Seven: Ommy Dimpoz hayupo ICU anaendelea vizuri

Seven ajifunze watu hawakanishi taarifa za mgonjwa hadharani. Wanavumilia. Mgonjwa maana yake anaumwa na anaendelea kutibiwa.
 
Ommy ana hali mbaya yupo ICU kitachomuokoa ni maombi yetu tu. Sijajua why Seven ataki kusema ukweli.
Kwa hiyo wewe ndio unajua ukweli kuliko yeye? Hivi kwanini watanzania mnapenda kuwa wajuvi kwa kila jambo?
 
Kuna member humu. Jana kama sio juzi alisema alienda hosp na kumkuta dimpoz kalazwa mi nadhani tumuamini yule
Hawa watu wenye majina makubwa bongo sio wa kuwaamini

Sent using Jamii Forums mobile app
Yeye alikwenda kama nani? unataka tumuamini yeye ni daktari wake au yeye anajua kuliko maneja?
 
Seven kasema Ommy hayupo ICU ameenda hosp kwa uangalizi wa kawaida ila wabongo tunalazimisha Ommy awe ICU hapo tunatamani tumzushie na kifo ili tupige story mingi za marehemu kua kaumwa hiki na kile na mboyoyo kibao.
Wapo wanazi wanalalama kabisa kwa nini taarifa za ugonjwa zinafanywa siri wakati hata zikiwekwa hadharani hawana msaada zaidi ya kutafuta likes na comments,yupo mtu alinifundisha kuheshimu faragha za mtu mwingine mfano ugonjwa ni ustaarabu wa kawaida kwa mgonjwa kuamua taarifaza za ugonjwa wake zimfikie nani hua nashangaa sana mtu anafyatuka tu fulani ana tezi dume khaaaa kweli Bongo nyoso.
 
Domo ilikuwaje akapost utumbo ule instagram baada ya kusikia Dimpoz yupo ICU ingawa kipindi anaumwa mwanzo hajawahi post..

Ni Habari njema kusikia anaendelea vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…