Service Road' nyingi zimekuwa sio salama kwa Watumiaji, kuna uzembe unafanyika na kusababisha ajali nyingi

Service Road' nyingi zimekuwa sio salama kwa Watumiaji, kuna uzembe unafanyika na kusababisha ajali nyingi

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
photo_2024-09-20_14-07-42.jpg
Licha ya jitihada mbalimbali ambazo zimekuwa zikichukuliwa na vyombo vilivyopewa dhamana kusimamia usalama barabarani hususani 'Traffic' pamoja na wadau wengine, lakini bado kuna changamoto ya msisitizo wa matumizi stahiki ya 'service road' hasa Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya barabara ambazo naweza kuzitumia kama mfano licha ya kuwa na tija, ni kipande cha Service road kilichopo Tabata Mwananchi, kipande cha Mbezi beach (kituo cha Shule hadi kituo cha Makonde pamoja na kipande cha Africana), njia hizi zimekuwa hatari kwa usalama wa wananchi wanaoendesha vyombo vya moto hata kwa watembea kwa miguu.

'Service road' zinaoneka kuwa njia hatarishi kutokana na kutokuwa na alama muhimu barabarani ambazo utakiwa kuzingatiwa kama zilivyo njia rasmi, mfano alama za zebra ambazo utumika kama sehemu ya watembea kwa miguu kuvuka.
photo_2024-09-20_14-07-42 (2).jpg

photo_2024-09-20_14-07-41.jpg
Kutokana na kukosekana kwa wingi kwa alama hizo muhimu, baadhi ya watu wamekuwa wakiendesha vyombo vya moto hususani magari na bodaboda bila kwa mwendokasi kwenye njia hizo kujali usalama wao sambamba na abiria watembea kwa miguu.

Hatari hiyo kubwa hasa inaongezeka zaidi mida ya usiku ambapo wandesha vyombo vya moto wengi wao wanakuwa na mwendokasi bila kuzingatia usalama wa watembea kwa miguu.

Changamoto nyingine inayochangia uwepo wa hatari kubwa baadhi ya service road kuna maeneo 'bodaboda' wameanzisha vituo (parking) jambo ambalo linaongeza uhatari.

Hatari katika njia hizo inakuwa kubwa kwa sababu Traffic fokasi (focus) yao kubwa inakuwa ni kwenye njia rasmi huku service road zikendelea kutumika vibaya.

Wito wangu kwa mamlaka, kwa kuwa tayari wapo watu wamepoteza maisha na wengine kupata ulemavu kutokana na 'service road', nashauri mamlaka kuongeza usimamizi katika njia hizo, ikibidi katika njia za aina hiyo ambazo wakati mwingi utumika kama njia rasmi ziwekewe alama muhimu ikiwemo zebra pamoja na matuta ili kupunguza ajari zinazoweza kuzuilika.

Pia mamlaka zifuatilie kwa ukaribu maeneo ya 'service road' ambapo bodaboda wameamua kuweka vituo vyao waone kama ni salama, ikibidi baada ya ufuatiliaji huo waelekeze kwa utaratibu rafiki bodaboda kupaki katika maeneo ambayo yataonekana kuwa salama.

Kwa kuyafanya hayo tutaokoa maisha ya wengi, lakini hali iliyopo ikiendelea uenda watu wataendelea kupata ulemavu na pengine wengine kupoteza maisha.
 
Tz service siyo service road tena
Nyingi zimevamiwa
Nchi ya ajabu sana hii

Ova
 
Sijaelewa maana ya service roads? Nacho fahamu ulicho onyesha wewe ni pedestrian. service road ni njia ya muda wakati njia kuu inatengenezwa au kufanyiwa ukarabati.
 
Back
Top Bottom