Serikali yatangaza mlipuko wa Ugonjwa wa Surua Nchini

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Serikali imetangaza mlipuko wa Ugonjwa wa Surua katika baadhi ya maeneo baada ya uchunguzi kufanyika na kubaini wagonjwa 54 lakini hakuna taarifa ya kifo.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema uchunguzi wa sampuli za Julai hadi Agosti 2022 umeonesha mlipuko upo katika Halmashauri 7 zikiwemo Bukoba, Handeni, Kilindi, Kigamboni, Mkuranga na Temeke.

Pia kuna Halmashauri zenye wagonjwa wa Surua lakini hazijafikia vigezo vya kuwa na mlipuko.

 
Mlipuko? Unajua maana ya mlipuko? Surua ni ugonjwa wa mlipuko (epidemic)?

Ugonjwa wa Surua unaweza kuwa unaanza kurudi kutokana na Magufuli kuwaaminisha Watanzania wengi kuwa Chanjo ni mpango wa wazungu kutuua
Sijui yeye kwa nini hakufa na wakati alipigwa chanjo

Aungue milele yule dikteta
 
Mimba yako ya chuki dhidi ya Hayati JPM itakutesa sana, na utapata tabu sana na kisichokujibu wala kukusikia.

Eventually an insanity it exists.
 
Mkuu asante,Wananchi waliaminishwa kuwa Chanjo ni mpango wa Mabeberu kutumaliza kisha wajizolee Madini na Maliasili zetu.
 
Mkuu asante,Wananchi waliaminishwa kuwa Chanjo ni mpango wa Mabeberu kutumaliza kisha wajizolee Madini na Maiasili zetu.
Mfia dini muda wa swala huu acha kuandika upumbavu jf
 
... sijui kama wale jamaa hii (chanjo) nayo wataikataa? Hizi chanjo ni kwa hisani ya watu wa Marekani na EU na sio Russia hilo liwekwe wazi.
Kwani ugonjwa wa Surua huwezi mtoto ukamfukiza nyungu au kwenye kinanda kilichojengwa muhimbili Hosp?
 
Endeleeni kugomea chanjo kumuenzi marehemu nduli wa chato
 
Hivi hizi mimba zenu alizowapa magufuli bado hamjajifungua tu?
 
Kids kufanana! Hii taarifa utatengeneza 'fursa kinoma'; inaweza hata kutupatia mkopo wa dharura kuthibiti surua.
 
... sijui kama wale jamaa hii (chanjo) nayo wataikataa? Hizi chanjo ni kwa hisani ya watu wa Marekani na EU na sio Russia hilo liwekwe wazi.
Nasikia

Kuadimika kwa chanjo mahospitalini ni BAADA ya USA kusitisha misaada ya kifedha kwa shirika la afya DUNIANI WHO BAADA ya kutoonyesha kwetu msimamo wa upande wetu kwe HIYO vita ya Ukraine na Russia!!

Sijui kuna ukweli kiasi GANI kwenye hili!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…