Serikali yafuta Vikosi Kazi vya ukusanyaji mapato TRA

Serikali yafuta Vikosi Kazi vya ukusanyaji mapato TRA

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1668502614553.png


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania, Uledi Mussa amesema Vikosi hivyo vimeondolewa ili kuhakikisha kunakuwa na Haki katika ukusanyaji mapato nchini.

Amesema TRA inataka watu walipe Kodi bila Shuruti na hivyo Mamlaka hiyo imeagiza Maofisa wake wakusanye kodi bila matumizi yoyote ya nguvu.

Utaratibu wa Ukusanyaji Kodi kwa kutumia Vikosi Kazi ulilalamikiwa kuwa na ukiukaji mkubwa wa Sheria na Haki za Binadamu katika utekelezaji wake.

====================

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Uledi Mussa amesema kwa sasa wanakusanya kodi kutoka kwa wafanyabiashara bila kutumia mabavu.

Amesema kitengo cha 'task force' kilichokuwapo huko nyuma na kutumika kukusanya kodi wamekiondoa.

Mussa amesema hayo leo Jumanne Novemba 15, 2022 katika kikao baina ya TRA na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) jijini Dar es Salaam.

"Kwa sasa tunakusanya mapato bila mabavu. Waachane kabisa kabisa na matumizi ya manavu. Tunataka walipa kodi wajisikie vizuri kabisa. Hatuna tena Taska Force (kikosi kazi)," amesema

Mwenyekiti huyo amesema,"walipa kodi, tunawaangalia kwa macho mawili kuhakikisha wanaendelea kufanya biashara zao ili wawe walipa kodi siku zijazo."

Amesema hatua hiyo imewezesha ukusanyaji wa mapato umeongezeka akitolea mfano mapato ya Septemba yamevuka lengo badala ya kukusanya Sh6.2 trilioni wamekusanya Sh6.3 trillion.

Katika kikao hicho, wahariri wameuliza maswali mbalimbali likiwemo umuhimu wa TRA kuwaomba radhi wale wote walioumizwa na kikosi kazi hicho.

Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipa Kodi, wa TRA, Richard Kayombo amesema,"kuna mengi yamefanyika nyuma ya pazia kuhakikisha yanakaa sawa. Kwa wale tuliokaa nao mmoja mmoja tumewezesha mambo kwenda sawa."

Amesema mazingira ya sasa na huko nyuma yalikuwa tofauti hivyo wanajitahidi kuweka mazingira rafiki zaidi kwa kila mmoja kufurahia anachokifanya.

Naye Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile amewapongeza TRA kwa kuamua kukutana na wahariri kwani ni inaingesha hali ya kushirikiana ili kuhakikisha dhamira ya elimu kwa wananchi kuhusu kulipa kodi inafanikiwa.

"Pamoja na malalamiko yote, tunawapongeza sana, kwa sasa hatujaona makufuri yakifungwa kwa wafanyabiashara, hili ni jambo zuri," amesema

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa TEF, Bakari Machumu amepongeza jitihada zinazofanywa za kuweka mazingira mazuri ya kulipa kodi hilo linatia moyo.

Machumu ambaye pia ni Mkurugenzi Mtebdaji wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) amesema, kila mmoja akiwa na uelewa wa pamoja na shirikishi hata mapato yataongezeka.
 
SERIKALI iajiri watu wa kutosha! wenye kuona leo na kesho ya mfanyabiashara sio mambo ya kukimbizana
 
#ZILIZOTUFIKIA: Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Uledi Mussa amesema hakuna tena vikosi kazi katika ukusanyaji mapato nchini.
-
Musa amewaambia Wahariri jijini Dar es Salaam kuwa TRA inataka watu walipe kodi bila shuruti, na wamewaagiza maofisa wakusanye kodi bila matumizi ya nguvu.
 
Mwandishi Wetu, Mwananchi

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Uledi Mussa amesema kwa sasa wanakusanya kodi kutoka kwa wafanyabiashara bila kutumia mabavu.

Amesema kitengo cha 'task force' kilichokuwapo huko nyuma na kutumika kukusanya kodi wamekiondoa.

Mussa amesema hayo leo Jumanne Novemba 15, 2022 katika kikao baina ya TRA na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) jijini Dar es Salaam.

"Kwa sasa tunakusanya mapato bila mabavu. Waachane kabisa kabisa na matumizi ya manavu. Tunataka walipa kodi wajisikie vizuri kabisa. Hatuna tena Taska Force (kikosi kazi)," amesema

Mwenyekiti huyo amesema,"walipa kodi, tunawaangalia kwa macho mawili kuhakikisha wanaendelea kufanya biashara zao ili wawe walipa kodi siku zijazo."

Amesema hatua hiyo imewezesha ukusanyaji wa mapato umeongezeka akitolea mfano mapato ya Septemba yamevuka lengo badala ya kukusanya Sh6.2 trilioni wamekusanya Sh6.3 trillion.

Katika kikao hicho, wahariri wameuliza maswali mbalimbali likiwemo umuhimu wa TRA kuwaomba radhi wale wote walioumizwa na kikosi kazi hicho.

Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipa Kodi, wa TRA, Richard Kayombo amesema,"kuna mengi yamefanyika nyuma ya pazia kuhakikisha yanakaa sawa. Kwa wale tuliokaa nao mmoja mmoja tumewezesha mambo kwenda sawa."

Amesema mazingira ya sasa na huko nyuma yalikuwa tofauti hivyo wanajitahidi kuweka mazingira rafiki zaidi kwa kila mmoja kufurahia anachokifanya.

Naye Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile amewapongeza TRA kwa kuamua kukutana na wahariri kwani ni inaingesha hali ya kushirikiana ili kuhakikisha dhamira ya elimu kwa wananchi kuhusu kulipa kodi inafanikiwa.

"Pamoja na malalamiko yote, tunawapongeza sana, kwa sasa hatujaona makufuri yakifungwa kwa wafanyabiashara, hili ni jambo zuri," amesema

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa TEF, Bakari Machumu amepongeza jitihada zinazofanywa za kuweka mazingira mazuri ya kulipa kodi hilo linatia moyo.

Machumu ambaye pia ni Mkurugenzi Mtebdaji wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) amesema, kila mmoja akiwa na uelewa wa pamoja na shirikishi hata mapato yataongezeka.

Mwananchi
 
Huu Ni ujinga sasa sijui watu watalipaje Kodi kwa hiari wakati hawana elimu ya Kodi na pia wanasikia Pesa yao inaliwa..

Na hakika hata TRA huwa wakienda madukani kununua hawadai risiti hasa wakipunguziwa hata akidai kinachoandikwa kwenye risiti Ni tofauti na thamani ya Mali.
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Huu Ni ujinga sasa sijui watu watalipaje Kodi kwa hiari wakati hawana elimu ya Kodi na pia wanasikia Pesa yao inaliwa..

Na hakika hata TRA huwa wakienda madukani kununua hawadai risiti hasa wakipunguziwa hata akidai kinachoandikwa kwenye risiti Ni tofauti na thamani ya Mali.
Hivyo vikosi kazi viligeuka vikosi vya uporaji, bora vifutwe kabisa, kuna njia za kistaarabu na kisheria zifuatwe, yule asiyelipa adhabu zipo.
 
Huu Ni ujinga sasa sijui watu watalipaje Kodi kwa hiari wakati hawana elimu ya Kodi na pia wanasikia Pesa yao inaliwa..

Na hakika hata TRA huwa wakienda madukani kununua hawadai risiti hasa wakipunguziwa hata akidai kinachoandikwa kwenye risiti Ni tofauti na thamani ya Mali.
Acha kuandika ukiwa usingizini/ unaota
 
Bado EFD inatakiwa iondolewe kwa wafanyabiashara wadogo ibaki kwa wafanyabiashara wakubwa tuu
 
Huu Ni ujinga sasa sijui watu watalipaje Kodi kwa hiari wakati hawana elimu ya Kodi na pia wanasikia Pesa yao inaliwa..

Na hakika hata TRA huwa wakienda madukani kununua hawadai risiti hasa wakipunguziwa hata akidai kinachoandikwa kwenye risiti Ni tofauti na thamani ya Mali.
Tuliza kijambio wewe zuzu wa ccm
 
Haijawahi kutokea mfanyabiashara alipe Kodi bila kukumbushwa ukitulia ofsini na yy anauchuna kmyaa,analeta siasa tu baada ya muda atarudisha kmyaa kmyaa
 
SERIKALI iajiri watu wa kutosha! wenye kuona leo na kesho ya mfanyabiashara sio mambo ya kukimbizana
Endeleeni kudanganya watu wakati mapato yameshuka kwa kiasi kikubwa kuliko hata awamu ya nne! Leo Halmashauri zote chini ya Tamisemi hazijapokea fedha kutoka BOT bila maelezo ya kina kwanini, matokeo yake ni kusimama kwa utekelezaji wa shughuli mbalimbali chini ya Halmasahuri hizo.

Tangia enzi ya Kaizari kodi haijawahi kukusanywa kirafiki ni lazima nguvu ya kadiri itumike vinginevyo utashi wa kulipa kodi hakunaga!

Mtu aniambie duka gani au mfanyabiashara gani anatoa receipt za EFD achilia mbali zilizotoka kwenye mashine fake? Ni wafanyabiashara wangapi wanatoa EFD receipt moja ya mauzo kwa mizigo ya wiki nzima? Ni wafanyabiashara wangapi wanakusanya na kuuza EFD receipts kwa wafanyabiashara wasafirishie mizigo kutoka sehemu moja kwenda nyingine?
Zipo mbinu nyingine nyingi za ukwepaji kodi na ambazo wafanyabiashara wanazohararisha kwa madai kwamba huwezi kulipa kodi ukapata faida yoyote kwenye biashara kutokana na rushwa na tozo zingine zinazoghubika sekta hiyo.
Hata hivyo utaratibu huu wa kuondoa taskforce iliyokuwa inakula rushwa lakini fungu la tajiri linahakikishiwa kufikishwa sasa wanakula wenyewe hata thumni haiendi kwa tajiri kwa sababu wanasema tumekwenda kudai tumekuta hana pesa tumemuachia ajichange atakuja kulipa!
 
Hata hivyo utaratibu huu wa kuondoa taskforce iliyokuwa inakula rushwa lakini fungu la tajiri linahakikishiwa kufikishwa sasa wanakula wenyewe hata thumni haiendi kwa tajiri kwa sababu wanasema tumekwenda kudai tumekuta hana pesa tumemuachia ajichange atakuja kulipa!
Naunga mkono Hoja
 
"Kwa sasa tunakusanya mapato bila mabavu. Waachane kabisa kabisa na matumizi ya manavu. Tunataka walipa kodi wajisikie vizuri kabisa. Hatuna tena Taska Force (kikosi kazi)," amesema
Ni kweli amesema hivyo!!?
 
Back
Top Bottom