SFO wanatuchunguzia serikali yetu au yao?

SFO wanatuchunguzia serikali yetu au yao?

Naanza kuhisi kwamba upinzani na JF tunazidi kulalama bila kuchukua hatua. Hivi haiwezekani mtu kufungua mashitaka ili kina Mkapa, Chenge, Yona, Mramba, nk. washitakiwe? Nakasirika sana kuona tukishamaliza kulalama mjadala unafungwa tunahamia kwenye issue nyingine.

Walau kuna matumaini kidogo baada ya wapinzani kupata nuru na kwenda kukagua daftari la mali za viongozi. Je lakini baada ya hapo kuna mkakati wowote wa kuwapeleka mahakamani wakikuta wamedanganya? Au ni hotuba na kusahau jumla wakiahidiwa serikali ya mseto zanzibar? Tuanze sasa jamani kuchukua hatua.
 
Naanza kuhisi kwamba upinzani na JF tunazidi kulalama bila kuchukua hatua. Hivi haiwezekani mtu kufungua mashitaka ili kina Mkapa, Chenge, Yona, Mramba, nk. washitakiwe? Nakasirika sana kuona tukishamaliza kulalama mjadala unafungwa tunahamia kwenye issue nyingine.

Walau kuna matumaini kidogo baada ya wapinzani kupata nuru na kwenda kukagua daftari la mali za viongozi. Je lakini baada ya hapo kuna mkakati wowote wa kuwapeleka mahakamani wakikuta wamedanganya? Au ni hotuba na kusahau jumla wakiahidiwa serikali ya mseto zanzibar? Tuanze sasa jamani kuchukua hatua.

Mkulu,
Hivi hiyo kesi unaifungua mahakama gani, Judge gani ataishulikia, tunaitaji kujenga mazingira kabla hatujafikia sehemu ya kupeleka kesi ya mkapa mahakamani. Mfano mzuri ni kesi ya Marehemu Ditopile, sheria zilipandwa mpaka akapewa dhamana, lakini kuna watu wameua bila kukusudia wana miaka 10 gerezani wala kesi zao hazijaanza kusikilizwa.
 
Back
Top Bottom