Serikali yaombwa kukipiga tafu kiwanda cha Mkulanzi

Serikali yaombwa kukipiga tafu kiwanda cha Mkulanzi

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Serikali imeombwa kukiongezea nguvu Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi ili uzalishaji wake ufike tani 75,000 kwa mwaka kutoka makadirio ya tani 50,000 za sasa.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mkulazi, Dk Hildelitha Msita wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, wilayani Kilosa mkoani Morogoro leo Jumatano Agosti 7, 2024.

“Mheshimiwa Rais kiwanda hiki kimejengwa kwa teknolojia ya hali ya juu kama ulivyoelekezwa na mtendaji mkuu wa kampuni, kiwanda hiki kina uwezo wa kuchakata tani 500,000 (miwa) kwa maana tunaweza tukapata tani 50,000 za sukari kwa mwaka lakini pia, ikiongezwa gharama kidogo tunaweza kufika tani 75,000 za sukari kwa mwaka.

“Pia, mheshimiwa Rais tunaomba uendelee kutoa fedha zaidi kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa barabara kwenye mashamba ya wakulima wadogo wadogo ambayo itaweza kufikisha miwa katika kiwanda chetu,” amesema Dk Msita.


 
I will be the last person to believe that...mbona private sector inafanya kwa kasi na kuongezea uzalishaji?

Hiki kiwanda toka kianze kujengwa kimeshaanza uzalishaji? Sokoni wanatumia brand name gani?
 
Hawa watu kila wakati wanafikiria kuiba tu! Sasa wao si waanze kuzalisha wakiuza na kupata faida wataongeza uzalishaji, Mbona makampuni binafsi hayaombi hela serikalini ila wanatanua uwezo wao kidogo kidogo!
 

Serikali imeombwa kukiongezea nguvu Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi ili uzalishaji wake ufike tani 75,000 kwa mwaka kutoka makadirio ya tani 50,000 za sasa.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mkulazi, Dk Hildelitha Msita wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, wilayani Kilosa mkoani Morogoro leo Jumatano Agosti 7, 2024.

“Mheshimiwa Rais kiwanda hiki kimejengwa kwa teknolojia ya hali ya juu kama ulivyoelekezwa na mtendaji mkuu wa kampuni, kiwanda hiki kina uwezo wa kuchakata tani 500,000 (miwa) kwa maana tunaweza tukapata tani 50,000 za sukari kwa mwaka lakini pia, ikiongezwa gharama kidogo tunaweza kufika tani 75,000 za sukari kwa mwaka.

“Pia, mheshimiwa Rais tunaomba uendelee kutoa fedha zaidi kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa barabara kwenye mashamba ya wakulima wadogo wadogo ambayo itaweza kufikisha miwa katika kiwanda chetu,” amesema Dk Msita.


Je, kiwanda hicho ni Cha nani??
Mmiliki wake ni Nani???

Nasikia sikia kwamba 'mzee wa msoga' ndiye Mmiliki wa kiwanda hicho. Kama taarifa hii ina ukweli, Je, kwa nini Basi huyo M/kiti wa Bodi ya Kiwanda hicho anataka Serikali iweke fedha zake hapo??
 
wazo la kiwanda hiki liliasisiwa na dr ramadhani dau likaonekana la kipuuzi sana, leo kila mtu anapiga makofi
 
Back
Top Bottom