Serikali yazidiwa nguvu kodi ya simu

Serikali yazidiwa nguvu kodi ya simu

Kama Naibu waziri wa Mawasiliano anapingana na Waziri wa fedha hadharani juu ya kitu ambacho wao wamekipitisha hii ina maana gani zaidi ya kukurupuka??

Kwa nini wasiwe na kauli moja ambayo tutaiita kauli ya serikali???

Wale wajenzi wa mnara wa babeli walianza kupishana lugha kama haya masisiem chama kinasema kinapinga huku majitu yalisema ndiyoooo kwa vile posho ndiyo kipaumbele shame on you
 
Serikali ni vivu kufikiri. Ukitaka kodi kutoka kwenye makampuni ya simu ni jambo rahisi sana. Kila kampuni ya simu inafanya reconciliation ya mapato kwa siku, kwa wiki kwa mwezi na nk. Naongelea actual reconciliation sio ile cooked report wanayoitengeneza.

Serikali inaweza kutumia vyombo vyake vikiwemo vya usalama kuconnect kwenye database za campuni za simu na kupata exact transaction na fund zinazoingia kwa siku kutoka hapo wanakata kodi yao bila kumuathir mtumiaji wa mwisho. Haliitaji kutenga budget wala fungu la kununu vifaa vya bilions of money kupata taarifa kama hizo. Serikali ikiwa serious kidogo tu na kuondoa maslai binafsi na kufikiri kwa maslai ya taifa hilo halina utata.

Amkeni tumikieni watanzania waliowaamini kuendesha nchi yao na sio matumbo yenu. Kizazi kijacho kitatusha ngaa kama tutaendelea kuongeza deni la nchi wakati tunaweza kukopesha nchi nyingine
 
Wale wajenzi wa mnara wa babeli walianza kupishana lugha kama haya masisiem chama kinasema kinapinga huku majitu yalisema ndiyoooo kwa vile posho ndiyo kipaumbele shame on you
Kimsingi hii ni dalili ya kuanguka kwa utawala wowote.siku zote utawala uliofitinika hauwezi kusimama hata siku moja.....
 
Ushauri wowote wa Chenge naufananisha na nguvu za giza.......hivi serikali imekosa mtu wa kuishauri mpk chenge? ukate sh 450 kwa siku ! huyu mzee alifikiria nini au ndio alitaka kufuta yale makovu ya vijisenti vyake kwa kujipendekeza kwa serikali?
 
Kumekuwa na mjadala mpana sana juu ya kodi iliyopitishwa na bunge ya kadi za simu za mkononi. Kimsingi kama Chama tumeshatoa msimamo juu ya kodi hii.(SERIKALI IANGALIE VYANZO VINGINE NA KODI HII IFUTWE). Ninamshukuru na kumpongeza Rais kwa msimamo wake juu ya hili. Agizo la Rais kwa wahusika kulitafakari upya swala hili ni la muhimu litekelezwe kwa wakati.

Hapa nataka kusisitiza tu kuwa ni lazima serikali isikilize kilio cha wananchi ambao ndio chanzo cha madaraka yote ya serikali. Kinachonitia moyo mijadala mingi kwasasa juu ya hili imehusisha mapendekezo ya maeneo mbadala ya wapi pengo litakalosababishwa na kuondolewa kwa kodi hiyo litakavyozibwa. Hapa serikali lazima ionyeshe usikivu.

Serikali isikilize kilio cha wananchi au serikali ikubali kuwa ilitaka kutuburuza na wananchi tumeigomea?
Acha porojo na kutufanya sote wajinga...mfa maji haishi kutapa.
Brother Nape nakuchukia sana b'se unalazimisha kutufanya sote wajinga.
Angalia lisije kukutokea puani.
 
Kaka bulama hebu acha kueneza hizi propaganda za rejareja. Wanaotoa matamshi wote wanakinzana. Nilishaacha kuwaamini nduli hawa miaka kadhaa, hata kabla ya CHADEMA kupata umaarufu.

Najua wapo wengi ambao wamejitwisha kazi niliyoianzisha ya kususia MITANDAO YOTE ya simu, kwa siku moja, kazi niliyoiasisi. Serikali inaogopa kupoteza mapato ndio maana inakuja na danganya toto za ki-hunihuni tu, ili tuamini tumeishinda. Hizo ni propaganda ambazo watu kama wewe wamelipwa kuzieneza. Kaka au dada, kaa uelewe kwamba Watanzania wa leo si wale wa 2005, na hakika, Watanzania wa leo hawatafanana hata kidogo na wale wa 2015. Nini kimebadilika au kitabadilika? Soma alama za nyakati!

Nakutuma uende kwa hao waliokutuma ukawaambie kwamba mgomo wetu wa kuzima simu nchi nzima kwa mitandao yote, 19-08-13 hadi 20-08-13 kwa muda wa saa 24, yaani kuanzia saa 6 usiku hadi saa 6 usiku wa kesho yake, UKO PALE PALE.

Niko radhi kutokuwa na mawasiliano kwa siku moja, lakini siko tayari kuiunga mkono serikali iliyoasi wananchi wake na kuwageuza chanzo cha mapato haramu. Wizi wa mchana na ufisadi huu tunaupinga kwa nguvu zetu zote.

Wakiuliza nani kakutuma, waambie ni mimi Mwana wa Haki, a.k.a. MwanaHaki, Mzalendo Namba 1.

Siogopi kufa. Nikifa nitakufa kifo cha kishujaa, Mungu atanipokea mbibguni kwa kuwatetea watoto wake Watanzania, na atanilipia kisasi.

Isitoshe, nikifa mtakuwa mmechochea moto wa mashujaa wengine kuja nyuma yangu kwa mamia ya maelfu, kama si mamilioni.

Kazi ni kwenu!
 
Last edited by a moderator:
Nape Nnauye sina mjadala mrefu nawe. Elewa kwamba Watanzania wa leo si wale wa 1995 na pia Watanzania wa leo hawatakuwa wale wa 2015.

Msitufanye wajinga na mazuzu, eti kodi iangaliwe upya! Ili iweje.

Hapa kuna mawili tu. Kuifuta au kuibakiza. Mkiibakiza msitarajie tutatishika na kuikubali. Mkiifuta mtakuwa mmeanza safari ndefu, ya si chini ya miaka 30 ya kukubalika kwa umma.

Kila la heri.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom