Shabiby mlinzi wa shamba la bibi anayehangaishwa na ngedere

Shabiby mlinzi wa shamba la bibi anayehangaishwa na ngedere

eddy

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2007
Posts
16,054
Reaction score
11,568
Nimekuwa mfuatiliaji wa michango ya huyu mheshimiwa shabiby kule bungeni, nimefurahishwa na namna anavyotetea rasilimali za taifa dhidi ya uhuni uliopachikwa jina la kufungua milango.

Mwanzoni nilijua huyu jamaa ni mchuuzi na mpiga deal wa mjini, aisee kumbe sikujua kuwa ni mtu makini na hazina ya taifa. Nilimsikia namna alivyochangia juu ya upandaji wa bei za mafuta kihuni huni naamini kupitia michango yake serikali iligutuka.

Juzi tena nilimsikia akielezea juu ya hii biashara kichaa ya wachina, kuwa wao wanatuzuia kwenda kwao kuna korona halafu wao wanakuja tena wanaingia kienyeji enyeji, hili liliniingia akilini na kuanza kumfuatilia huyu jamaa aisee kichawani ni mzima, halafu kuna chawa wake anaitwa msukuma, yaani anapokuwa anamwaga nondo huwa anakatizwa na chembeza za taarifa za mh musukuma.

Hongera sana shabiby nitakuja Gairo.
 
Unataka kwenda Gairo kufanya nini sasa! Na wewe unataka kuwa kama Msukuma?
 
Majizi yanasema mafuta ni lazima yaagizwe kwa bulk procurement na si vinginevyo. Shabby anajaribu kuyazuia majizi kujinufaisha, majizi yatashinda tu.
 
Majizi yanasema mafuta ni lazima yaagizwe kwa bulk procurement na si vinginevyo. Shabby anajaribu kuyazuia majizi kujinufaisha, majizi yatashinda tu.

Bulk procurement na majizi[emoji28][emoji28] ubaya wa bulk procurement n upi?
 
Nimekuwa mfuatiliaji wa michango ya huyu mheshimiwa shabiby kule bungeni, nimefurahishwa na namna anavyotetea rasilimali za taifa dhidi ya uhuni uliopachikwa jina la kufungua milango.

Mwanzoni nilijua huyu jamaa ni mchuuzi na mpiga deal wa mjini, aisee kumbe sikujua kuwa ni mtu makini na hazina ya taifa. Nilimsikia namna alivyochangia juu ya upandaji wa bei za mafuta kihuni huni naamini kupitia michango yake serikali iligutuka.

Juzi tena nilimsikia akielezea juu ya hii biashara kichaa ya wachina, kuwa wao wanatuzuia kwenda kwao kuna korona halafu wao wanakuja tena wanaingia kienyeji enyeji, hili liliniingia akilini na kuanza kumfuatilia huyu jamaa aisee kichawani ni mzima, halafu kuna chawa wake anaitwa msukuma, yaani anapokuwa anamwaga nondo huwa anakatizwa na chembeza za taarifa za mh musukuma.

Hongera sana shabiby nitakuja Gairo.
Anawaponda wachina sababu wanatoka bara moja yeye ni mhindi
 
Back
Top Bottom