Serikali yapiga marufuku mazao ya uhandisijeni(GMOs) nchini

Serikali yapiga marufuku mazao ya uhandisijeni(GMOs) nchini

You seriously need to see a doctor, rising sea levels, global warming, is that all?
Do us a favor stop using the internet because you are contributing to the same thing you fight against.

Got no time to waste with you man! just do your thing. I'm off.
This is my last reply on this bs.

Let me ask you this, which one you would rather choose, Saving the World or Destroying it?

You really typing BS you know? have you imagined how it will be if we depend on these seeds rather than what the nature has to offer? and let me ask you one thing, why GMO and not natural ones? give me a good reason if you make sense
 
Nov 21, 2018

KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO AITAKA TARI KUSITISHA MAJARIBIO YA GMO

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma

Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo, Mhandisi Mathew Mtigumwe leo tarehe 21 Novemba 2018 ameiagiza Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kusitisha mara moja utafiti na majaribio ya uhandisijeni (Genetic Modified Organisms(GMO) yanayofanyika kwenye vituo vyake vya utafiti.

Aidha, Katibu Mkuu ameilekeza Taasisi hiyo ya TARI kuwa mabaki yote ya majaribio ya Uhandisijeni yateketezwe mara moja.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Taasisi hiyo kuanza kutoa matokeo ya utafiti bila kupata idhini ya serikali.

Siku za hivi karibuni Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kupitia kituo cha Makutupora imekuwa inaalika watu mbalimbali kwenda kuona matokeo ya utafiti wakati serikali haijaruhusu matumizi ya uhandisijeni nchini.

For the English Audience
The Tanzanian government has ordered The Agricultural Research Institute(TARI) to stop all Genetic Engineering (Genetic Modified Organisms-GMO) research and testing in all its centers.

This is to be followed by destroying all of what remains of the GMO testing materials.

Recently the Institute without the consent of the Government, had started to disseminate and exhibit research results at one of its centers.


Zaidi, soma >> Nimeona wabunge wakishangilia ujio wa mbegu za GMO. Je, hawajui madhara yake kwa binadamu? - JamiiForums


Kwa wale wageni kwenye swala la GMOs,mada ifuatayo itasaidia kwa kiasi fulani kuonyesha hatari kubwa iliyopo mbele yetu.

Barua ya wazi kwa Rais Joseph Pombe Magufuli kuhusu GMOs.

areafiftyone
JF-Expert Member

Nov 5, 2018.

Mazao ya uhandisijeni(GMOs) ni janga la dunia,pamoja na sisi tulioko JamiiForums.
Mwenzetu Dr Richard Mbunda ambaye anakerwa na GMOs pamoja na mimi, labda na wengine,
amemuandikia Rais barua ya wazi akieleza kwa kina ubaya wa GMOs na kueleza wazi kwa nini anaamini GMOs kama zitaruhusiwa kulimwa nchini,zitaleta adhari kubwa kwa mazingira yetu,uchumi wetu, hasa wa wakulima wadogo wadogo na afya za Watanzania.Kwa vile janga la GMOs ni letu sote,tusome barua ya Dr.Richard Mbunda kwa makini halafu totoe mawazo yetu kama JF.Naomba baada ya hilo angalizo, sasa niombe moderators wasitoe uzi huu, ili watu waweze kutoa mawazo yao.Michango itakayotolewa hapa ina maana kubwa kwa kizazi hiki na vizazi vingi vijavyo.


Barua ya Wazi kwa Rais wa Tanzania: Je, GMOs ni Sera ya Serikali?

Na Dkt. Richard Mbunda (UDSM)

Mheshimiwa Rais,

Heri ya siku ya kuzaliwa!

Kwa heshima na taadhima, niruhusu mimi mtoto wa mkulima mdogo na mwananchi wa nchi yetu tukufu nikusalimu. Hali yangu mimi na wanafamilia wenzangu, ambao ni wakulima wadogo nchini, si njema kabisa. Mheshimiwa Rais, kama ujuavyo, sisi ni takribani asilimia zaidi ya 70 ya wananchi wote wa Tanzania, na naamini kuna ndugu zako wa damu ambao ni sehemu ya jamii hii ya watanzania.

Ukulima mdogo ndiyo uhalisia wetu. Hatuwezi kuukataa kwa sasa, japo wengi tuna matumaini ya kupiga hatua, kama serikali itatuwekea misingi thabiti. Lakini hali yetu ni ile, Waswahili wanasema ‘bora ya jana kuliko leo.’ Mikakati ya kumkwamua mkulima mdogo nitaieleza katika kitabu changu, lakini kwa leo niruhusu tu nikuulize swali la kisera.

Mheshimiwa Rais, tarehe 28 Septemba, 2018 Jijini Geneva, Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ilipitisha Azimio la Haki za Wakulima Wadogo. Azimio hili ni ushindi kwa wakulima wadogo duniani dhidi ya Makampuni hodhi katika sekta ya kilimo katika mapambano yaliyochukua zaidi ya miaka 17. Azimio hili linazungumzia haki za ARDHI, MBEGU, BAIOANUAI (Biodiversity) na SOKO LA NDANI LISINAJISIWE NA BIDHAA KUTOKA NJE.

Kimsingi haki hizi zinaendana na Uhuru wa Chakula (Food Sovereignty) kwa nchi maskini, ambao ndiyo uhuru pekee tuliobaki nao. Kinachonishangaza Mheshimiwa Rais, ni kuwa, pamoja na kuwa na idadi kubwa ya wakulima wadogo nchini, Tanzania haikuwakilishwa katika Azimio hili muhimu. Jumla ya nchi 34 zilikubali Azimio, nchi 11 zilikaa(abstain) na kama ilivyotegemewa, nchi zilizoendelea zilipinga Azimio hili. Mheshimiwa Rais, tulipitwa au hatujali? Namshukuru Mungu wa wanyonge, Azimio limepita.

Lakini Mheshimiwa Rais, mienendo ya Serikali inatupa mashaka makubwa zaidi sisi familia ya wakulima wadogo. Naliongea hili kwa ujasiri kwa kuwa nimekulia kilimo na naishi na wakulima wadogo. Hata utafiti wangu wa uzamivu uliwalenga wakulima wadogo na unahusu Uhuru wa Chakula Tanzania.

Mheshimiwa Rais, serikali imekuwa ikipigia chapuo teknolojia ya uhandisijeni wa mazao ya GMOs nchini. Tumeliona hilo katika Programu ya ASDP II uliyoizindua hivi karibuni, ambayo inatamka wazi mwelekeo wa kilimo chetu kwa matumizi ya GMOs, siyo tu katika mimea, bali hata wanyama (ikanifanya niwaze majaliwa ya ng’ombe za rafiki zangu Wamasai). Angalau basi tukusikie kwa maneno yako, je, wewe ni shabiki wa teknolojia hiyo na kwamba ni mdau wa mradi ya GMOs katika utafiti unaoendelea Makutupora, ambayo sasa inahalalishwa hapa nchini kupitia vyombo vya habari?

Barua yafaa iwe fupi ili isomeke kwa haraka na kueleweka kirahisi. Hivyo, Mheshimiwa Rais, nitaandika kwa uchache kuhusu sababu kwa nini Tanzania haihitaji GMOs. Lakini ninazo makala ndefu za kitaaluma zinazohusu jambo hili.

Sababu mojawapo ya kukataliwa GMOs inatokana na athari zake katika mazingira. Kwa mfano, katika utafiti uliofanywa na Mwanazuoni John Paul na kuchapishwa mwaka huu wa 2018, ikiwa na kichwa Genetically Modified Organisms (GMOs) as Invasive Species unaonesha kuwa GMOs ni viumbe vamizi. Huharibu mazao asilia, mimea mingine, wanyama na kuleta athari katika mazingira ya viumbe hai.

Hata katika elimu ndogo ya Kilimo tuliyojifunza sekondari, Mheshimiwa Rais, mahindi huzaa kwa uchavushaji. Kama mahindi ya GMOs na ya kawaida yatapandwa pamoja tutegemee nini? Kimsingi mahindi ya mbegu zisizo za GMOs yakiingiliana na ya GMOs yatapotea na kutuletea balaa kubwa la utegemezi huko mbeleni. Izingatiwe kuwa mbegu za GMOs hazirudiwi kupandwa zikatoa mazao.

Mheshimiwa Rais, napenda kujua kama hayo majaribio ya Makutupora yanajibu wasiwasi huu. Kwamba mbegu zao za GMOs hazitaathiri mbegu zetu, mimea mingine na mazingira kwa ujumla! Au ni utafiti unaoonesha tu kuwa GMOs zitastawi nchini? Mheshimiwa Rais unisamehe kwa kusema hili, hata bangi, ule mmea tunaoupiga vita, bado unastawi katika nchi yetu tukufu, tena vizuri mno.

Kupotea kwa mbegu zetu [kutokana na kuingiliana na mbegu za GMOs] kutatufanya tuwe watumwa wa makampuni ya mbegu. Mheshimiwa Rais, naamini umefuatilia habari kuhusu kampuni ya Monsanto, ambayo sasa imenunuliwa na kampuni ya Bayer ya Ujerumani kwa zaidi ya shilingi trilion 120 (USD 62 bn). Monsanto imekuwa ikipigwa vita hasa Amerika ya Kusini kwa namna ilivyotaka kuwafanya watu wake watumwa wa chakula. Pale ambapo tutapoteza mbegu zetu za asili, au tulizoziendeleza muda mrefu kupitia taasisi zetu za utafiti, tutakuwa tumekubali kuwa mateka.

Mheshimiwa Rais, wewe umekuwa ukipinga ubeberu kwa nguvu zako zote, na nisingependa hili la utumwa wa mbegu litokee katika utawala wako. Afrika Kusini, ambako waliruhusu GMOs tangu miaka ya 90, sasa zaidi ya asilimia 90 ya mahindi ni GMOs na wakulima wanalazimika kulipa ziada ya ada ya teknolojia kwa Monsanto. Pamoja na kubeparisha kilimo chao, bado Afrika Kusini hawajaweza kutokomeza njaa.

Suala la utamaduni wa chakula ni muhimu pia liongelewe katika muktadha huu. Kuna ladha, harufu nzuri na uasili wa chakula. Kama ujuavyo, Mheshimiwa Rais, hizi ni sifa pekee zinazotofautisha chakula chetu. Na tunapaswa kuvitunza vyakula hivi kwa choyo kubwa - hasa kwa kuwa sisi ni kitovu cha utalii Afrika.

Tukisoma baadhi ya makabrasha na shuhuda za wageni, tunaona watalii wanakizungumzia chakula chetu katika namna ya sifa ya pekee. Mheshimiwa Rais, pengine unakumbuka kuwa, mmoja kati ya watetezi wa GMOs Robert Paarlberg aliwahi kusema mwaka 2009 kuwa “chakula kilichozalishwa kiasili (organically) kina ladha na harufu ya kuvutia zaidi kuliko vyakula vya GMOs ndiyo maana nchi za Ulaya hazitaki GMOs" lakini "masikini wa Afrika hawapaswi kuwa na uchaguzi” Je, ni kweli tumefika sehemu ambayo hatupaswi kuwa na uchaguzi kwa kuwa sisi ni maskini?

Mheshimiwa Rais, katika makala yenye kichwa "No Scientific Consensus on GMO Safety," iliyochapisha wa wanasayansi 15 kwa pamoja katika Jarida la Environmental Sciences Europe mwaka 2015, tunaelezwa kwamba japo kumekuwa na jitihada za kuuaminisha ulimwengu kuwa GMOs ni salama kwa afya, lakini kimsingi hakujawa na muafaka wa usalama wa GMOs. Na kuna baadhi ya tafiti zilizoenda mbele kueleza kuwa GMOs zina madhara kiafya. Baadhi ya madhara ya afya yanayotajwa ni pamoja na uzio na saratani. Je, utafiti unaofanyika Makutupora unalenga kuleta majibu ya wasiwasi wa madhara ya afya yatokanayo na GMOs?

Monsanto imeshtakiwa zaidi ya mara hamsini huko Marekani na hivi karibuni ilipatikana na hatia, wananchi wakiilalamikia bidhaa zao kuwaleatea saratani. Kuhusu chakula cha GMO, jibu la kampuni hiyo limekuwa hilo hilo kuwa hawalazimiki kisheria kudhibitisha kuwa vyakula vyao havina madhara. Wanaojiita wanasayansi wetu nchini hawatuambii ukweli, labda kwa maslahi yao binafsi. Lakini katika majadiliano tuliyofanya HakiArdhi hivi karibuni, mmoja wa wanasayansi hao, baada ya kubanwa na wakulima, alikiri kuwa uangalifu unahitajika hasa katika mimea iliyobadilishwa kuzalisha sumu ili kuua wadudu.

Mheshimiwa Rais, Takwimu za Wizara ya Kilimo zinaonesha kuwa Tanzania bado hatujafikia hata asilimia 30 ya matumizi ya mbegu bora, mbolea na viuatilifu. Bado tumekuwa tukizalisha zaidi ya asilimia 120 ya chakula kinachohitajika nchini. Wiki tatu zilizopita nilikuwa Mkoa wa Rukwa (Sumbawanga) na nilikutana na Wazalishaji wanaolalamikia soko la mahindi na siyo changamoto za uzalishaji. Tena kuna waliovuna mahindi ya kutosha bila hata kutumia mbolea.

Lakini watu wa GMOs wanatuletea taarifa kuwa kuna uzalishaji mdogo sana na mahindi yanashambuliwa sana na wadudu. Kimsingi wanatangaza Hali ya Hatari (National Emergency) kwa jinsi wanavyotuonesha wadudu wala mahindi katika video zao. Mheshimiwa Rais, ni kweli tumefikia huko? Kama ni kweli mbona hujatutangazia hali ya hatari ili basi GMOs tuipokee kama hatua yetu ya kupunguza kifo cha haraka? Na kama siyo kweli, kwa nini tunalazimishwa kuruka kutoka kutumia mbegu za asili kwa asilimia 80 za sasa hadi GMOs, teknolojia ya juu kabisa wakati hatujaweza kuvuna tija itokanayo na mbegu bora za OPVs na Hybrid?

Kuna agenda gani hapo? Tunakimbilia wapi? Tunapitwa na nini?

Mheshimiwa Rais, sipendi nikuchose sana. Naomba niulize swali moja la mwisho. Ubora tulio nao kama nchi ukilinganisha na nchi zingine (Comparative Advantage) wanaouongelea wachumi au kile wasomi wa fani ya Biashara wanachokiiita eneo la ubora (niche) wetu lipo katika nini? Sidhani kama tunaweza kushindana na Marekani katika kuzalisha mahindi ya GMOs, chakula chenye unyanyapaa duniani kote. Sisi tunapaswa kuwa msingi wa chakula salama Afrika Mashariki na kwingineko duniani. Wakulima wetu wanapaswa kuwa msingi wa kuzalisha chakula hiki na kunufaika kama ilivyo sasa, ambapo soko bado si la uhakika.

Katika utafiti wangu nilitembelea vituo vya utafiti wa kilimo. Nikiri kuwa ni taasisi nyeti na zina wataalam (japo wametelekezwa) wanaoweza kutusaidia katika kuboresha mbegu zetu za asili kama wakiwezeshwa. Sote tunajua mbegu bora siyo lazima ziwe za GMO.

Mheshimiwa Rais, tukumbuke kuwa wakati wa Utawala wa Rais Dkt. Jakaya Kikwete, mradi wa GMO wa WEMA haukuanza nchini japo ulipaswa kuanza 2008. Hii ilitokana na kifungu kinachohusiana na dhamana ya uharibifu kijulikanacho kwa Kiingereza kama ‘strict liability’ kilichopo katika kanuni zetu za usalama wa viumbe na uhai (Biosafety). Kifungu hiki kilisema mtu atakeyeingiza GMOs nchini atawajibika moja kwa moja kwa madhara yoyote yatakayotokana na GMOs kiafya, kimazingira na kiuchumi.

Hiki kifungu kiliwachelewesha watu hawa wa WEMA kuanza utafiti mpaka mwaka 2016 Serikali ilipolegeza masharti na kuweka kifungu kinachosema ‘strict liability’haitatumika katika utafiti. Kama GMOs ni kitu chema kama WEMA unavyodai na ni ukombozi wetu, waliogopa nini kuanza 2008 hadi wakashawishi kanuni zibadilike? Hata sasa wanadai sheria zetu zinawabana wanataka tulegeze zaidi watuletee balaa tushindwe pa kuwabana.

Walaji wa chakula kinacholimwa na wakulima wadogo hawapo salama pia. Muda si mrefu tutaanza kuona maduka makubwa (supermarkets) za vyakula vya asili (organic food) ambavyo watu wa kada ya juu tu ndio pekee watamudu kununua. Wameshaanza na madogo madogo. Tunaendelea kutengeneza matabaka kwa maslahi ya mwekezaji.

Mheshimiwa Rais, huenda barua hii haitakupendeza. Najua pia barua hii haitawapendeza wadau na watunga sera wanaopigania GMOs izidi kutamalaki nchini. Hakika itaichukiza kampuni husika inayowekeza katika mradi wa WEMA huko Makutupora.

Wanatudhihaki kuwa sisi tunapinga sayansi. Lakini ni sayansi zipi tumezipinga hapa nchini? Kama alivyowahi kusema mwanazuoni nguli Karl Polanyi mwaka 1944, hatuwezi kuiruhusu teknolojia ya kinyonyaji na inayokusudia kunufaika na majanga ya watu itamalaki.

Mheshimiwa Rais, nakushukuru kwa kusoma hii barua. Hatimaye nimetimiza wajibu wangu. Nimesema ukweli na sina haja ya kujificha.
All said, all written and all researched, ni ukweli kwamba matumizi ya mbegu za aina hii ya GMO, ndiyo mwanzo wa kuua kilimo asilia na mwanzo mpya wa UKOLONI MAMBO LEO katika KILIMO. Ukisha ingizwa kwenye ukoloni mambo leo katika kilimo chako unadhani ni nini kitafuata, kama siyo kuwa TEGEMEZI KWA WAKOLONI katika mahitaji yako yote ikiwa ni pamoja na CHAKULA? Ukitegemea hata chakula kutoka kwa mtu mwingine, basi ujue wewe na familia yako MMEKWISHA! Ndicho wanachotaka kutufanyia hawa WAKOLONI kwa kutumia mlango wa sayansi na teknolojia na utafiti uchwara through watafiti na "wasomi" wachache wenye uchu wa fedha na "njaa kali". Hii hoja ilikwisha kataliwa na serikali miaka mingi na ikasahaurika, mara ghafla inazushwa na hawa "wasomi na watafiti uchwara" kwa kushirikiana wabunge na viongozi wachache kwa maslahi yao wenyewe.

Hiyo hoja ya kuwa wabunge walishangilia si hoja, jiulize na fanya utafiti kidogo, utaona composition ya hao wabunge walioshangilia na kupiga makofi on this GMO issue. Kwa kweli ni WALE WALE TU! Kwa ufupi, matumizi na utegemezi wa hizi mbegu zinazotokana na GMO teknolojia, ndiyo mwanzo wa kufa kwa njaa kwani wenye mbegu zao wanaweza kuamua wasikuuzie aidha hizo mbegu au hiyo teknolojia! Under such a SITUATION, UNAFANYAJE KUTOKA? Nimalizie kwa kusema kuwa uamuzi huu wa Serikali hii ni wa ujasiri na wenye lengo la kuinusuru nchi yetu na hili JANGA LA UKOLONI MAMBO LEO NA NJAA YA KUDUMU. Mbinu hizo ZISHINDWE NA MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
labda tafsiri ya gmo watu hwajailelewa vizuri , mbegu organic ni zile za kienyeji tuu. Hizi zote zinazozalishwa na zilizopo madukani na tunazohamasishwa tulime kisasa na nyingi zipo kwa majina ya F.1 zote ni geneticaly modfined ( G.M.O) I stand to be corrected
 
labda tafsiri ya gmo watu hwajailelewa vizuri , mbegu organic ni zile za kienyeji tuu. Hizi zote zinazozalishwa na zilizopo madukani na tunazohamasishwa tulime kisasa na nyingi zipo kwa majina ya F.1 zote ni geneticaly modfined ( G.M.O) I stand to be corrected
Unaweza kuwa sahihi kidogo, lakini hizi za GENETICALLY MODIFIED ORGANISMS AU GMO ni kama jina lilivyo ni mbegu zinazotokana na ufundi wa kitaalamu na kimaabra kisayansi zaidi kutokana na "genes" mbalimbali kisayansi na kisha zinakuwa "modified" kadri wapendavyo hao wataalamu ili to fit their needs and requirements. Wanaweza kuchukua genes za kuku na kuzi modify wapendavyo na kutoa kuku "mwenye ubora zaidi"! Lakini wewe uliye mnunua huyo modified kuku huwezi kumuendeleza zaidi ya labda kumla tu, kwani huwezi kupata muendelezo wa huyo "kuku mwenye bora zaidi" bila kununua hiyo GMO ya huyo kuku kutoka kwao! Hayo ndiyo mambo ya GMO! Yanafanyika hivyo hadi kwenye mazoa! Hapa ndipo utegemezi na hatari inapo anzia.

Hizi za madukani ni nzuri sana ndizo hizo wanataka kuziondoa katika maisha na kilimo chetu. Kwa mfano mbegu zote zinazouzwa madukani zimezalishwa kutokana na utafiti wa kawaida tu , siyo wa kutumia GENES na kisha kuzi MODIFY, mbegu hizi ni zile zile zetu za miaka yote ila sasa zinaboreshwa kisayansi bila kutumia genes. Kwa mfano mahindi yanayotoa magunia 40 au zaidi kwa ekari ni yale yale ya miaka yote ila yamefanyiwa UTAFITI na kuboresha uzaaji wake. Hiyo ni kweli pia kwa mazao yote kama matikiti maji, mapapai n.k. Mbegu za GMO zitatufanya tuwe tegemezi kwa wenye mbegu zao na hivyo kutuingiza kwenye utegemezi hatarishi. Kongole kwa Serikali yetu kwa uamuzi huu wa ujasiri wa kupiga marufuku utafiti wake. Hongera sana Wizara ya Kilimo kwa kutunusuru na janga hilo.
 
Binafsi siukubali uhandisijeni. Nawapongeza wanasayansi wanaosimama kupinga uhandisijeni.

Uhandisijeni unaweza kuwa part and parcel ya conspiracy theory ye new world order...kwa maana kwamba watu wanatumia sayansi kwa malengo yao mabaya, hasa ktk kutaka kuitawala dunia kiuchumi na kisiasa, na kikubwa wao wanaona dunia imezidiwa na wingi wa watu hivyo kuna nia ya kupunguza idadi ya watu. Ni kama ilivyo kwa UKIMWI, EBOLA, SARS, saratani...ILA kubwa ni mabeberu kuuteka uchumi wa dunia kwa kumfanya mtu wa tabaka la chini kuwa mtumwa wa watu wa tabaka la juu.

Nashukuru serikali kufutilia mbali GMOs, warudi kwenye sheria na kurudisha kipengele cha awali kinachomtaka mtu aliyeingiza au kuleta GMOs kuwajibika kwa athari zote zitakazojitokeza.
 
Unaongea nini wewe unajua ulimwengu uliko sasa katika technology ya kilimo?. Mbona huwa mnaongea pumba tu. Unafikiri Ulaya, America, Asia wote hao wanakula chakula cha asili.

The matter here is TBS and TFDA mzee. Nikupe mfano unafikili nyanya zinazolimwa na kupigwa madawa yasiyo na uwiano sahihi ni salama Kwa matumizi ya binadamu?.

Haupo salama Kama unavyofikili, kuna asali ya kutoka Tabora tena wanaitwa ni ya asili ilifanyiwa analysis majubi yake haifai Kwa matumizi ya binadamu Kwa sababu imeasiliwa na dawa za kupulizia tumbaku.

Msishangilie Kila kitu jiulizeni Kwanini wazungu wanatumia Sana chemical food bado Maisha yao no marefu kuliko tuaojiita walaji wa vyakula vya asili. Baba TBS ni mhimu Kwa vyakula.
We kamtu mbona umejaa pumba kiasi hicho? Watu wanazungumzia sayansi wewe unaleta siasa na mambo ya kusema wengine, wengine... Wengine wanatuhusu nini? Ukiletewa GMO unadhani umependwa? Mbona mambo tunayohitaji hayaletwi kwa mshawasha kama hiyo GMO.

Kuna mtu pale Mwenge kakazana saana akiamini yeye gwiji wa sayansi, swa lakini hatuihitaji sasa hivi. Utapewa sifa na pesa kibao za utafiti lakini ibaki huko huko! Hatuhitaji promosheni na kampeni za GMO.
 
Nimeona makala nyingi zikielezea madhara ya GMO lakini serekali.ilikubali.kinyemela makampuni makubwa kuanza tafiti na kuingiza hiyo tech nchini! Athari zake ni kubwa sana kiafya ila naona tuna ahueni baada ya kupigwa marufuku!!
Naunga mkono hoja ya kuzipiga marufuku hizi mbegu
Unayoitaja kwamba ni serikali, ni watalaamu wanaodhani wanatufundisha ujanja wa GMO. Tamaa ya pesa kujikimu kama ilivyokuwa tawala za nyuma, inawafanya baadhi yao vichwa vichemke.

Jamaa wanahangaika kupitia kila njia. Akila Bill Gates wanajidai kuja na kusifu watu ili tutamani kufanya wanayotaka. Wanaojiita wanasayansi wanafanya kama ya wale waliowasaidia wazungu ktk biashara ya utumwa. Wanajua upuunzi ndani ya GMO lakini hawajali kwa kuwa tu, wanapewa pesa za kununua VX.
 
Unaongea nini wewe unajua ulimwengu uliko sasa katika technology ya kilimo?. Mbona huwa mnaongea pumba tu. Unafikiri Ulaya, America, Asia wote hao wanakula chakula cha asili.

The matter here is TBS and TFDA mzee. Nikupe mfano unafikili nyanya zinazolimwa na kupigwa madawa yasiyo na uwiano sahihi ni salama Kwa matumizi ya binadamu?.

Haupo salama Kama unavyofikili, kuna asali ya kutoka Tabora tena wanaitwa ni ya asili ilifanyiwa analysis majubi yake haifai Kwa matumizi ya binadamu Kwa sababu imeasiliwa na dawa za kupulizia tumbaku.

Msishangilie Kila kitu jiulizeni Kwanini wazungu wanatumia Sana chemical food bado Maisha yao no marefu kuliko tuaojiita walaji wa vyakula vya asili. Baba TBS ni mhimu Kwa vyakula.

Hivi do you know utofauti kati ya GMO ukiliganisha na madawa ya kupulizia mimea ili kuikinga dhidi ya wadudu waharibifu - hill LA kwanza.

La pili: Nchi zipi za Ulaya au Majimbo ya Marekani ulizo wahi kutembelea, ukabahatika kuingia kwenye aidha Super,Hypermarket au soko la kawaida ukakuta shelves za vyakula zimejazwa vyakula vya GMO?

Unayo yasema hapa yana ukweli gani? Au tuseme yanarandana vipi na masuala ya GMO?
 
Unayoitaja kwamba ni serikali, ni watalaamu wanaodhani wanatufundisha ujanja wa GMO. Tamaa ya pesa kujikimu kama ilivyokuwa tawala za nyuma, inawafanya baadhi yao vichwa vichemke.

Jamaa wanahangaika kupitia kila njia. Akila Bill Gates wanajidai kuja na kusifu watu ili tutamani kufanya wanayotaka. Wanaojiita wanasayansi wanafanya kama ya wale waliowasaidia wazungu ktk biashara ya utumwa. Wanajua upuunzi ndani ya GMO lakini hawajali kwa kuwa tu, wanapewa pesa za kununua VX.

Well said mkuu,jamaa hawa nilikwisha washtukia siku nyingi - wala sitashangaa kama hizi mbegu wanapewa na Monsanto halafu wanazuga Watanzania kwamba wamefanya tafiti wao!!

Yaani shinikizo lililokuwa linatumiwa na baadhi ya wabunge kupigia debe mbegu za GMO halikuwa la kawaida hata kidogo - miaka kama minne/mitano iliyo pita niliwahi kuzungumzia kwa kirefu kuhusu ubaya wa kula Frankstein food (GMO),kwa bahati mbaya bandiko langu lilidumu kwa siku moja tu baadae likaondolewa fasta, nafikiri walifabya hivyo kutokana na shinikizo la watu wanao pigia debe GMO nk - kumbuka Kampuni hizo zina fedha lukuki consequently are capable of doing anything under the SUN mradi malengo yao yanafikiwe

Mataifa mengi ya Dunia ya tatu Govt officials wanaongwa na jamaa hawa ili washinikize Serikali zao - kama huna Uzalendo unaweza kujikuta unawaingiza Watanzania wenzako kwenye matatizo ya kiafya pamoja na utegemezi wa mbegu zinazo zalishwa na makampuni ya kibepari, mbegu za asili zinakuwa cross pollinated na za GMO kwa njia ya pollen kupeperushwa na upepo, mwisho was siku mbegu asili zinakuwa extinct - watu wengi hawajui tu, mambo haya ni hatari sana sio ya kuchukuliwa poa hata kidogo. Mbinu za Bill Gates na wenzake zinajulikana zipo mpaka kwenye chanjo....
 
Awali ya yote, nipende kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa usikivu wake na kuchukua hatua stahiki kuhusiana na sakata la mimea na mbegu Zilizobadilishwa Vinasaba (GMO) nchini. Kama mtafiti wa Uhuru wa Chakula, napenda kuihakikishia Serikali kuwa, wadau mbalimbali wakiwemo wakulima, walaji, wazalishaji wa mbegu wa ndani, watafiti katika taasisi zetu za Kilimo (mbali na wale waliokuwa wakinufaika na mradi wa WEMA), na wauzaji wa vyakula nje na ndani ya nchi wamefarijika sana na hatua hii. Namshukuru Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, lakini pia natambua suala hili ni la kisera hivyo kwa namna yeyote linamhusu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania-Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Natoa pongezi za dhati kabisa kwa Serikali, na katika makala hii fupi nitaeleza kwa nini uamuzi huu ni wa kupongezwa.
 

Attachments

  • GMO.jpg
    GMO.jpg
    9.3 KB · Views: 32
Nov 21, 2018

KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO AITAKA TARI KUSITISHA MAJARIBIO YA GMO

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma


Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo, Mhandisi Mathew Mtigumwe leo tarehe 21 Novemba 2018 ameiagiza Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kusitisha mara moja utafiti na majaribio ya uhandisijeni (Genetic Modified Organisms(GMO) yanayofanyika kwenye vituo vyake vya utafiti.

Aidha, Katibu Mkuu ameilekeza Taasisi hiyo ya TARI kuwa mabaki yote ya majaribio ya Uhandisijeni yateketezwe mara moja.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Taasisi hiyo kuanza kutoa matokeo ya utafiti bila kupata idhini ya serikali.

Siku za hivi karibuni Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kupitia kituo cha Makutupora imekuwa inaalika watu mbalimbali kwenda kuona matokeo ya utafiti wakati serikali haijaruhusu matumizi ya uhandisijeni nchini.

For the English Audience
The Tanzanian government has ordered The Agricultural Research Institute(TARI) to stop all Genetic Engineering (Genetic Modified Organisms-GMO) research and testing in all its centers.

This is to be followed by destroying all of what remains of the GMO testing materials.

Recently the Institute without the consent of the Government, had started to disseminate and exhibit research results at one of its centers.


Zaidi, soma >> Nimeona wabunge wakishangilia ujio wa mbegu za GMO. Je, hawajui madhara yake kwa binadamu? - JamiiForums


Kwa wale wageni kwenye swala la GMOs,mada ifuatayo itasaidia kwa kiasi fulani kuonyesha hatari kubwa iliyopo mbele yetu.

Barua ya wazi kwa Rais Joseph Pombe Magufuli kuhusu GMOs.

areafiftyone
JF-Expert Member

Nov 5, 2018.

Mazao ya uhandisijeni(GMOs) ni janga la dunia,pamoja na sisi tulioko JamiiForums.
Mwenzetu Dr Richard Mbunda ambaye anakerwa na GMOs pamoja na mimi, labda na wengine,
amemuandikia Rais barua ya wazi akieleza kwa kina ubaya wa GMOs na kueleza wazi kwa nini anaamini GMOs kama zitaruhusiwa kulimwa nchini,zitaleta adhari kubwa kwa mazingira yetu,uchumi wetu, hasa wa wakulima wadogo wadogo na afya za Watanzania.Kwa vile janga la GMOs ni letu sote,tusome barua ya Dr.Richard Mbunda kwa makini halafu totoe mawazo yetu kama JF.Naomba baada ya hilo angalizo, sasa niombe moderators wasitoe uzi huu, ili watu waweze kutoa mawazo yao.Michango itakayotolewa hapa ina maana kubwa kwa kizazi hiki na vizazi vingi vijavyo.


Barua ya Wazi kwa Rais wa Tanzania: Je, GMOs ni Sera ya Serikali?

Na Dkt. Richard Mbunda (UDSM)

Mheshimiwa Rais,

Heri ya siku ya kuzaliwa!

Kwa heshima na taadhima, niruhusu mimi mtoto wa mkulima mdogo na mwananchi wa nchi yetu tukufu nikusalimu. Hali yangu mimi na wanafamilia wenzangu, ambao ni wakulima wadogo nchini, si njema kabisa. Mheshimiwa Rais, kama ujuavyo, sisi ni takribani asilimia zaidi ya 70 ya wananchi wote wa Tanzania, na naamini kuna ndugu zako wa damu ambao ni sehemu ya jamii hii ya watanzania.

Ukulima mdogo ndiyo uhalisia wetu. Hatuwezi kuukataa kwa sasa, japo wengi tuna matumaini ya kupiga hatua, kama serikali itatuwekea misingi thabiti. Lakini hali yetu ni ile, Waswahili wanasema ‘bora ya jana kuliko leo.’ Mikakati ya kumkwamua mkulima mdogo nitaieleza katika kitabu changu, lakini kwa leo niruhusu tu nikuulize swali la kisera.

Mheshimiwa Rais, tarehe 28 Septemba, 2018 Jijini Geneva, Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ilipitisha Azimio la Haki za Wakulima Wadogo. Azimio hili ni ushindi kwa wakulima wadogo duniani dhidi ya Makampuni hodhi katika sekta ya kilimo katika mapambano yaliyochukua zaidi ya miaka 17. Azimio hili linazungumzia haki za ARDHI, MBEGU, BAIOANUAI (Biodiversity) na SOKO LA NDANI LISINAJISIWE NA BIDHAA KUTOKA NJE.

Kimsingi haki hizi zinaendana na Uhuru wa Chakula (Food Sovereignty) kwa nchi maskini, ambao ndiyo uhuru pekee tuliobaki nao. Kinachonishangaza Mheshimiwa Rais, ni kuwa, pamoja na kuwa na idadi kubwa ya wakulima wadogo nchini, Tanzania haikuwakilishwa katika Azimio hili muhimu. Jumla ya nchi 34 zilikubali Azimio, nchi 11 zilikaa(abstain) na kama ilivyotegemewa, nchi zilizoendelea zilipinga Azimio hili. Mheshimiwa Rais, tulipitwa au hatujali? Namshukuru Mungu wa wanyonge, Azimio limepita.

Lakini Mheshimiwa Rais, mienendo ya Serikali inatupa mashaka makubwa zaidi sisi familia ya wakulima wadogo. Naliongea hili kwa ujasiri kwa kuwa nimekulia kilimo na naishi na wakulima wadogo. Hata utafiti wangu wa uzamivu uliwalenga wakulima wadogo na unahusu Uhuru wa Chakula Tanzania.

Mheshimiwa Rais, serikali imekuwa ikipigia chapuo teknolojia ya uhandisijeni wa mazao ya GMOs nchini. Tumeliona hilo katika Programu ya ASDP II uliyoizindua hivi karibuni, ambayo inatamka wazi mwelekeo wa kilimo chetu kwa matumizi ya GMOs, siyo tu katika mimea, bali hata wanyama (ikanifanya niwaze majaliwa ya ng’ombe za rafiki zangu Wamasai). Angalau basi tukusikie kwa maneno yako, je, wewe ni shabiki wa teknolojia hiyo na kwamba ni mdau wa mradi ya GMOs katika utafiti unaoendelea Makutupora, ambayo sasa inahalalishwa hapa nchini kupitia vyombo vya habari?

Barua yafaa iwe fupi ili isomeke kwa haraka na kueleweka kirahisi. Hivyo, Mheshimiwa Rais, nitaandika kwa uchache kuhusu sababu kwa nini Tanzania haihitaji GMOs. Lakini ninazo makala ndefu za kitaaluma zinazohusu jambo hili.

Sababu mojawapo ya kukataliwa GMOs inatokana na athari zake katika mazingira. Kwa mfano, katika utafiti uliofanywa na Mwanazuoni John Paul na kuchapishwa mwaka huu wa 2018, ikiwa na kichwa Genetically Modified Organisms (GMOs) as Invasive Species unaonesha kuwa GMOs ni viumbe vamizi. Huharibu mazao asilia, mimea mingine, wanyama na kuleta athari katika mazingira ya viumbe hai.

Hata katika elimu ndogo ya Kilimo tuliyojifunza sekondari, Mheshimiwa Rais, mahindi huzaa kwa uchavushaji. Kama mahindi ya GMOs na ya kawaida yatapandwa pamoja tutegemee nini? Kimsingi mahindi ya mbegu zisizo za GMOs yakiingiliana na ya GMOs yatapotea na kutuletea balaa kubwa la utegemezi huko mbeleni. Izingatiwe kuwa mbegu za GMOs hazirudiwi kupandwa zikatoa mazao.

Mheshimiwa Rais, napenda kujua kama hayo majaribio ya Makutupora yanajibu wasiwasi huu. Kwamba mbegu zao za GMOs hazitaathiri mbegu zetu, mimea mingine na mazingira kwa ujumla! Au ni utafiti unaoonesha tu kuwa GMOs zitastawi nchini? Mheshimiwa Rais unisamehe kwa kusema hili, hata bangi, ule mmea tunaoupiga vita, bado unastawi katika nchi yetu tukufu, tena vizuri mno.

Kupotea kwa mbegu zetu [kutokana na kuingiliana na mbegu za GMOs] kutatufanya tuwe watumwa wa makampuni ya mbegu. Mheshimiwa Rais, naamini umefuatilia habari kuhusu kampuni ya Monsanto, ambayo sasa imenunuliwa na kampuni ya Bayer ya Ujerumani kwa zaidi ya shilingi trilion 120 (USD 62 bn). Monsanto imekuwa ikipigwa vita hasa Amerika ya Kusini kwa namna ilivyotaka kuwafanya watu wake watumwa wa chakula. Pale ambapo tutapoteza mbegu zetu za asili, au tulizoziendeleza muda mrefu kupitia taasisi zetu za utafiti, tutakuwa tumekubali kuwa mateka.

Mheshimiwa Rais, wewe umekuwa ukipinga ubeberu kwa nguvu zako zote, na nisingependa hili la utumwa wa mbegu litokee katika utawala wako. Afrika Kusini, ambako waliruhusu GMOs tangu miaka ya 90, sasa zaidi ya asilimia 90 ya mahindi ni GMOs na wakulima wanalazimika kulipa ziada ya ada ya teknolojia kwa Monsanto. Pamoja na kubeparisha kilimo chao, bado Afrika Kusini hawajaweza kutokomeza njaa.

Suala la utamaduni wa chakula ni muhimu pia liongelewe katika muktadha huu. Kuna ladha, harufu nzuri na uasili wa chakula. Kama ujuavyo, Mheshimiwa Rais, hizi ni sifa pekee zinazotofautisha chakula chetu. Na tunapaswa kuvitunza vyakula hivi kwa choyo kubwa - hasa kwa kuwa sisi ni kitovu cha utalii Afrika.

Tukisoma baadhi ya makabrasha na shuhuda za wageni, tunaona watalii wanakizungumzia chakula chetu katika namna ya sifa ya pekee. Mheshimiwa Rais, pengine unakumbuka kuwa, mmoja kati ya watetezi wa GMOs Robert Paarlberg aliwahi kusema mwaka 2009 kuwa “chakula kilichozalishwa kiasili (organically) kina ladha na harufu ya kuvutia zaidi kuliko vyakula vya GMOs ndiyo maana nchi za Ulaya hazitaki GMOs" lakini "masikini wa Afrika hawapaswi kuwa na uchaguzi” Je, ni kweli tumefika sehemu ambayo hatupaswi kuwa na uchaguzi kwa kuwa sisi ni maskini?

Mheshimiwa Rais, katika makala yenye kichwa "No Scientific Consensus on GMO Safety," iliyochapisha wa wanasayansi 15 kwa pamoja katika Jarida la Environmental Sciences Europe mwaka 2015, tunaelezwa kwamba japo kumekuwa na jitihada za kuuaminisha ulimwengu kuwa GMOs ni salama kwa afya, lakini kimsingi hakujawa na muafaka wa usalama wa GMOs. Na kuna baadhi ya tafiti zilizoenda mbele kueleza kuwa GMOs zina madhara kiafya. Baadhi ya madhara ya afya yanayotajwa ni pamoja na uzio na saratani. Je, utafiti unaofanyika Makutupora unalenga kuleta majibu ya wasiwasi wa madhara ya afya yatokanayo na GMOs?

Monsanto imeshtakiwa zaidi ya mara hamsini huko Marekani na hivi karibuni ilipatikana na hatia, wananchi wakiilalamikia bidhaa zao kuwaleatea saratani. Kuhusu chakula cha GMO, jibu la kampuni hiyo limekuwa hilo hilo kuwa hawalazimiki kisheria kudhibitisha kuwa vyakula vyao havina madhara. Wanaojiita wanasayansi wetu nchini hawatuambii ukweli, labda kwa maslahi yao binafsi. Lakini katika majadiliano tuliyofanya HakiArdhi hivi karibuni, mmoja wa wanasayansi hao, baada ya kubanwa na wakulima, alikiri kuwa uangalifu unahitajika hasa katika mimea iliyobadilishwa kuzalisha sumu ili kuua wadudu.

Mheshimiwa Rais, Takwimu za Wizara ya Kilimo zinaonesha kuwa Tanzania bado hatujafikia hata asilimia 30 ya matumizi ya mbegu bora, mbolea na viuatilifu. Bado tumekuwa tukizalisha zaidi ya asilimia 120 ya chakula kinachohitajika nchini. Wiki tatu zilizopita nilikuwa Mkoa wa Rukwa (Sumbawanga) na nilikutana na Wazalishaji wanaolalamikia soko la mahindi na siyo changamoto za uzalishaji. Tena kuna waliovuna mahindi ya kutosha bila hata kutumia mbolea.

Lakini watu wa GMOs wanatuletea taarifa kuwa kuna uzalishaji mdogo sana na mahindi yanashambuliwa sana na wadudu. Kimsingi wanatangaza Hali ya Hatari (National Emergency) kwa jinsi wanavyotuonesha wadudu wala mahindi katika video zao. Mheshimiwa Rais, ni kweli tumefikia huko? Kama ni kweli mbona hujatutangazia hali ya hatari ili basi GMOs tuipokee kama hatua yetu ya kupunguza kifo cha haraka? Na kama siyo kweli, kwa nini tunalazimishwa kuruka kutoka kutumia mbegu za asili kwa asilimia 80 za sasa hadi GMOs, teknolojia ya juu kabisa wakati hatujaweza kuvuna tija itokanayo na mbegu bora za OPVs na Hybrid?

Kuna agenda gani hapo? Tunakimbilia wapi? Tunapitwa na nini?

Mheshimiwa Rais, sipendi nikuchose sana. Naomba niulize swali moja la mwisho. Ubora tulio nao kama nchi ukilinganisha na nchi zingine (Comparative Advantage) wanaouongelea wachumi au kile wasomi wa fani ya Biashara wanachokiiita eneo la ubora (niche) wetu lipo katika nini? Sidhani kama tunaweza kushindana na Marekani katika kuzalisha mahindi ya GMOs, chakula chenye unyanyapaa duniani kote. Sisi tunapaswa kuwa msingi wa chakula salama Afrika Mashariki na kwingineko duniani. Wakulima wetu wanapaswa kuwa msingi wa kuzalisha chakula hiki na kunufaika kama ilivyo sasa, ambapo soko bado si la uhakika.

Katika utafiti wangu nilitembelea vituo vya utafiti wa kilimo. Nikiri kuwa ni taasisi nyeti na zina wataalam (japo wametelekezwa) wanaoweza kutusaidia katika kuboresha mbegu zetu za asili kama wakiwezeshwa. Sote tunajua mbegu bora siyo lazima ziwe za GMO.

Mheshimiwa Rais, tukumbuke kuwa wakati wa Utawala wa Rais Dkt. Jakaya Kikwete, mradi wa GMO wa WEMA haukuanza nchini japo ulipaswa kuanza 2008. Hii ilitokana na kifungu kinachohusiana na dhamana ya uharibifu kijulikanacho kwa Kiingereza kama ‘strict liability’ kilichopo katika kanuni zetu za usalama wa viumbe na uhai (Biosafety). Kifungu hiki kilisema mtu atakeyeingiza GMOs nchini atawajibika moja kwa moja kwa madhara yoyote yatakayotokana na GMOs kiafya, kimazingira na kiuchumi.

Hiki kifungu kiliwachelewesha watu hawa wa WEMA kuanza utafiti mpaka mwaka 2016 Serikali ilipolegeza masharti na kuweka kifungu kinachosema ‘strict liability’haitatumika katika utafiti. Kama GMOs ni kitu chema kama WEMA unavyodai na ni ukombozi wetu, waliogopa nini kuanza 2008 hadi wakashawishi kanuni zibadilike? Hata sasa wanadai sheria zetu zinawabana wanataka tulegeze zaidi watuletee balaa tushindwe pa kuwabana.

Walaji wa chakula kinacholimwa na wakulima wadogo hawapo salama pia. Muda si mrefu tutaanza kuona maduka makubwa (supermarkets) za vyakula vya asili (organic food) ambavyo watu wa kada ya juu tu ndio pekee watamudu kununua. Wameshaanza na madogo madogo. Tunaendelea kutengeneza matabaka kwa maslahi ya mwekezaji.

Mheshimiwa Rais, huenda barua hii haitakupendeza. Najua pia barua hii haitawapendeza wadau na watunga sera wanaopigania GMOs izidi kutamalaki nchini. Hakika itaichukiza kampuni husika inayowekeza katika mradi wa WEMA huko Makutupora.

Wanatudhihaki kuwa sisi tunapinga sayansi. Lakini ni sayansi zipi tumezipinga hapa nchini? Kama alivyowahi kusema mwanazuoni nguli Karl Polanyi mwaka 1944, hatuwezi kuiruhusu teknolojia ya kinyonyaji na inayokusudia kunufaika na majanga ya watu itamalaki.

Mheshimiwa Rais, nakushukuru kwa kusoma hii barua. Hatimaye nimetimiza wajibu wangu. Nimesema ukweli na sina haja ya kujificha.
SERIKALI YA MHESHIMIWA RAIS DOCTOR JP. MAGUFULI NINAIPONGEZA KWA KUONA UMUHIMU WA AFYA ZA BINADAMU KWA KUPIGA MARUFUKU UTENGENEZAJI WA MBEGU ZA VYAKULA FEKI VYENYE SUMU VYAKULA VYA KUTENGENEZWA MAVIWANDANI AKA VYAKULA VYA GMO HONGERA SANA RAISI WETU MUNGU MLINDE DOCTOR MAGUFULI AMIN.

Zijue faida na hasara za mbegu za kisasa za GMO zilizopigwa marufuku Tanzania chanzo.https://www.bbc.com/swahili/habari-46313408

Zijue faida na hasara za mbegu za kisasa za GMO zilizopigwa marufuku Tanzania.jpg
 
1. Wakuu hebu tuelimishane kidogo, hizo mbegu za gmo zinazoongelewa hapa ni zipi?

2. Nachojua mbegu zooote zinazotumiwa na wakulima wetu kwa sasa ni hizo ambazo ukivuna huwezi kutumia mazao yake kama mbegu kwa zao la mwaka unaofata.

3. Sasa hivi ili uweze kupata mazao ya uhakika ni lazima kwanza ununue mbegu mpya dukani ndo uipande. Hapo mavuno yanakuwa ni uhakika. Na hii unafanyika kila mwaka.

4. Hii haijaanza juzi wala jana, ni miaka mingi sasa.

Je mbegu hizi zina utofauti na hizo za gmo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari nzuri sana, hizi mbegu za GMOs ni mpango wa wazungu wa kuzifanya nchi za Dunia ya Tatu ziwategee wao,..

Ukianza kutumia hizi mbegu basi inabidi uagize kutoka kwao, kila unapozihitaji..
 
Naona Waziri Mkenda Katoa tena tamko kulikoni ina maana hili agizo toka 2018 halikufanyiwa kazi?
 
Sasa mbona na huyu leo anapiga tena marufuku, ina maana serikali ilidharauliwa marufuku ya kwanza?
 
labda tafsiri ya gmo watu hwajailelewa vizuri , mbegu organic ni zile za kienyeji tuu. Hizi zote zinazozalishwa na zilizopo madukani na tunazohamasishwa tulime kisasa na nyingi zipo kwa majina ya F.1 zote ni geneticaly modfined ( G.M.O) I stand to be corrected
Tofautisha Hybridization na Genetic modification, sawa? Mzungu akizaa na muAfrika hiyo ni hybridization, ila ukichukua vinasaba vya mbwa na kuviingiza kwenye yai la binadamu ili azaliwe binadamu mwenye uwezo wa kunusa kama mbwa hiyo ni genetic modification, tumeelewana?
 
1. Wakuu hebu tuelimishane kidogo, hizo mbegu za gmo zinazoongelewa hapa ni zipi?

2. Nachojua mbegu zooote zinazotumiwa na wakulima wetu kwa sasa ni hizo ambazo ukivuna huwezi kutumia mazao yake kama mbegu kwa zao la mwaka unaofata.

3. Sasa hivi ili uweze kupata mazao ya uhakika ni lazima kwanza ununue mbegu mpya dukani ndo uipande. Hapo mavuno yanakuwa ni uhakika. Na hii unafanyika kila mwaka.

4. Hii haijaanza juzi wala jana, ni miaka mingi sasa.

Je mbegu hizi zina utofauti na hizo za gmo?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ni hivyo usemavyo, basi, tumeshamalizwa !!
 
Tofautisha Hybridization na Genetic modification, sawa? Mzungu akizaa na muAfrika hiyo ni hybridization, ila ukichukua vinasaba vya mbwa na kuviingiza kwenye yai la binadamu ili azaliwe binadamu mwenye uwezo wa kunusa kama mbwa hiyo ni genetic modification, tumeelewana?
Kuna tofauti kubwa kati ya Natural hybridization kama hiyo ya mzungu na mwafrika na artificial hybridization inayofanywa na gene technologists .Kwenye suala la mimea wanabadilisha mpangilio halisi wa gene ,wanaondoa zile bad traits zote kama magonjwa, kuchelewa kukua, ukame na udogo na ku replace na traits bora kitu ambacho hakifanyiki baina ya binaadamu
 
Kuna tofauti kubwa kati ya Natural hybridization kama hiyo ya mzungu na mwafrika na artificial hybridization inayofanywa na gene technologists .Kwenye suala la mimea wanabadilisha mpangilio halisi wa gene ,wanaondoa zile bad traits zote kama magonjwa, kuchelewa kukua, ukame na udogo na ku replace na traits bora kitu ambacho hakifanyiki baina ya binaadamu
Hybridization (natural/artificial) imekuwepo tangu karne na karne, ambapo genes ambazo zipo tayari ina nature zinakuwa cross bred kama zilivyo Kwenye organism of origin ili kupata desirable traits, kinachokatazwa hapa ni Genetic modification (modification at the genetic level)
 
Back
Top Bottom