Shabani Kado; anajielewa kweli?

Shabani Kado; anajielewa kweli?

Kwa kweli ni halali adhurumiwe tuu kwa uvaaji ule maana anaonekana bado mtoto na hawezi kunegoshiet chochote kuhusu fedha yake..lakini hili la kuvaa si la singano au kado pekee ni tatizo la kitaifa..hatujui kuvaa kipi katka tukio gani!!!

Mkuu yaani hili ni tatizo na ni kama msiba vile kwa Taifa letu. Yaani hawa Wachezaji wetu wanashindwa hata kuiga kuona wale waliopiga hatua mbele huko Ulaya wanavaaje kwenye matukio muhimu kama haya. Hao wachezaji wa Ulaya wenyewe wakiwa na majeruhi na hawapo kwenye list ya mchezo za Clubs zao wakiwa Jukwaani wanapiga suti za maana sembuse kwenda kwenye vikao.
 
Tatizo wachezaji wa kibongo wengi wanatokea kwenye vijiwe vya bange hakuna mchezaji atakaelelewa kwenye academy kama wenzetu mbele eti anaenda kwenye tuzo au kikao muhimu avae kibangebange kama hawa kina singano,

Pili maisha wanayokulia niyakiswazi sana,kubasii??? Au hujui wanaopenda makubasi!

Hata kama wanatokea Uswazi huko sio kuhalalisha kuvaa hovyo hovyo kama teja. Unapotoka hatua moja kwenda nyingine ni lazima mazingira yakubadilishe utake usitake,unataka kuniambia huko kwenye vilabu vyao hakuna watu wanaovaa kinadhifu mpaka washindwe kuiga?. Tatizo kubwa la hawa wachezaji wa kibongo wanajifanya wao ni Masela Nondo na wanatumia neno ''Umaskini'' kwa malengo yao ya kipuuzi.
 
huyu singano naye kavaa kama chinga tu wa karume au mtaa wa kongo.... inaonesha hata akili yake haipo sawa. naanza kupata shida hata hii issue kuna watu wanamshika tu masikio hana lolote. ameshindwa kuvaa hata suruali akachomekea? hivi hawa wachezaji wetu ina maana hawajifunzi kabisa kwa wenzao wa nje? mbona mazuri hawajifunzi wanajikitika kwenye ya kijinga tu na kuvuta mibhangi? nguo gan hizo mtu anavaa.... anaonekana hayupo serious kabisa,

Mkuu we acha tuu,kama Mkuu IL Capitano alivyosema hapo juu kuwa watu wa aina hii ni halali kabisa kudhulumiwa kwa sababu hawajielewi,hawajithamini na hawajui ni nini wanachokitaka hasa. Umakini na thamani ya Mtu inaanzia kwenye muonekano wake/unadhifu hasa mavazi. Kama unapata hela unashindwa hata kujinunulia nguo na viatu vizuri vitakavyokufanya uwe nadhifu,ya nini kukupa hela nyingine kama sijakudhulumu kabisa sababu haujui matumizi ya hizo hela.
 
Back
Top Bottom