Ni miaka 21 imepita tangu Shabani Nonda kuelekea South Africa na baadae kufanikiwa kuvuma sana Ulaya na Dunia nzima. Baada ya Nonda kufahamika tulitetegemea milango itafunguka kwa soka letu na wachezaji wetu kujielewa na kupambana ili kupata mafanikio kama ya Nonda lakini imekuwa ni shida. Mwezi uliopita mganda Emmanuel Okwi amepata nafasi ya kwenda kuanza maisha mapya Denmark hii ikiwa ni nafasi ya pili baada ya Eteol Du Sahel kuisha kwa mizwengwe, Sasa tujiulize Okwi anondoka mara ya pili wazawa kuna hata mmoja anaeonyesha nia?. Labda tuseme ya Okwi makubwa vipi ya Kpha Sherman kacheza mechi 27 na kufunga magoli 6mengi yakiw sio ya ligi Jana kakamilisha mkataba wake na Mpulanga black Acers timu ya ligi kuu PSL bila ya kufanya majaribio, amepimwa afya tu kasaini mkataba. Sasa tujiulize mfungaji bora wa Tanzania msimu uliopita Simoni Msuva alishindwaje majaribio wakati Sherman amepita? na pia vipi kuhusu mchezaji anaeaminika ni kiungo bora Sasa nchini Jonas Mkude nae siku mbili tu karudi tatizo liko wap? Au shida ni mawakala maana naambiwa wakala ndo anamtangaza mchezaji kama bidhaa sokoni na pia kumhudumia tusije tukawa tunawalaumu bure kumbe wanapelekwa sokoni na wahuni tu kama yale ya Kapombe kwenda kushindia maji Ufaransa alafu akakabane na wakina Cisse. Tujiulize jamani tutatue tatizo tusiwe njia tu.