Bi. Senti 50
JF-Expert Member
- Apr 17, 2007
- 287
- 12
I found this on Tanzania Daima for those who need updates:
KATIKA kuwasaidia wanafunzi walikokwama nchini Ukraine, Shirika la kuhudumia wanafunzi la Tanzania Legal Education Trust (TANLET), limekusanya sh milioni 3 ambazo zitasaidia kuwalipia sehemu ya ada wanazodaiwa wanafunzi hao.
Uchangishaji wa fedha hizo umekuja baada ya wanafunzi hao kukwama kujilipia ada na serikali kukataa kuwalipia kwa kile kinachodaiwa kuwa, hawapo katika mahesabu ya kulipiwa na serikali.
Hivi karibuni, viongozi kutoka vyama vya upinzani vinne walilitaka shirika hilo kufungua akaunti maalumu kwa ajili ya wahisani mbalimbali kuweza kuchangia ili wanafunzi hao waweze kulipiwa fedha hizo.
Akizungumza kwa njia ya simu jana, Mkurugenzi Mtendaji wa TANLET, Mwalimu Nderakindo Kesi, aliiambia Tanzania Daima kuwa, hadi sasa akaunti hiyo ina sh milioni 3 na jana waliweza kuwatumia dola 1,000.
Alisema kiasi hicho bado ni kidogo kutokana na mahitaji ya fedha zinazotakiwa, kinachohitajika ni kikubwa kulingana na ukubwa wa ada wanazotakiwa kulipa.
Fedha hizi bado ni kidogo kutokana na ukweli kuwa wanadaiwa fedha nyingi na katika akaunti kuna sh milioni 3, lakini hii ni kwa sababu hapa katikati tulikwama kuendelea kuchangisha kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo, alisema Kesi.
Alisema mbali ya kufungua akunti hiyo yenye namba 2016600043 katika benki ya NMB, pia wanachangisha kupitia kusaini katika makaratasi ambapo wafanyabiashara wengi wamejitokeza kuchangia.
TANLET yasaidia wanafunzi Ukraine
na Mkolo KimenyaKATIKA kuwasaidia wanafunzi walikokwama nchini Ukraine, Shirika la kuhudumia wanafunzi la Tanzania Legal Education Trust (TANLET), limekusanya sh milioni 3 ambazo zitasaidia kuwalipia sehemu ya ada wanazodaiwa wanafunzi hao.
Uchangishaji wa fedha hizo umekuja baada ya wanafunzi hao kukwama kujilipia ada na serikali kukataa kuwalipia kwa kile kinachodaiwa kuwa, hawapo katika mahesabu ya kulipiwa na serikali.
Hivi karibuni, viongozi kutoka vyama vya upinzani vinne walilitaka shirika hilo kufungua akaunti maalumu kwa ajili ya wahisani mbalimbali kuweza kuchangia ili wanafunzi hao waweze kulipiwa fedha hizo.
Akizungumza kwa njia ya simu jana, Mkurugenzi Mtendaji wa TANLET, Mwalimu Nderakindo Kesi, aliiambia Tanzania Daima kuwa, hadi sasa akaunti hiyo ina sh milioni 3 na jana waliweza kuwatumia dola 1,000.
Alisema kiasi hicho bado ni kidogo kutokana na mahitaji ya fedha zinazotakiwa, kinachohitajika ni kikubwa kulingana na ukubwa wa ada wanazotakiwa kulipa.
Fedha hizi bado ni kidogo kutokana na ukweli kuwa wanadaiwa fedha nyingi na katika akaunti kuna sh milioni 3, lakini hii ni kwa sababu hapa katikati tulikwama kuendelea kuchangisha kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo, alisema Kesi.
Alisema mbali ya kufungua akunti hiyo yenye namba 2016600043 katika benki ya NMB, pia wanachangisha kupitia kusaini katika makaratasi ambapo wafanyabiashara wengi wamejitokeza kuchangia.