Serikali yatoa siku 30 kwa Taasisi zinazodaiwa na TTCL kulipa madeni ya huduma waliyopewa

Serikali yatoa siku 30 kwa Taasisi zinazodaiwa na TTCL kulipa madeni ya huduma waliyopewa

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk Faustine Ndugulile amezipa siku 30 taasisi za umma zinazodaiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) zilipe shilingi bilioni 30 ndani ya mwezi mmoja.

Dk Ndugulile alitoa agizo hilo jana alipotembelea TTCL na kuzungumza na wajumbe wa Bodi, menejimenti na wafanyakazi wa shirika hilo Dar es Salaam.

Alisema, zaidi ya taasisi 20 za Serikali zinadaiwa na TTCL zaidi ya shilingi bilioni 30, na kwamba, zipo taasisi zinazotumia huduma za shirika hilo na zinakusanya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa mwezi ila hazipo tayari kulipa huduma za TTCL. Dk Ndugulile pia alitoa onyo kali kwa kampuni zinazohujumu miundombinu ya TTCL ili ishindwe kutoa huduma za mawasiliano kwa wateja wake.

Alisema, wanaoiba nyaya za shaba za TTCL na kuuza kama chuma chakavu nao waache mara moja kwa kuwa watahusishwa na uhujumu uchumi kwa kudhoofisha utendaji kazi wa TTCL.

Aliwataka watendaji wa Wizara kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kufanya utafiti na tathmini ya kubaini mchango wa sekta ya mawasiliano aidha wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja katika kukuza uchumi na kuchangia pato la taifa.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Kundo Mathew aliwataka watumishi wa TTCL kuwa wabunifu na kuacha kufanya kazi kwa mazoea na wajenge utaratibu wa kufuata na kuwahudumia wateja waliko badala ya kuwasubiri ofisini.
 
Kwani TTCL wenyewe hawawezi kwenda kudai mpaka wamtumie waziri? Ndiyo biashara zipo hivyo? Inakuwa kama maloan sharks na Ndugulile ndiyo enforcer!
 
Watoto wa baba mmoja hawa sasa baba yao anawambia walipe, pesa zote zipo serikali kuu sasa hata wakilipa hazikai kwenye account ya TTCL koo wanahamisha tu mfuko wa kushoto wanapeleka kulia.
 
Kwani TTCL haiwezi kudai hadi kwa msaada wa waziri?
Umesahau matrekta ya Suma jkt nao wakopaji hawakuyalipa mpk mkuu akaingilia na sijui kama yalilipwa.

Habari gani mkuu pia kushurutisha wafanyakazi wote wa serikali wawe na laini za hiyo titisiel

Kwa hiyo ndiyo style hiyo ili mambo yaende ni mpk mkubwa aseme
 
IMG_20201222_155611.jpg

Happy New Year
 
Waziri wa michezo batshungwa amepewa wizara ambayo haimtoshi/haiwezi yupoyupo tu, yy Kila sehemu lazima aende .

Hana focus ajui michezo ni nn? Hana vipaumbele, zaidi ya kutembea tembea tu.

Rais amtafutie kazi ingine huyu kijana, haters mpite hivi haha no maoni yangu.
 
Nayo TTCL iwe tayari sasa kuwapa ajira ya kudumu wahitimu shahada wanaosota kama vibarua kwenye shirika hilo.
 
WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk Faustine Ndugulile amezipa siku 30 taasisi za umma zinazodaiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) zilipe shilingi bilioni 30 ndani ya mwezi mmoja.

Dk Ndugulile alitoa agizo hilo jana alipotembelea TTCL na kuzungumza na wajumbe wa Bodi, menejimenti na wafanyakazi wa shirika hilo Dar es Salaam.

Alisema, zaidi ya taasisi 20 za Serikali zinadaiwa na TTCL zaidi ya shilingi bilioni 30, na kwamba, zipo taasisi zinazotumia huduma za shirika hilo na zinakusanya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa mwezi ila hazipo tayari kulipa huduma za TTCL. Dk Ndugulile pia alitoa onyo kali kwa kampuni zinazohujumu miundombinu ya TTCL ili ishindwe kutoa huduma za mawasiliano kwa wateja wake.

Alisema, wanaoiba nyaya za shaba za TTCL na kuuza kama chuma chakavu nao waache mara moja kwa kuwa watahusishwa na uhujumu uchumi kwa kudhoofisha utendaji kazi wa TTCL.

Aliwataka watendaji wa Wizara kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kufanya utafiti na tathmini ya kubaini mchango wa sekta ya mawasiliano aidha wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja katika kukuza uchumi na kuchangia pato la taifa.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Kundo Mathew aliwataka watumishi wa TTCL kuwa wabunifu na kuacha kufanya kazi kwa mazoea na wajenge utaratibu wa kufuata na kuwahudumia wateja waliko badala ya kuwasubiri ofisini.
Tuanomba baada ya siku 30 tupate mrejesho wa utekelezaji wakee kwa kuwa hizi directive order nyingi huishia mititi baada ya kutangazwa kwa mbwebwe
 
WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk Faustine Ndugulile amezipa siku 30 taasisi za umma zinazodaiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) zilipe shilingi bilioni 30 ndani ya mwezi mmoja.

Dk Ndugulile alitoa agizo hilo jana alipotembelea TTCL na kuzungumza na wajumbe wa Bodi, menejimenti na wafanyakazi wa shirika hilo Dar es Salaam.

Alisema, zaidi ya taasisi 20 za Serikali zinadaiwa na TTCL zaidi ya shilingi bilioni 30, na kwamba, zipo taasisi zinazotumia huduma za shirika hilo na zinakusanya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa mwezi ila hazipo tayari kulipa huduma za TTCL. Dk Ndugulile pia alitoa onyo kali kwa kampuni zinazohujumu miundombinu ya TTCL ili ishindwe kutoa huduma za mawasiliano kwa wateja wake.

Alisema, wanaoiba nyaya za shaba za TTCL na kuuza kama chuma chakavu nao waache mara moja kwa kuwa watahusishwa na uhujumu uchumi kwa kudhoofisha utendaji kazi wa TTCL.

Aliwataka watendaji wa Wizara kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kufanya utafiti na tathmini ya kubaini mchango wa sekta ya mawasiliano aidha wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja katika kukuza uchumi na kuchangia pato la taifa.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Kundo Mathew aliwataka watumishi wa TTCL kuwa wabunifu na kuacha kufanya kazi kwa mazoea na wajenge utaratibu wa kufuata na kuwahudumia wateja waliko badala ya kuwasubiri ofisini.
Hayo ni maelewano ya kibiashara Kati ya TTCL na wateja wake,waziri hapaswi kuingilia.Yeye atoe falsafa za kuboresha TTCL na wizara kwa ujumla.
 
Hii huduma naona kama tunalazimishwa sasa.

Kwanini wasiendeshe kwa mfumo kwa PRE-PAID kwa ushindani kama makampuni mengine?

Naona serikali inajitafuna yenyewe halafu inajipa onyo yenyewe.

Maagizo kama haya tumeyazoea. Yanakamyagwa mara tu baada ya wiki moja

Kwani TTCL wenyewe hawawezi kwenda kudai mpaka wamtumie waziri? Ndiyo biashara zipo hivyo? Inakuwa kama maloan sharks na Ndugulile ndiyo enforcer!

Kwani TTCL haiwezi kudai hadi kwa msaada wa waziri?

Watoto wa baba mmoja hawa sasa baba yao anawambia walipe, pesa zote zipo serikali kuu sasa hata wakilipa hazikai kwenye account ya TTCL koo wanahamisha tu mfuko wa kushoto wanapeleka kulia.

Umesahau matrekta ya Suma jkt nao wakopaji hawakuyalipa mpk mkuu akaingilia na sijui kama yalilipwa.

Habari gani mkuu pia kushurutisha wafanyakazi wote wa serikali wawe na laini za hiyo titisiel

Kwa hiyo ndiyo style hiyo ili mambo yaende ni mpk mkubwa aseme

Inatakiwa baada ya siku 30 kuisha waandishi wamfate kumuuliza kama agizo lake lilitekelezwa, na kama kuna ambaye hajatekeleza anachukuliwa hatua gani?

Na uzuri au ubaya wadaiwa sugu wanajulikana wanaongozwa na Majeshi yote sio Polisi,Magereza,Uhamiaji na wale wazee wa Bakabaka wenyewe

Sasa nani wa kwenda kuwakatia hiyo huduma huko??

Haya ni maneno kama maneno mengine tu siku 30 zitapita na hakuna litakalofanyika.

Na ndio maana TTCL haiwezi kuendelea kibiashara wala kujiendesha bila kuingiliwa kisiasa kwasababu ya mafungamano hayo.

Wakitaka wawabadilishie woote wawe na mfumo wa PREPAID baasi sio hiyo habari ya pili mpk inafika mabilioni
 
WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk Faustine Ndugulile amezipa siku 30 taasisi za umma zinazodaiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) zilipe shilingi bilioni 30 ndani ya mwezi mmoja.

Dk Ndugulile alitoa agizo hilo jana alipotembelea TTCL na kuzungumza na wajumbe wa Bodi, menejimenti na wafanyakazi wa shirika hilo Dar es Salaam.

Alisema, zaidi ya taasisi 20 za Serikali zinadaiwa na TTCL zaidi ya shilingi bilioni 30, na kwamba, zipo taasisi zinazotumia huduma za shirika hilo na zinakusanya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa mwezi ila hazipo tayari kulipa huduma za TTCL. Dk Ndugulile pia alitoa onyo kali kwa kampuni zinazohujumu miundombinu ya TTCL ili ishindwe kutoa huduma za mawasiliano kwa wateja wake.

Alisema, wanaoiba nyaya za shaba za TTCL na kuuza kama chuma chakavu nao waache mara moja kwa kuwa watahusishwa na uhujumu uchumi kwa kudhoofisha utendaji kazi wa TTCL.

Aliwataka watendaji wa Wizara kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kufanya utafiti na tathmini ya kubaini mchango wa sekta ya mawasiliano aidha wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja katika kukuza uchumi na kuchangia pato la taifa.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Kundo Mathew aliwataka watumishi wa TTCL kuwa wabunifu na kuacha kufanya kazi kwa mazoea na wajenge utaratibu wa kufuata na kuwahudumia wateja waliko badala ya kuwasubiri ofisini.
Na wao TTCL madeni wanayodaiwa walipe ndani ya siku ngapi?
 
Back
Top Bottom