanataka waziuze 500M. Haiwezekani.
 
Habari njema sana hii kwa tuliopo kwenye hii sekta. Kuna Wazee wanamiliki acres kibao walizolipia application fees tu afu wanataka waziuze 500M. Haiwezekani.
Hii itaumiza pia wachimbaji wadogo
 
Hii itaumiza pia wachimbaji wadogo

Hapana. Tatizo wachimbaji wadogo hawapendi kufuata taratibu kwa kigezo wao ni wazawa. Hata wazawa wengine wenye uwezo wa kuendeleza maeneo hawawezi.

Watu wanachukua coordinates wanakata leseni sio kwa kigezo cha kuchimba au kuendeleza bali kuhodhi ili wafanye udalali. Wanakata PML kwa bei ndogo sana hata laki5 haifiki ili tu mtu akijitokeza wauze 500M. Hii sio sawa.
 
Back
Top Bottom